43959 UTEKELEZWAJI WA MKAKATI WA KUONGEZA UWAZI KATIKA TASNIA YA UZIDUAJI MATUMIZI YA MAFUNZO YA AWALI KUTOKA KWENYE MAENEO YA UTENDAJI EITI ni mkakati wa kidunia ulioanzishwa mnamo mwaka 2002 ili kuinua na kuunga mkono maboresho ya utawala kwa nchi zenye utajiri wa rasilimali kwa kuchapisha na kuelezea malipo toka kwa makampuni na mapato ya serikali yatokanayo na mafuta, gesi na madini. Kama umoja wa kujitolea wa washikadau wenye lengo moja, muundo wa mkakati wa EITI kidunia umekuwa wazi na shirikishi ukihusisha wigo mpana wa washikadau. Bodi ya EITI inasimamia mkakati, pamoja na mwenyekiti na wanachama waliochaguliwa wanaowakilisha nchi zenye utajiri wa rasilimali; wahisani na nchi zinazounga mkono; makampuni ya kitaifa na kimataifa yanayojihusisha na shughuli za mafuta, gesi na madini; wanachama wa vyama vya kijamii na wawakilishi wa wawekezaji. Wakala wa maendeleo wa kimataifa kama Benki ya Dunia, Shirika la Fedha la Dunia, na Benki ya Maendeleo ya Afrika wanahudhuria kwenye vikao vya bodi ya EITI kama watazamaji. Sekretarieti iliyopo Oslo, Norway inaunga mkono shughuli za bodi ya EITI na kuratibu shughuli za EITI kwa ujumla. Taarifa zaidi za mkakati, bodi na sekretarieti zinaweza kupatikana kwenye http://www.eitransparency.org. Mfuko wa Hisani kwa ajili ya EITI Kuhusu suala na malengo ya EITI kidunia yaliyoelezewa hapo juu, Benki ya Dunia inasimamia mfuko wa hisani ambao unasaidia kuunga mkono msaada wa kifedha na utaalamu toka kwa makundi ya Benki ya Dunia kwa nchi zinazotekeleza EITI na ufahamu wa EITI kidunia. Kuanzia mwezi Novemba mwaka, 2007 nchi zilizochangia kwenye mfuko wa hisani ni kama zifuatazo:- Australia, Ubeligiji, Canada, Ufaransa, Ujerumani, Uholanzi, Norway, Hispania, Umoja wa Ulaya na Uingereza -- mwanzilishi wa uchangiaji huu. Msaada wa mfuko wa hisani kwenye kutengenezwa kwa ripoti hii unatambuliwa na kushukuriwa sana. I Muhimu Ripoti hii ina lengo la kuchukua baadhi ya mambo ya kipekee katika utekelezaji masomo yaliyofunzwa kutoka kwa nchi zinazo tekeleza EITI. Ripoti hii inatazamiwa kutoa muongozo muhimu na kuchokoza mijadala zaidi kuhusu aina za utekelezaji baina ya watengeneza sera wa serikali; makundi ya vyama vya kijamii; makampuni ya mafuta, gesi na madini; wakala wa wahisani; na wadau wengine wanaohusika katika mkakati. Hata hivyo, ni lazima ifahamike kuwa kanuni za EITI, vigezo vya EITI na "Muongozo wa uthibitishwaji wa EITI" (na matangazo mengine ya Bodi ya EITI) ­ ukiachilia mbali ripoti hii ndio vyanzo vya sera ya taifa ya EITI ambayo inatengeneza viwango vilivyokubalika ambavyo ni lazima vifikiwe na nchi zenye msimamo na zinazotekeleza EITI. II UTEKELEZWAJI WA MKAKATI WA KUONGEZA UWAZI KATIKA TASNIA YA UZIDUAJI MATUMIZI YA MAFUNZO YA AWALI KUTOKA KWENYE MAENEO YA UTENDAJI III UTEKELEZWAJI WA MKAKATI WA KUONGEZA UWAZI KATIKA TASNIA YA UZIDUAJI MATUMIZI YA MAFUNZO YA AWALI KUTOKA KWENYE MAENEO YA UTENDAJI IV ©2008 Benki ya Kimataifa ya Maboresho na Maendeleo / Benki ya Dunia 1818 H Street NW Washington DC 20433 Simu: 202-473-1000 Mtandao: www.worldbank.org Barua pepe: feedback@worldbank.org Haki zote zimehifadhiwa 1 2 3 4 5 11 10 09 08 Juzuu hii ni kazi iliyofanywa na wafanyakazi wa Benki ya Kimataifa ya Maboresho na Maendeleo / Benki ya Dunia. Tafsiri, yaliyogunduliwa na mahitimisho ya juzuu hii hayana uhusiano wa moja kwa moja na mawazo ya wakurugenzi wa Benki ya Dunia au serikali wanazo ziwakilisha. Benki ya Dunia haitoi garantii ya data zilizomo kwenye kazi hii. Mipaka, rangi, viwango, na taarifa zingine zilizoonyeshwa kwenye ramani yeyote ya kazi hii hazi maanishi maamuzi yeyote kwa upande wa Benki ya Dunia kuhusu hali ya kisheria ya tawala yeyote au kupitishwa au kukubalika kwa mipaka hiyo. Haki na Ruhusa Mambo yaliyomo kwenye chapisho hili yana haki ya umiliki. Unakili au uhamishaji wa sehemu au kazi nzima bila ruhusa ni uvunjaji wa sheria husika. Benki ya Kimataifa ya Maboresho na Maendeleo / Benki ya Dunia inahimiza usambazwaji wa kazi hii na itatoa ruhusa ya kuchapishwa kwa sehemu za kazi hii itakapobidi. Kwa ruhusa ya kudurusu au kunakili sehemu yeyote ya kazi hii, tafadhari tuma maombi yakiambatana na taarifa kamili kwa Kitengo cha Usimamizi wa Haki za Unakili Inc., 222 Rosewood Drive, Danvers, MA 01923, USA; Simu: 978-750-8400; faksi: 978-750-4470; Mtandao: www.copyright.com. Maulizo mengine yote juu ya haki na leseni ikijumuisha haki ndogo ndogo yapelekwe kwa Ofisi ya mchapishaji, The World Bank, 1818 H Street NW, Washington, DC 20433, USA; fax: 202-522-2422; e-mail: pubrights@worldbank.org. ISBN-13: 978-0-8213-7501-3 eISBN-13: 978-0-8213-7502-0 DOI: 10.1596/978-0-8213-7501-6 Maombi ya Data za uchapishaji za Librari ya Kongresi yamepelekwa V YALIYOMO ORODHA YA MASANDUKU ................................................................................................................IX ORODHA YA PICHA...............................................................................................................................IX ORODHA YA MAJEDWALI..................................................................................................................IX SHUKRANI................................................................................................................................................XI VIFUPISHO NA MAANA ZA MANENO YA EITI.............................................................................XII UTANGULIZI ........................................................................................................................................... xv MADHUMUNI YA RIPOTI......................................................................................................................... xv NCHI ZILIZOJIUNGA NA EITI MPAKA NOVEMBA 1, 2007 ........................................................................xvi MIONGOZO NA VIGEZO VYA EITI...........................................................................................................xvii KITABU CHA MAREJEO CHA EITI KAMA MUONGOZO.............................................................................xix MUONGOZO WA UTHIBITISHAJI EITI ......................................................................................................xix KAZI YA BENKI YA DUNIA ........................................................................................................................xix SURA 1: KUANZA PROGRAMU YA EITI...........................................................................................1 MANUFAA YA UTEKELEZAJI WA EITI.........................................................................................................1 NCHI ZINAZO TEKELEZA EITI......................................................................................................................3 KUJENGA MAKUBALIANO KWENYE EITI....................................................................................................4 KUJIUNGA NA EITI NA HATUA ZA KWANZA ..............................................................................................5 KAULI YA PAMOJA JUU YA KUJIUNGA NA EITI..........................................................................................5 SURA 2: WADAU NA MFUMO WA UTAWALA................................................................................8 UTANGULIZI ..............................................................................................................................................8 WADAU WANAOHUSISHWA.....................................................................................................................8 MAKUNDI VIONGOZI YA WASHIKADAU NA UTAWALA WAKE................................................................10 MAMBO MENGINE YA KUZINGATIA .......................................................................................................13 KAZI ZA MAKUNDI VIONGOZI YA WADAU .............................................................................................. 14 VI SURA 3: UPAMBANUZI WA MIPAKA YA PROGRAMU YA EITI...............................................17 UTANGULIZI ............................................................................................................................................17 MAMBO YANAYO ZINGATIWA WAKATI WA KUTENGENEZA WIGO WA PROGRAMU YA EITI................19 MAJADILIANO KUHUSU MALIGHAFI .......................................................................................................26 MJADALA KUHUSU KIASI CHA WINGI NA UPUNGUFU ...........................................................................29 MALIPO NA MAPATO KWA SERIKALI NDOGO.........................................................................................30 UGATUAJI MADARAKA............................................................................................................................30 SEKTA SAIDIZI NA BIASHARA ZINGINE ZIHUSUZO MAFUTA, GESI NA MADINI.......................................32 KUTOFAUTISHA KATI YA EITI HALISI NA "EITI YA ZIADA"........................................................................35 SURA 4: KUUANDAA MPANGO WA KAZI WA EITI ....................................................................38 UTANGULIZI ............................................................................................................................................38 UUNDAJI NA USHAURI JUU YA MPANGO WA KAZI WA EITI...................................................................38 MUDA WA UTEKELEZAJI..........................................................................................................................42 UFADHILI WA PROGRAMU YA EITI..........................................................................................................42 SURA 5: KAZI YA SERIKALI KWENYE UTEKELEZAJI WA EITI ............................................46 UTANGULIZI ............................................................................................................................................46 KUTOA MUONGOZO WA KISIASA NA KUUNGA MKONO MCHAKATO WA EITI......................................46 KUJENGA UWEZO KWA KITENGO CHA UTEKELEZAJI NA WAKALA WA SERIKALI....................................48 KUHAKIKISHA USHIRIKI WA JUMLA WA KAMPUNI NA MAMBO YA USIRI..............................................49 KUWEKA MISINGI YA KISHERIA YA UTEKELEZAJI ....................................................................................50 KUWEKA WAZI MAPATO YA SERIKALI.....................................................................................................52 SURA 6: KAZI YA MAKAMPUNI NA VYAMA VYA KIJAMII.......................................................53 UTANGULIZI ............................................................................................................................................53 KUSAIDIA UANZISHWAJI WA HARAKA WA MCHAKATO WA EITI NA KUONGOZA MKAKATI..................53 KUSAIDIA KUPANGILIA MIPAKA YA EITI, URIPOTI NA UWEKAJI WAZI WA MAMBO YA EITI ..................54 VII UWASILISHWAJI WA MATOKEO YA EITI..................................................................................................54 KUJENGA UWEZO....................................................................................................................................55 SURA 7: UANDAAJI WA RIPOTI YA EITI.......................................................................................57 UTANGULIZI ............................................................................................................................................57 KUCHAGUA MSIMAMIZI (AU MKAGUZI, KAMA HALI IKO HIVYO) ..........................................................57 HADIDU ZA REJEA KWA MSIMAMIZO (MKAGUZI) NA MAMBO YANAYOTAKIWA KUWEMO KWENYE RIPOTI YA EITI..........................................................................................................................................58 UKUMBUSHO KWENYE MUUNDO WA KURIPOTI WA EITI......................................................................63 MUHTASARI WA UHUSIANO KATI YA VIWANGO VYA KIMATAIFA VYA UKAGUZI NA VIGEZO VYA EITI.64 SURA 8: USAMBAZWAJI WA EITI...................................................................................................66 UTANGULIZI ............................................................................................................................................66 MIKAKATI YA KAWAIDA YA MAWASILIANO NA VIFAA ...........................................................................66 SURA 9: MATOKEO: TATHMINI NA USIMAMIZI WA PROGRAMU ZA EITI .......................69 UTANGULIZI ............................................................................................................................................69 KUSIMAMIA NA KUTATHMINI UTENDAJI UNAOANZA............................................................................69 SURA 10: MUUNDO WA KIMATAIFA WA EITI.............................................................................71 UTANGULIZI ............................................................................................................................................71 MUUNDO WA UTAWALA WA EITI KIMATAIFA .......................................................................................71 KAZI YA MASHIRIKA YA MAENDELEO YA KIMATAIFA KWENYE BODI YA EITI .........................................73 SURA 11: USHAHIDI UNAOIBUKA JUU YA MADHARA YA PROGRAMU YA TAIFA YA EITI ............................................................................................................................................................74 MATOKEO YANAYOIBUKA JUU YA PROGRAMU YA EITI..........................................................................74 SURA 12: HITIMISHO: VIGEZO MUHIMU KWENYE PROGRAMU YA EITI ILIYOFANIKIWA .....................................................................................................................................76 MAMBO MUHIMU KATIKA RIPOTI HII.....................................................................................................76 KIAMBATISHO A: HAIDROKABONI ­ NA NCHI TAJIRI ZA MADINI.....................................79 KIAMBATISHO B: MCHAKATO WA KUHALALISHA EITI.........................................................84 VIII UFUPISHO WA MCHAKATO WA UHALALISHAJI WA EITI NA VIASHIRIA VYAKE......................................85 KIAMBATISHO C: SAMPULI YA MATOKEO YA MFUMO WA UPIMAJI WA EITI (NA VIASHIRIA) ..............................................................................................................................................90 KIAMBATISHO D: NYENZO MUHIMU............................................................................................93 VIELEZO ..................................................................................................................................................97 ORODHA YA MASANDUKU Sanduku 1.1: Nchi za EITI mpaka Novemba 1, 2007...........................................XVI Sanduku 1.2: Kanuni na Taratibu za EITI..........................................................XVII Sanduku 2.1: Wadau wanaohusishwa katika mchakato wa EITI..............................8 Sanduku 2.2: Makampuni yanayomilikiwa na serikali...........................................10 Sanduku 2.3: Wakala wa Maelewano/ Hadidu za rejea .........................................13 Sanduku 3.1: Mitazamo tofauti kwenye nchi zinazozalisha mafuta, gesi na madini.19 Sanduku 3.2: Aina nyingine ya ukaguzi................................................................24 Sanduku 4.1: Mambo yaliyomo kwenye mpango wa kazi........................................40 Sanduku 8.1: Zana muhimu za mawasiliano kwa EITI.............................................67 ORODHA YA PICHA Picha 3.1: Viwango vya malipo na makampuni .........................................................27 Picha 3.2: Mkusanyo wa makampuni na malipo........................................................31 Picha 7.1: Mchakato wa kuripoti EITI........................................................................61 Picha 10.1: Muundo wa utawala wa kimataifa wa EITI.............................................72 ORODHA YA MAJEDWALI Jedwali 3.1: Kutofautisha kati ya EITI halisi na "EITI ya Ziada"...........................36 Jedwali 4.1: Mfano wa bajeti ya EITI iliyorahisishwa kwa mwaka...........................45 Jedwali A.1: Nchi tajiri kwa haidrokaboni ....................................................80 IX Jedwali A.2: Nchi tajiri kwa madini ..............................................................83 VIAMBATISHO VILIVYO KWENYE CD ILIYOAMBATANISHWA Kiambatisho A: Dondoo toka kwenye Hadidu za Rejea za utafiti wa awali wa EITI ­ Zambia Kiambatisho B: Waraka wa maelewano juu ya utekelezaji wa EITI ­ Azerbaijan Kiambatisho C: Mpangilio wa EITI ­ Guinea Kiambatisho D: Agizo kwa kundi tekelezi la washikadau ­ Peru Kiambatisho E: Dondoo toka kwenye Ripoti ya awali ­ Ghana Kiambatisho F: Mpango wa kazi wa EITI ­ Timor Leste Kiambatisho G: Hadidu za Rejea za Halmashauri ya EITI ­ Mongolia Kiambatisho H: Sheria ya EITI (Uzalishwaji wa marudio ­ Nigeria Kiambatisho I: Sampuli ya Hadidu za Rejea kwa ajili ya msimamizi wa EITI ­ Kameruni Kiambatisho J: Sampuli ya kiolezo cha ripoti za EITI ­ Ghana (Uchimbaji madini) na Kazakhstan (mafuta) Kiambatisho K: Kitabu cha marejeo cha EITI Kiambatisho L: Muongozo wa Uthibitishwaji wa EITI Kiambatisho M: Sampuli ya Ripoti za EITI zilizochapishwa hivi karibuni kutoka Novemba 1, 2007 a. Azerbaijan b. Kameruni c. Gaboni d. Ghana e. Guinea f. Jamuhuri ya Kyrgyz g. Mauritania h. Nigeria X SHUKRANI Msaada wa wabia toka kwa nchi tekelezi za EITI katika kutengeneza ripoti hii unashukuriwa sana. Mwandishi kiongozi wa ripoti hii ni Sefton Darby wa Idara ya mafuta, Gesi, Madini na Madawa wa Benki ya Dunia, Kitengo cha Sera na Utendaji. Ripoti imepata muongozo na michango toka kwa wafanya kazi wa kitengo cha COCPO na zaidi. Ripoti ilipitiwa kwa ufasaha na Clive Armstrong (Umoja wa Fedha Duniani) na Charles McPherson (shirika la Fedha Duniani). Pia michango muhimu ilitoka kwa Anwar Ravat, Craig Andrews, Marianne Bergstrom, Boubacar Bocoum, Michael Levitsky, and Eleodoro Mayorga ­ Alba ya COCPO, pamoja na Yerlan Akishev (Benki ya Dunia Khazakhstan), Henri Laurent Bateg (Benki ya Dunia Cameroon), David Brown (Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ­ Uingereza ­ DFID/ Benki ya Dunia Indonesia), Allison George (DFID ­ Siera Leon), Faustin ­ Ange Koyasse (Benki ya Dunia Cammeroon), Kristian Lempa (GTZ ­ Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo), Fridolin Ondobo (Benki ya Dunia Cameroon), Anton Op De Beke (Shirika la Fedha Duniani) na Stan Perri (Sekretarieti ya EITI Nigeria). Utengenezwaji wa ripoti ulifadhiliwa na Esther Petrilli ­ Massey COCPO. Makamu wa Raisi, Mtandao wa maendeleo endelevu: Kathy Sierra Mkurugenzi, Idara ya mafuta, gesi, uchimbaji madini na madawa: Somit Varma Meneja, Kitengo cha utendaji na Sera (COCPO): Paulo De Sa Meneja wa Programu/ Kiongozi wa timu, EITI (COCPO): Anwar Ravat XI VIFUPISHO NA MAANA ZA MANENO YA EITI Bodi ya EITI: Bodi ya Kimataifa inayosimamia mambo ya EITI kidunia. Bodi inajumuisha wawakilishi toka serikali zinazotekeleza EITI, wahisani, makampuni ya uziduaji, wawekezaji na makundi ya vyama vya kijamii. EITI: Mkakati wa kuongeza Uwazi katika Tasnia ya Uziduaji. Kanuni za EITI: Itikadi za uanzilishi wa mkakati. Zinaweza kupatikana kwenye http://www.eitransparency.org/eiti/principles Kusanyiko: Njia ya kuripoti ambayo malipo yaliyotolewa na kampuni moja moja yana jumuishwa ili malipo ya kampuni moja moja yasitambuliwe kwenye ripoti ya EITI/ na au pale malipo ya aina mbali mbali yaliyofanywa na kampuni yanajumuishwa kwa namna ambayo malipo yaliyofanywa na kampuni hayatambuliwi. MDTF: Mfuko wa hisani wa wafadhili (Unaosimamiwa na Benki ya Dunia) ambao wafadhili mbali mbali wamechangia. Mfuko wa hisani unatoa misaada ya kitaalam na fedha kwa nchi zinazotekeleza ama zinazofikiria kujiunga na EITI. Mkaguzi: Huduma ya kitaalam inayochunguza na kutoa mapendekezo ya kikaguzi (ama "kupitishwa" au "kutokupitishwa") kwa makampuni au serikali au matamko ya fedha ya vitengo vingine (na katika baadhi ya matukio matamko yanayohusiana na kiwango cha uzalishaji) mkaguzi ataamua kama matamko hayo ya fedha yanatoa mtazamo wa kweli na haki au yamewasilisha kisahihi kulingana na viwango vya uwasilishaji wa ripoti za fedha. Kazi ya ukaguzi inafanyika pamoja na viwango vya ukaguzi vilivyokubalika kimataifa (angalia ukurasa unaofuata) Msimamizi/ Mlinganishaji: Shirika (kwa kawaida kampuni ya ukaguzi) lililoteuliwa kwa ajili ya kupitia data za malipo na mapato zilizotolewa na makampuni na serikali. Katika hali hii kampuni halifanyi ukaguzi bali linapitia na kuzichunguza data (za fedha na itakapobidi kiwango cha uzalishaji) na kuchunguza tofauti zozote zitakazojitokeza. Muhimu/ Umuhimu: Kipimo cha kiwango kinachotumika kuamua kama malipo ya kampuni yana umuhimu kwenye matokeo, yaani yanaathiri matokeo kama yakijumuishwa au yasipojumuishwa. Nchi zinazotekeleza EITI zinaweka ngazi za umuhimu kwa kuzingatia ukubwa wa kampuni au malipo. Umuhimu wa malipo ya kampuni utaelezea ukubwa wa kampuni ambapo juu ya kiwango XII hicho makampuni yatatakiwa kushiriki kwenye mchakato wa EITI kitaifa. Umuhimu wa kimalipo utaelezea kiasi cha malipo ambapo malipo hayo yatajumuishwa kwenye mchakato wa EITI. Nchi Tahiniwa: Nchi ambayo imeahidi kwa uma kutekeleza EITI na imetimiza viashiria vinne vya kwanza vya uthibitishwaji. Nchi Tiifu: Nchi ambayo imetekeleza EITI kikamilifu na imepitia uthibitishwaji wa nje uliofanikiwa pamoja na viashiria uthibitishwaji wa EITI. Sekretarieti ya EITI (Kimataifa): Sekretarieti yenye makazi yake Oslo, Norway, inaunga mkono kazi za bodi ya EITI na inatumika kama sehemu ya kwanza ya mawasiliano kwa washikadau wote wanaojihusika na EITI duniani. Tawanyiko: Njia ya kuripoti ambayo malipo yaliyotolewa na kampuni moja moja (kwa mfano kodi, mrahaba na kadharika) yana wekwa bayana na yanayoweza kutambuliwa katika ripoti ya EITI. Uthibitishaji: Mchakato uliokubalika ambao maendeleo ya utekelezwaji wa EITI wa nchi unapimwa kwa kuzingatia vigezo vya EITI. Maelezo zaidi juu ya mchakato wa uthibitishwaji yanaweza patikana kwenye: http://www.eitransparency.org/document/validationguide. Vigezo vya EITI: Vigezo sita vilivyokubalika kimataifa ambavyo vinaelezea matokeo ya chini kabisa ya program ya EITI iliyofanikiwa. Vinaweza kupatikana kwenye http://www.eitransparency.org/eiti/criteria. Viwango vya Ukaguzi vya Kimataifa: Viwango vya kimataifa vya kitaaluma na kimaadili vilivyokubalika kwa shughuli za ukaguzi na uhakika wa huduma kwamba makampuni ya kitaaluma ya mahesabu na ukaguzi yanazitumia na kuzifuaata katika kazi zao za kitaaluma karibu nchi zote ama katika kutii sheria za ndani au kwa kufuata ahadi za kitaaluma chini ya Bodi za kitaifa za mahesabu na ukaguzi. Bodi hizi za kitaifa Pia ni wanachama wa Shirikisho la Kimataifa la Wanamahesabu za Fedha - IFAC, lenye makazi yake New York, USA, ambayo inatoa viwango vya kimataifa vya ukaguzi (kwa kupitia Bodi yake ya Ukaguzi na Uhakika ya Viwango ya Kimataifa -- IAASB) kwa ajili ya kutumiwa na wanachama wote wa IFAC. Vyama vya Kijamii: Neno pana linalotumika kuelezea mashirika yasiyo ya kiserikali na yasiyo rasmi ­ kwa mfano, vyombo vya habari, vyama vya XIII wafanyakazi, makundi ya kidini, wasomi, wanazuoni,na kuendelea. Vyama vya kijamii ni vipana na vimetawanyika, kwa kawaida vinawakilisha kwa mapana wadau mbali mbali. Washikadau/ Kundi Kiongozi: Chombo muhimu cha maamuzi katika mchakato wa EITI kitaifa; kinaongoza na kusimamia utekelezaji wa EITI katika nchi husika. Kundi hili la washikadau mbalimbali linajumuisha wawakilishi wa serikali, makamapuni ya uziduaji na vyama vya kijamii. XIV UTANGULIZI EITI ilizinduliwa mwaka, 2002 kwa madhumuni ya kuendeleza na kudumisha uwazi na uwajibikaji kwa nchi zenye utajiri wa malighafi1 za mafuta, gesi na madini. Toka kuanzishwa kwake EITI nchi kadhaa zimejiunga na kuweza kutoa na kuchapisha ripoti za EITI. Tangu Mwaka, 2004 Benki ya Dunia ikishirikiana na mashirika yanayotoa misaada duniani yaliungana kusaidia utekelezaji wa malengo ya EITI, EITI yenyewe pamoja na mashirika mengine ya misaada ndio yamekuwa chanzo cha msingi cha misaada ya kiufundi na fedha kwa nchi zinazojiunga na EITI. Nchi zenye utajiri wa rasilimali za mafuta, gesi na madini zimefanikiwa kuitumia EITI kama njia ya kuonyesha msimamo wa serikali katika kudumisha utawala bora, kuongeza umakini katika makusanyo ya mapato na kuboresha mazingira ya uwekezaji ya nchi husika. MADHUMUNI YA RIPOTI Ripoti hii inajumuisha taarifa ya mambo yaliyojitokeza2 na vitu ambavyo nchi zilizokuwa zinajiunga na EITI zilijifunza, na vile vile kwa yale mambo ambayo timu ya Benki ya Dunia walikutana nayo wakati wa kusaidia utekelezwaji wa EITI. Mambo yaliyomo katika ripoti hii ni mtazamo wa awali tu, kwa kuwa katika nchi nyingi zilizojiunga na EITI mchakato wa utekelezaji ndio unakua. Baadhi ya nchi zimetengeneza ripoti, lakini uchanganuzi wake bado uko kwenye hatua za awali. Inategemewa, kuwa ripoti hii itakuwa chachu ya majadiliano zaidi juu ya njia za utekelezaji kwa watengeneza sera; vyama vya 1Katika muktadha wa EITI "utajiri wa rasilimali" unarejea kwenye nchi inayotegemea tasnia ya uziduaji. Angalia kiambatisho A. 2Katika ripoti hii hatuja zichambua nchi maalum ambazo zimetekeleza vipengele tofauti vya EITI. Viambatanisho vya repoti hii (kwenye CD iliyo ambatanishwa) ina mifano ya nchi zilizo tekeleza vipengele tofauti vya EITI. xv kiraia; makampuni ya mafuta, gesi, madini na mashirika ya misaada yanayojihusisha na mchakato huu3. NCHI ZILIZOJIUNGA NA EITI MPAKA NOVEMBA 1, 2007 Mpaka sasa nchi ambazo zimejiunga na EITI kwa uwazi zimeorodheshwa kwenye sanduku namba 1.1. Kufikia Novemba 1, 2007 jumla ya nchi 29 duniani zilikuwa zimeishajiunga na EITI, kati ya hizo nchi 15 zinatambuliwa rasmi na EITI na bodi ya EITI (angalia majadiliano kuhusu upitishwaji kwa matabaka ya nchi). Jumla ya nchi 8 mpaka hivi sasa, ndizo zimepiga hatua kwenye mchakato wa EITI hadi kufikia kuandaa ripoti ya EITI moja au zaidi, nchi hizi zimeweza kutoa ripoti zake hadharani na kuweza kujadiliwa kwa uwazi. Kuna uwezekano mkubwa kuwa kundi la kwanza la nchi zitakazojiunga baadae litaweza kufanya vizuri zaidi. SANDUKU 1.1 NCHI ZA EITI MPAKA NOVEMBA 1 MWAKA 2007. AFRIKA ASIA YA MASHARIKI Botswana Mongolia^ Cameroon^* Timor-Leste Chad Congo, Dem. Rep. of ULAYA NA ASIA YA KATI Congo, Rep. of Azerbaijan^* Cote d' Ivoire Kazakhstan^ equatorial Guinea KyrgzRepublic^* Gabon^* Ghana^* Norway Guinea^* Liberia^ AMERIKA YA KUSINI NA CARIBEAN Madagascar Bolivia Mali^ colombia Mauritius^* Peru^ Niger^ Trinidad and Tobago Nigerai^* Sao Tome and principe MIDDLE EAST Sierra Leone Yemen^ 3Maoni yoyote kuhusu ripoti hii yanakaribishwa na yatumwe kwa barua pepe, ogmc@worldbank.org xvi MIONGOZO NA VIGEZO VYA EITI Miongozo ya EITI ilianzishwa mwaka, 2003 kwenye Kongamano la kwanza la mkakati huu, na wakati huo ndipo kanuni na miongozo ya EITI ilipotengenezwa. Miongozo hii ilipitishwa na wadau wote wanaounga mkono EITI. Kanuni za EITI zilipitishwa mnamo mwaka, 2005 kwenye Kongamano la pili la EITI, kwa makubaliano ya wote na kuwekwa vigezo vya chini kwa nchi zote zinazo tekeleza EITI; Kanuni hizi zinajumuisha kwa ufupi maelezo juu ya matokeo ya kujiunga na mchakato wa EITI. SANDUKU 1.2 KANUNI NA TARATIBU ZA EITI KANUNI ZA EITI (2003) Tunaamini kwamba matumizi bora ya utajiri utokanao na maliasili ni kigezo muhimu cha kuwa na uchumi endelevu ambao utachangia 1 kwenye maendeleo na upunguzaji wa umaskini, lakini kama hazita simamiwa kiusahihi, zinaweza kupelekea madhara katika uchumi na jamii. Tunakubali kuwa usimamizi wa maliasili kwa manufaa ya wananchi 2 wa nchi fulani uko chini ya serikali husika na utafanyika kwa manufaa ya maendeleo ya taifa. Tunatambua kuwa manufaa yatokanayo na uziduaji wa rasilimali 3 yanatokea kama njia za mapato kwa miaka mingi na inategemea sana kwenye bei. Tunatambua kuwa uelewa wa jamii juu ya mapato na matumizi ya 4 serikali baada ya muda utasaidia mijadala ya kijamii na kutoa taarifa juu ya njia sahihi na ya uhakika kwa maendeleo endelevu. Tunasistiza umuhimu wa uwazi kwa serikali na makampuni katika 5 tasnia ya uziduaji na uhitaji wa kusisitiza usimamizi wa fedha na uwajibikaji 6 Tunatambua kuwa mafanikio ya uwazi wa hali ya juu lazima uandaliwe katika misingi ya kuheshimu mikataba na sheria. 7 Tunatambua kwamba uwazi katika mambo ya kifedha utaleta mazingira bora kwa uwekezaji wa ndani na nje. xvii 8 Tunaamini kanuni za serikali za utendaji wa uwajibikaji kwa wananchi wote kwa usimamizi wa mapato na matumizi ya taifa. 9 Tunaahidi kuhimiza uwazi na uwajibikaji wa hali ya juu kwenye maisha ya jamii, shughuli za serikali na biashara. 10 Tunaamini kwamba inahitajika njia thabiti, inayotekelezeka na rahisi kutumia kwa kuweka bayana malipo na mapato. 11 Tunaamini kuwa kuweka wazi malipo kwa nchi husika, itatakiwa ishirikishe makampuni yote ya uziduaji nchini humo. Katika kutafuta suluhu, tunaamini kwamba wadau wote wana nafasi muhimu na husika za kuchangia - ikijumuisha serikali na taasisi 12 zake, vyanzo vya uziduaji, viwanda vya watoa huduma, mashirika ya kijamii, mashirika ya kifedha, wawekezaji na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali. VIGEZO VYA EITI (2005) Uchapishwaji wa mara kwa mara wa malipo ya makampuni ya 1 mafuta, gesi na madini kwa serikali na mapato yote yanayopokelewa na serikali kutoka kwa makampuni ya mafuta, gesi na madini kwa wasomaji wengi yenye kufikika kirahisi na yanayoeleweka Kwa zile sehemu ambazo ukaguzi huo bado haujaanzishwa, malipo 2 na mapato ni suala la ukaguzi wa kujitegemea unaokubalika na wenye kutumia taratibu za kimataifa. Malipo na mapato yana hakikiwa na msimamizi wa kujitegemea anae 3 kubalika, mwenye kutumia njia za ukaguzi za kimataifa na kwa kuchapisha mapendekezo ya msimamizi kutokana na uhakiki huo, ikijumuisha hitilafu yeyote itakayogundulika. 4 Njia hii itajumuisha makampuni yote yakiwemo yale yanayomilikiwa na serikali. Vyama vya kijamii vitahusishwa kama washiriki katika kutengeneza, 5 kuendeleza na kukagua mchakato huu na kuchangia kwenye mjadala wa jamii. 6 Njia hii itajumuisha makampuni yote yakiwemo yale yanayomilikiwa na serikali. Serikali itatengeneza mpango endelevu wa kazi ambao utakuwa na uchumi wa kudumu, na msaada kutoka kwa taasisi za fedha za 7 kimataifa pale utakapohitajika, ukijumuisha vipimo vya malengo, ratiba ya utekelezaji na makadirio ya vikwazo vyenye uwezekano wa kutokea. xviii KITABU CHA MAREJEO CHA EITI KAMA MUONGOZO Kutoa muongozo kwa nchi zinazotaka kutekeleza au tayari zinatekeleza, EITI, sekretarieti ya EITI ilichapisha kitabu cha mrejesho nyuma mnamo mwaka, 2005; kinajumuisha vigezo na taratibu za EITI. Ifahamike kwamba vigezo vya EITI ni kipimo cha chini kabisa. Baadhi ya nchi zimeamua kutengeneza vigezo vya EITI vinavyokwenda juu ya vile vilivyoshauriwa na sekretarieti. Kitabu kizima cha marejeo kimeambatanishwa kwenye CD-ROM. MUONGOZO WA UTHIBITISHAJI EITI Mwaka, 2006, "muongozo wa uthibitishaji EITI"4 uliandaliwa na kukubalika. Muongozo huu unaelezea kwa undani viwango ashiria kwenye vigezo vya EITI, vitakavyotumika na mthaminishaji wa kujitegemea kuchunguza utekelezaji wa EITI katika nchi husika. Bodi ya EITI iligundua kuwa uthaminishaji ni tukio la kujitegemea ambalo nchi zote za EITI zitahitaji kupitia miaka miwili ili kutengeneza utaratibu ulio sawia wa kukadiria utekelezaji wa EITI. Matokeo ya uthaminishaji wa nchi yatakuwa yakiidhinishwa na Bodi ya EITI na itaamua kama nchi imetimiza vigezo vyote vya EITI (na inatii EITI) au inaendelea kusonga mbele ( na ni watahiniwa wa EITI). Kiambatisho B kinaelezea kwa ufupi muongozo wa uthibitishaji na viashilia uthibitishaji. Muongozo mzima wa uthibitishaji umejumuishwa kwenye CD- Rom inayoambatana na ripoti hii. KAZI YA BENKI YA DUNIA Benki ya Dunia ilirasimisha EITI mnamo mwaka, 2003, Benki ya Dunia ili idhinisha EITI, na imekuwa ikiunga mkono mkakati mzima wa EITI duniani na nchi kwa kupitia shughuli mbali mbali tangu mwaka, 2004, hii inajumuisha kusimamia mfuko wa dhamana wa wafadhili ambao unatoa misaada ya kifedha na kiufundi kwa nchi zilizo au zinazotaka kutekeleza EITI. Msaada huu unajumuisha yafuatayo:- kuwawezesha washauri na wataalam wa EITI kusaidia serikali kwenye utekelezaji; kubadilishana uzoefu wa kiutendaji wa 4Kitabu cha marejeo cha EITI na Muongozo wa Uthibitishaji EITI vinapatikana: http://www.eitranspatency.org/document/validationguide. xix kimataifa (ikijumuisha ripoti hii); na kutoa misaada ya kifedha kwa serikali kwa ajili ya utekelezaji wa EITI. Benki ya Dunia inaitumia EITI kama muitikio wao katika kuipitia tasnia ya uziduaji5 na pia kama njia mojawapo iliyochaguliwa na Benki kama mkakati wa kurekebisha utawala na kupambana na rushwa. Katika mtizamo huu benki pia inafanya kazi na serikali katika kuandaa mkakati madhubuti wa kurekebisha tasnia ya uziduaji, usimamizi wa maliasili, na utawala bora/ mapambano dhidi ya rushwa. Benki pia imetoa misaada mbali mbali ya kifedha kwa vyama vya kijamii vinavyojihusisha na utekelezaji wa EITI katika nchi zinazo tekeleza EITI. 5http://www.worldbank.org/ogmc. xx SURA 1: KUANZA PROGRAMU YA EITI MANUFAA YA UTEKELEZAJI WA EITI EITI ni kipimo cha dunia katika kuinua uwazi na uwajibikaji kwenye malipo na mapato ya nchi tajiri kwenye rasilimali za mafuta, gesi na madini. Asili ya tasnia hizi ambazo mirija mikubwa ya vyanzo vya mapato inamaanisha kuwa nchi huwa zinapata ugumu kwenye kusimamia manufaa ya sekta hii. EITI inasaidia serikali na washikadau wengine kama makampuni, vyama vya ushirika, wawekezaji, vyombo vya habari na wengineo kutoa taarifa, kupitia na kukagua kwa utaratibu, malipo yanayotolewa na makampuni na kiasi kinachopokelewa na mawakala wa serikali. Uwazi huu ndio msingi madhubuti wa usimamizi mzuri wa sekta na utawala bora kwa ujumla. Kuwashirikisha wadau wote kwenye kutengeneza progamu ya namna hii inaongeza uwajibikaji wa serikali na makampuni. Manufaa kwa nchi zinazo tekeleza EITI yanajumuisha: - · Kuonyesha msimamo wa taifa kwenye uwazi: Utekelezaji wa EITI unaweza kuwa ni ujumbe tosha kwa wadau wote kwamba serikali husika inadhamini uwazi na uwajibikaji katika malipo na mapato ya tasnia ya uziduaji ­ hii inaweza kuwa kwa uboreshaji utawala bora wa sekta hizi. Programu ya EITI inapopewa kipaumbele kwenye mapambano dhidi ya rushwa inasaidia kutengeneza mazingira magumu kwa "kodi iliyofichika" ya rushwa kulipwa. Kwa kuwa EITI ina viwango vya kimataifa nchi iliyoandikishwa kama inatimiza EITI inakutana na mfululizo wa vigezo vilivyokubalika kimataifa kwenye kuboresha uwazi na utendaji unaosimamiwa kwa kujitegemea kupitia uthibitishwaji. · Ukusanyaji mapato wenye ufanisi zaidi: Kwa kuongeza ufuatiliaji kwenye malipo, mapato na mtiririko wa misaada, mara nyingine programu ya EITI inapelekea ufanisi mkubwa zaidi katika kukusanya kodi kutoka makampuni yaliyo kwenye tasnia ya uziduaji. Kwa kuweka taarifa zote wazi inarahisisha kutambua rushwa. · Utaratibu wa muundo wa ushirikiano: Uwajibikaji wa hali ya juu wa serikali, makampuni na vyama vya kijamii kwa kupitia EITI unaweza kuongeza uaminifu kwa makundi hayo. Kwa kutoa utaratibu wa 1 kuwasiliana na wadau wote, EITI inaweza kufanikisha upatikanaji wa suluhu ya pamoja kwa matatizo yaliyopo, kwa kufanya hivi itapunguza uwezekano wa migogoro na kuongeza uthibiti, ambayo ni muhimu katika kujenga mazingira bora ya uwekezaji na maendeleo endelevu ya uchumi. · Kuboresha Mamlaka na viwango vya madaraka: Kwa kuandaa ripoti za EITI za mapato na matumizi ya mara kwa mara, nchi inaweza kuboresha na kutengeneza mazingira ya kukopesheka zaidi kwa serikali na makampuni. Mamlaka ya viwango vya mikopo inategemea ubora wa utawala wa nchi na uwezo wake kutimiza majukumu ya kifedha. Jinsi taarifa zilizo katika mamlaka ya uma, kuhusu mapato zinavyozidi kuwa za kuaminika, uwezo wa taasisi za fedha na wakala wa uthamini kutathmini uwezo wa nchi kukopesheka unaongezeka. Uwezo wa kukopesheka ukiboreshwa utaleta uwezo wa nchi kuvutia mikopo, na utapunguza gharama ya udhamini huo. · Kuongeza uwajibikaji: Pale kiasi kinacholipwa kwa wakala mbali mbali wa serikali (na wakati mwingine kwa serikali ndogo) kikijulikana kwa jamii, wananchi wanaweza kuweka mikakati ya kuhoji na kuziwajibisha jinsi wakala husika zinavyotumia mapato na matumizi ya taifa. Usimamizi wa bajeti ya serikali ni shughuli muhimu inayoweza kuendana na programu ya EITI, lakini ni vigumu kubeba maana iwapo hakuna taarifa za uhakika za mapato. · Uangalizi wa Usalama katika biashara: EITI inaweza kusaidia kupunguza hatari kuingia hasara kwa makampuni ya uziduaji. Kwa kuonyesha bayana kiwango kinacholipwa kwa serikali na kwa jamii, kampuni pia itatoa ripoti ya manufaa yatokanayo na utendaji wake. Hii inasaidia pia kuipa serikali majukumu ya maendeleo endelevu ya muda mrefu kwa sekta na uchumi kwa ujumla. Usimamizi bora katika makampuni utanufaisha pande zote makampuni na nchi, kwa mikakati ya muda mrefu ya uziduaji yenye gharama ndogo. Kwa kupunguza gharama kwa makampuni nchi inaweza kuongeza wawekezaji kwa kuwavutia. Uzoefu unaonyesha kuwa manufaa zaidi yanapatikana kwa serikali ambazo zinashirikisha EITI kama sehemu ya uboreshaji wa programu ya utawala bora wa maliasili. Wakati EITI inaweza kuwasilisha manufaa mengi zaidi kama mkakati unaojitegemea, una nafasi ya kufanya kazi vizuri zaidi kama kutakuwa na mkakati wa kudumu kwa kuifanya EITI sehemu ya harakati za urekebishaji wa mambo kama uboreshwaji wa usimamizi wa bajeti, 2 utengenezaji wa mkakati wa kupambana na rushwa, au uboreshwaji wa usimamizi wa tansnia ya uziduaji (kuanzia kwenye uwazi wa utolewaji wa leseni za utafutaji mpaka kwenye usimamizi na ungalizi bora wa watendaji waliopo). NCHI ZINAZO TEKELEZA EITI Nchi zote zenye utajiri wa rasilimali zinatakiwa zihimizwe kujiunga na EITI. Kwenye Muongozo wa Uwazi katika Rasilimali na Mapato , Shirika la fedha la 6 dunia (IMF) linaelezea nchi tajiri kwa rasilimali kama nchi ambazo jumla ya hazina ya serikali, au jumla ya wastani wa mauzo ya nje ya nchi yanatokana na mafuta, gesi au sekta ya madini, imekuwa zaidi ya asilimia 25 kwa zaidi ya miaka mitatu iliyopita (Angalia kiambatisho A). Nchi hizo zinategemea sana mauzo ya nchi za nje na mapato toka kwa kiwango kidogo cha mirija ya mapato iliyounganishwa pamoja, na kutokana na sababu hii kuna haja ya kusimamia rasilimali hizi kwa umakini zaidi ili kuzuia mmomonyoko wa uchumi, kijamii na serikali kwa ujumla ambao ulikwisha kutokea kwenye nchi zenye utajiri wa rasilimali. Kuna nchi nyingine ambazo pamoja na kuwa hivi sasa hazijaelezewa kama nchi zenye utajiri wa rasilimali zinaweza kuingi kwenye kundi hilo hapo baadae, lakini hazijaweka msimamo wa kutekeleza EITI. Nchi Zilizo endelea na Zenye Utajiri wa rasilimali Kumekuwa na swali kwamba: Ni kwanini nchi zilizoendelea zinazounga mkono EITI kiuchumi na kisiasa hazijiungi na kutekeleza vigezo vya EITI? Sehemu ya jibu ni kuwa wakati nchi nyingi zilizoendelea zina viwanda muhimu vya uziduaji kuna nchi chache ambazo tasnia ya uziduaji ina mchango mkubwa kwenye mauzo yake ya nje. Jibu lingine ni kuwa nchi hizi zilizoendelea zenye utajiri wa rasilimali tayari zina mikakati ambayo inafanana na ile ya EITI ya uwazi na utawala bora kwa kusimamia sekta ya uziduaji kwenye nchi zao. 6Kwa maelezo zaidi angalia http://www..imf.org/external/np/pp/2007/eng/051507g.pdf. 3 Hata hivyo ifahamike kuwa Norway ambayo inatambulika kama nchi tajiri kwa rasilimali7 inafikiria kutekeleza mkakati huu. KUJENGA MAKUBALIANO KWENYE EITI Wakati wa kufanya maamuzi ya kuipitisha EITI, serikali huwa zinawasiliana na washikadau ambao wataathiriwa na utekelezaji wa EITI. Aina ya washika dau wanaohusishwa na EITI (wanajadiliwa zaidi kwenye sura ya 2: wadau na mfumo wa utawala) inajumuisha, makampuni ya uziduaji ya kitaifa na kimataifa, makundi ya kibiashara, vyama vya kijamii vya ndani ya nchi, na wakala wengine wa serikali (na inawezekana, serikali ndogo na viongozi wa kimila). Uzoefu unaonyesha kuwa nchi zilizoanza kutekeleza EITI bila kuhusisha wadau hawa zinapata ugumu kwenye utekelezaji. Na pia utekelezaji wa EITI bila kushirikisha wadau hawa ni kwenda kinyume na vigezo vya EITI. Nchi nyingi zimeendesha warsha na makongamano ili kupata mapendekezo kutoka kwa wadau juu ya kuingia kwenye EITI na utekelezaji wake. Baadhi ya 8 nchi zimefanya utafiti wa awali ili kusaidia kugundua wadau muhimu na hatua za kuchukua ili kutekeleza EITI. Vitu muhimu kwenye hadidu za rejea zilizotumika kufanya uatafiti wa awali huko Zambia zimeambatanishwa kwenye CD kama kiambatisho A. 7Ripoti hii haijadili mambo yaliyojitokeza kama madhara ya kutegemea kwenye rasilimali na uimara wa jamii hizo (madhara wakati mwingine yana tambulika kama "laana ya rasilimali", "Kinza ya wingi" na kuendelea), ambayo imetafitiwa kwa kina na imekuwa chanzo cha mijadala. 8Makundi ya Benki ya Dunia na timu ya EITI (na wadhamini wengine) mara kwa mara wanafanya kazi kwa karibu na serikali na wadau katika hatua hii, wakati utekelezaji wa EITI ukifikiliwa ­ kwa mfano kwa kutoa misaada ya fedha kusaidia kupata ushauri wa wadau na utafiti wa awali. Katika hatua hii na kwa mzunguko wa EITI nchi nzima, msaada wa Benki ya Dunia unatoka kwa Mfuko wa hisani wa wafadhili. (MDTF) 4 KUJIUNGA NA EITI NA HATUA ZA KWANZA Mara serikali inapoamua kujiunga na EITI, inapitia hatua9 zifuatazo pamoja na vigezo na muongozo wa uthibitishaji wa EITI: 1. Kutoa kauli moja kwa jamii juu ya madhumuni yake ya kujiunga na EITI 2. Kuahidi kufanya kazi pamoja na vyama vya kijamii na makampuni wakati wa utekelezaji wa EITI; 3. Kuteua mtu wa kuongoza harakati za utekelezaji wa EITI; na 4. Kuchapisha mkakati wa kazi (ambao gharama yake imekwisha kisiwa) na makadirio yanayopimika na ratiba ya utekelezaji ambayo imekubalika na wadau wote muhimu. KAULI YA PAMOJA JUU YA KUJIUNGA NA EITI Kauli ya serikali juu ya utekelezaji wa EITI na mkakati wake wa kufanya kazi pamoja na vyama vya kijamii na makampuni ya uziduaji, itakuwa na maana zaidi kama itatangazwa vizuri na kuwafikia wananchi wote, na pia inabidi iwepo kwenye tovuti ya EITI. Baadhi ya serikali zinaandika moja kwa moja kwa wadau muhimu juu ya dhamira yake hiyo ya kujiunga na EITI. Baadhi ya kauli inazipa jukumu serikali sio tu la kutekeleza EITI lakini pia kuweka programu ya EITI kwenye mtazamo mpana zaidi wa mapitio ya uchumi na utawala. Kauli hizi zinatolewa katika hatua ya wizara. Wakati huo huo Sekretarieti ya kimataifa ya EITI na wafadhili wanaounga mkono na mawakala (kama Benki ya Dunia, Shirika la fedha Duniani (IMF) na mabenki ya maendeleo ya kanda) wameishataarifiwa juu ya mkakati wa nchi kujiunga na EITI, pamoja na mkakati utakaotumika kutekeleza hatua za kujiunga kama zilivyoainishwa hapo juu. Mawasiliano haya wakati mwingine yamekuwa njia ya ya kupata misaada ya utekelezaji wa EITI kwa mfano kutoka kwa mashirika ya misaada ya kimataifa ikisimamiwa na Benki ya Dunia. 9Hizi ni hatua kuu nne za kwanza, maana yake "hatua ya usajili" viashiria "muongozo wa uthibitishaji EITI". Kwenye taratibu za sasa za Bodi ya EITI hatua hizi zinapokamilika, nchi itapewa hadhi ya utahiniwa na itahorodheshwa hivyo kwenye (www.eitransparency.org). 5 Wakati huo huo katika hatua za awali nchi nyingi za EITI zimekuwa na "kongamano la uzinduzi" ambalo linasaidia kutangaza uamuzi wa serikali kujiunga na kuanza kutengeneza makubaliano na EITI. Matamasha hayo ya uzinduzi yanatumika kuwaleta wadau kutoka pande tofauti kujadili mambo yahusuyo EITI na kuanza kutambua mashirika yatakayoshiriki kwenye mchakato huu pamoja na makundi ya wadau wengine mbali mbali. Kuchagua Kiongozi wa EITI Ili kuongoza jitihada hizi kwa ufasaha zaidi serikali itatakiwa kuchagua mtu mmoja wa kuongoza mchakato mzima wa kujiunga na kutekeleza EITI. Mtu huyu atajulikana kama "Kiongozi wa EITI". Katika nchi nyingi zinazo tekeleza EITI mtu huyu anayeteuliwa anakuwa amewahi kufanya kazi katika ngazi ya wizara kwenye wakala wa fedha (kwa mfano wizara ya fedha) au wakala wa sekta (kwa mfano wizara ya madini/ mafuta)). Wakati mwingine mteuliwa anakuwa ni mtu aliwahi kuwa mshauri wa juu katika ofisi ya raisi. Tabia za viongozi wa EITI katika nchi zinajumuisha yafuatayo: Wanapewa dhamana ya wadau wa taifa kutokana na ufahamu wao juu ya sekta nzima; wana mamlaka ya kuratibu shughuli za EITI katika wakala mbali mbali za serikali; wana uwezo wa kuanzisha mabadiriko yoyote muhimu katika udhibiti na sheria; na wana uwezo wa kupata vitendea kazi ili kutekeleza mkakati huu. Shughuli ya msingi kwa kiongozi huyu ni kuongoza na kusimamia kazi za wadau mbali mbali wa EITI kwenye nchi husika, na kuwaleta pamoja wadau. Kutengeneza mikakati ya kazi Hatua ya mwisho kwa serikali katika "Ngazi za kujisajili" EITI (na au kwenye makundi ya wadau mbali mbali) ni kuorodhesha, kurekebisha na kukubaliana na makakati wa kazi wa EITI kwa ushauri wa wadau. Mkakati huu wa kazi unaainisha yafuatayo: · Madhumuni: Malengo ya juu kabisa ya programu ya EITI. · Utendaji: Hatua bayana zinazohitajika kuyafikia madhumuni. · Mpangilio wa utendaji: Baadhi ya matukio yanaweza kuanza pale tu matukio mengine yatakapokamilika. 6 · Ratiba: Inaonyesha tarehe ambayo utendaji unategemewa kukamilika · Mhusika: Inaonyesha ni shirika au mtu gani anahusika kukamilisha utendaji ulioandaliwa. · Gharama na vyanzo vya fedha: gharama ya mpango mzima na nani atakaye lipia gharama hizo Katika hatua za awali za EITI, mikakati hii ya kazi inakuwa na uwanja mpana sana, lakini jinsi serikali inavyofanya kazi na makundi ya wadau mbali mbali kwa kuelezea kwa undani zaidi programu za EITI, na jinsi utekelezaji unavyoanza , mkakati wa kazi unakuwa bayana zaidi (kama inavyoelezewa kwa undani zaidi kwenye sura ya 4: Kutengeneza Mkakati wa kazi wa EITI). Upatikanaji wa Fedha za Kutosha kwa ajili ya utekelezaji wa EITI. Ikiambatana na kuteua kiongozi na kuanzisha Makakati wa kazi wa EITI, watoa maamuzi wanaanza kutenga pesa zinazohitajika kutoka kwenye bajeti za serikali, na kutengeneza mkakati wa kukusanya vitendea kazi na misaada ya kitaalam kutoka kwa nchi zinazojitolea, mashirika ya misaada na mashirika ya maendeleo ya kimataifa. Mambo ya fedha yanaelezewa kwa undani baadae kwenye ripoti hii. 7 SURA 2: WADAU NA MFUMO WA UTAWALA UTANGULIZI Kanuni ya msingi ya EITI ni kuwa inatekelezwa kwa ushirikiano na wadau mbalimbali. Hii ina maana kuwa wadau walio nje ya serikali kama makampuni ya uziduaji na vyama vya kijamii havishirikishwi kwa ushauri tu bali pia kwenye mkakati mzima wa kusanifu, kuendesha na kusimamia mchakato mzima. Kanuni hii inaonekana kwenye mfumo wa utawala wa kimataifa wa EITI. Uzoefu unaonyesha kuwa kuhusishwa kwa wadau mbali mbali kunachangia kwa kiasi kikubwa katika mafanikio ya utekelezaji wa mkakati wa EITI, sura hii inachanganua kuhusishwa kwa wadau katika mchakato wa taifa wa EITI. WADAU WANAOHUSISHWA Mwenendo wa wadau wanao husishwa na utekelezaji wa programu ya EITI kwa nchi tofauti, unatofautiana, lakini kwa kawaida wadau ni wawakilishi wa makundi yanayoathiriwa na EITI (yaani serikali, vyama vya kijamii, na makampuni ya uziduaji), na wana nafasi kwa kuzingatia utekelezaji kitaifa. Sanduku 2.1 linaonyesha aina ya wadau ambao kwa kawaida wanahusishwa kwenye mchakato wa EITI. SANDUKU 2.1 WADAU WANAOHUSIHWA KATIKA MCHAKATO WA EITI SERIKALI NA MASHIRIKA YA UMA - Wakala wanaohusika kusimamia maliasili - Wakala wanaohusika na makusanyo na usimamizi wa kodi - Wakala wanaohusika na maendeleo ya kiuchumi, mipango, sekta binafsi n.k - Bunge na mabaraza yake, kwa mfano, bajeti, mipango, fedha na/au mali asili. 8 - Tume za taifa za uchunguzi - Makampuni ya kitaifa ya mafuta na madini - Viongozi wa kimila SEKTA BINAFSI - Makampuni ya mafuta, gesi na madini yanayofanya shughuli zake katika nchi husika (ikijumuisha makampuni ya kimataifa yanayomilikiwa na nchi fulani, makampuni binafsi ya nchi husika, makampuni binafsi ya kimataifa) - Makampuni ya kitaifa ya mafuta na madini - Wawekezaji - Shirikisho za biashara na viwanda VYAMA VYA KIJAMII - Mashirika ya kijamii - Mashirika ya kitaifa yasiyokuwa ya kiserikali - Mashirika ya kimataifa yasiyokuwa ya kiserikali - Vyombo vya habari - Vyama vya wafanyakazi - Vyuo na taasisi za utafiti - Mashirika ya Kidini - Viongozi wa kimila MASHIRIKA YALIYOPEWA MIKATABA KUUNGA MKONO MCHAKATO WA EITI - Wasuluhishi, wakaguzi; na mashirika mengine ya uchunguzi. WASHIRIKA WA KIMATAIFA - Bodi ya EITI na Sekretarieti ya EITI - Taasisi za maendeleo za kimataifa (shirika la fedha la dunia, Benki ya Dunia, na Benki za Maendeleo za Kanda) - Wakala wa Misaada Note: Orodha hii ya wadau ni kwa ajili ya kuonyesha wadau wanaoweza kuhitajika katika kukamilisha mchakato wa EITI. Pamoja na kuwa nchi zote zilizo tekeleza EITI zimeonyeshwa katika makundi makuu matatu ya wadau (serikali, makampuni na vyama vya kijamii), hakuna nchi iliyoweka wadau wote kama walioorodheshwa katika kila kundi. 9 SANDUKU 2.2 MAKAMPUNI YANAYOMILIKIWA NA SERIKALI Katika nchi nyingi zinazozalisha mafuta na baadhi ya nchi za uchimbaji madini, serikali inashiriki moja kwa moja kwenye sekta ya uziduaji kwa kupitia makampuni yake inayoyamiliki. Makampuni haya yanaweza kuhusika katika sekta kwa namna mbali mbali. - Kama shirika la uwekezaji lenye umiliki kwenye makampuni mbali mbali yanayojihusisha na uzalishaji wa mafuta, gesi na madini katika nchi husika. - Kama kampuni ambayo (kwa nchi zinazohusika na uzalishaji wa mafuta) ina jukumu la kukusanya na kutafuta soko na kuuza hisa za serikali. - Kama mbia kwenye makampuni na - Kama muendeshaji wa mgodi au visima vya mafuta. Zaidi ya hapo, makampuni yanayomilikiwa na serikali kusimamia na kurekebisha makampuni yote yanayofanya kazi ndani ya nchi husika. Kutokana na majukumu haya katika maeneo ambayo kuna makampuni yanayomilikiwa na serikali yameonekana kuwa ni wadau muhimu, na wanahitaji kuhusishwa mapema katika mchakato mzima. Katika kukusanya taarifa juu ya mapato na malipo, makampuni yanayomilikiwa na serikali yanajikuta sehemu zote kama wapokea malipo hisa za uzalishaji kutoka kwa makampuni mengine na wakati huo huo walipaji kwa bajeti ya taifa. Baadhi ya makampuni yanayomilikiwa na serikali yanabanwa na matakwa ya uwazi yanayozibana wakala zingine za serikali na hii inamaanisha kwamba taarifa nyingi kuhusu kampuni hizo zinapatikana kwa uma. Kwa upande mwingine nchi zingine zimegundua kwamba mashirika yanayomilikiwa na serikali yanahitaji kutoa taarifa zaidi kwenye mchakato wa EITI kuliko kampuni zisizo za kiserikali ( hii ni kwa sababu ya mchanganyiko wa majukumu yake) MAKUNDI VIONGOZI YA WASHIKADAU NA UTAWALA WAKE Kwa kuangalia asili ya uhusishwaji wa EITI, uchambuzi wa wadau mbali mbali kusimamia mkakati mzima umekuwa ukichukua muda na mchakato mrefu kwenye baadhi ya nchi, hasa wakati wa kuuanza mchakato. Hata hivyo nchi zote zinazo tekeleza EITI zimeunda makundi ya washikadau wa baraza la EITI ­ kwenye ripoti hii yanatambulika kama "makundi viongozi". 10 Mambo muhimu yanayohusishwa na makundi viongozi na usimamizi wake ni pamoja na:- · Vigezo vya kisheria vya kuunda kundi kiongozi: Katika muktadha sheria, kwenye baadhi ya nchi kundi la wadau liliundwa kwa mwaliko wa kiongozi wa juu wa serikali au waziri. Ijapokuwa, kwa baadhi ya nchi namna fulani ya chombo cha kisheria (kwa mfano agizo maalum toka kwa rais au waziri, au sheria fupi) ilitumika kuunda kundi hilo. · Kupata ukubwa na uanachama wa kundi kiongozi: Utaratibu unatofautiana. Kwa nchi nyingi makundi haya yanakuwa na wanachama 10 hadi 20. Hakuna kanuni inayoonyesha makundi haya ya wadau yanawakilishwa kwenye makundi viongozi, na suala la uzito limekuwa likijadiliwa kwenye nchi nyingi za EITI. Kwenye nchi ambazo kuna namba kubwa ya makampuni makubwa, ambapo hakuna makampuni mengine yanayoleta makundi ya wadau pamoja, au sehemu ambazo kuna wakala wengi wa kukusanya mapato ya serikali, kumekuwa na haja ya kuyapa uzito makampuni hayo au wakala wa serikali kuliko wadau wengine kutoka sekta zingine. Katika hali kama hizi nchi zimetakiwa kuwa makini sana kuhakikisha kuwa vyama vya kijamii pia vinashirikishwa kikamilifu katika mchakato mzima. · Uanachama wa vyama vya kijamii: Bila kujali ukubwa, uwakilishi wa vyama vya kijamii kwenye makundi viongozi umekuwa na unatakiwa uwe na maana timilifu. Uwakilishi wa vyama vya kijamii umetawanyika sana, kwa asili yake vyama vya kijamii vina mchanganyiko mkubwa. Nchi pia zimeona ni muhimu kuviachia vyama hivi vichague uwakilishi wake kwenye makundi viongozi ili kuzuia uwezekano wa kuwa na uwakilishi uliowekwa na serikali na ukakosa michango halisi kutoka kwa wadau wake. Suala la ushiriki wa vyama vya kijamii ambavyo vina asili ya kisiasa kwa minajili ya kuunga mkono au kupingana na serikali vimeleta utata katika baadhi ya nchi. (Baadhi ya nchi zimesitisha ushirikishwaji wa vyama vya kijamii zikihofia kupunguza kazi ya utekelezwaji wa EITI na wasiwasi wa EITI kuonekana haijatimiza taratibu na viwango. · Uanachama wa Kampuni: Makundi viongozi yanakuwa na uwakilishi toka kwa kila kampuni inayojiusisha na mafuta, gesi na madini; au kutokana na wingi wa makampuni kama njia hii ikishindikana namna nyingine ya uwakilishi inaweza kutumika kutoa taarifa ya maamuzi yaliyofikiwa na wadau kwa makampuni. 11 · Kuanzisha na kurejea uanachama wa kundi kiongozi: Uanachama katika makundi viongozi ni kwa muda wa mwaka mmoja hadi miwili. Njia za kuchagua wanachama wa makundi haya zinatofautiana, lakini zinajumuisha: () kuchaguliwa na serikali (ii) kuhodhi mikutano rasmi na isiyo rasmi kuhusu EITI kuelezea madhumuni ya programu kabla wadu hawaja pendekeza wawakilishi (iii) uchaguzi kwa kupitia makundi mbali mbali ya wadau ambayo yaliomba kupendekeza wawakilishi ( katika nchi nyingi vyama vya ushirika vinachagua wawakilishi wao kwa mkutano wa siri kuingia kwenye kundi kiongozi na makampuni yanafanya hivyo hivyo kupitia chama cha wachimbaji au umoja wa wazalisha mafuta) na (iv) uchapishaji wa taarifa za uma kuomba mapendekezo ya majina. Nchi zenye programu za EITI zilizofanikiwa ni zile zilizoruhusu wadau mbali mbali kuchagua wawakilishi kwenye "majimbo" yao. Kama serikali ikichagua wanachama wa kundi kiongozi ni vigumu kwa serikali kuonyesha kuwa vyama vya ushirika vinajitegemea katika uwakilishi. · Mteuliwa binafsi kuwa mwanachama: makundi viongozi yanajumuisha wanachama binafsi wakiwakilisha mashirika mbali mbali, ili kuhakikisha kwamba uwakilisha utakuwa ni wa kudumu nchi nyingi zimeweka nafasi maalum kutoka kila kundi la wadau. Pamoja na hiyo nafasi ya uwakilishi mbadala inaendelea kuwepo ikitokea mwanachama wa msingi ameshindwa kuhudhuria. · Kazi ya mwenyekiti: Makundi viongozi mengi yana mwenyekiti mpendekezwa ambae ana majukumu (kwa kushirikiana na sekretarieti na tume ya utekelezaji) kuitisha na kusimamia mikutano. Mwenyekiti kwa kawaida ni aliyeteuliwa na serikali "Kiongozi wa EITI". SANDUKU 2.3 WAKALA WA MAELEWANO/ HADIDU ZA REJEA 12 Ili kushirikisha wadau wote na kuwa wazi katika sheria na uendeshaji wa makundi viongozi, nchi nyingi zimetengeneza wakala wa maelewano na hadidu za rejea kwa ajili ya kundi kiongozi au kwa mkakati mzima wa EITI. Wakala hizo za maelewano zina sainiwa na wanachama wa makundi viongozi (na mashirika mengine kadhaa, kuonyesha kujitoa kwao kwa EITI) na kwa kawaida inazungumzia. - Msimamo wa watia saini kwa taratibu na vigezo vya EITI; - Jinsi makakti utakavyosimamiwa na kuendelezwa - Haki na majukumu ya kila shirika lililo tia saini kwenye wakala wa maelewano; - Maelezo ya jinsi ripoti za EITI zitakavyoandaliwa - Jinsi wasimamizi na wakaguzi wa kujitegemea (wenye wajibu wa kupitia nakala za malipo na mapato) watakavyoteuliwa; Mfano wa wakala wa maelewano wa kundi kiongozi la huko Azerbaijan umeambatanishwa kwenye CD kama kiambatisho B. · Uchaguzi na maamuzi mengine: Baada ya makundi viongozi kuundwa, wanachama watakubaliana jinsi kundi litakavyo jiendesha kwa taratibu na miongozo watakayojiwekea. Miongozo na taratibu hizo zitaweka bayana chaguzi na mikutano muhimu ya kufanya maamuzi; vipindi vya mikutano na miongozo ya uendeshaji wa mikutano hiyo (kwa mfano, Chatham House Rule ambayo inawahakikishia washiriki kutoa mawazo yao bila wasiwasi na nafasi za wahusika). Taratibu hizi zitaunganishwa kwenye wakala wa maelewano au hadidu za rejea kwa ajili ya makundi kama inavyo jadiliwa hapo chini. · Misaada na Fedha: Katika baadhi ya nchi vitendea kazi vinakuwepo kwa ajili ya kuwawezesha wanachama wa makundi (kwa mfano kutoka miji mbali mbali) kuhudhuria vikao. MAMBO MENGINE YA KUZINGATIA Makundi ya viongozi huwa yanakutana na changamoto ya upana wa uwakilishi wao, wakati yanahitaji kuwa madogo ili kurahisisha kukutana mara kwa mara na kwa urahisi. Katika kulizingatia hili, nchi zimetumia mbinu mbali mbali kama vile: · Njia ya Majimbo: Kwenye njia hii (mwana chama anawakilisha kitu kile kile kwa mtindo wa mzunguko) hii ina manufaa na hasara zake. Ina hakikisha kuwa majibo yote yatawakilishwa na makundi yatakuwa na 13 ukubwa wa kuweza kusimamiwa. Lakini pia inaweza kuzuia majimbo mengine kama majimbo yenye watu wachache au wawakilishi wachache"" mtindo wa maamuzi ambapo wanachama wataweza kukubaliana na baadhi tu ya mapendekezo. · Kongamano la kitaifa la EITI: Katika baadhi ya nchi watu ambao hawa husishwi katika shughuli za kila siku za makundi viongozi wanahudhuria makongamano ili waweze kushauri juu ya maendeleo ya mkakati kwenye nchi husika; hii inaruhusu makundi ya mashirika na watu binafsi wanaofuatilia mchakato wa EITI kushiriki kikamilifu. · Vyombo vya utekelezaji vya Kitaifa: Utekelezaji wa EITI unategemea sekretarieti kuratibu mambo yote yahusuyo mkakati huu. Baadhi ya nchi zimefikiria kufanikiwa zaidi kwa kuwatumia na kuwaalika wadau wa makampuni na vyama vya kijamii kufanya kazi katika vyombo vya utekelezaji. (Kwa maelezo zaidi, angalia sura 5: Nafasi ya Serikali katika Utekelezwaji wa EITI) · Makundi ya Wataalam: Kutengeneza mtazamo wa kazi za kitaalam ambao makundi viongozi yatazifanya, nchi nyingi zimeanzisha makundi madogo ya kwa ajili ya shughuli maalum. KAZI ZA MAKUNDI VIONGOZI YA WADAU Moja kati ya kazi za kwanza za kundi kiongozi ni kuzielezea kazi zake na kuziweka bayana kulingana na nchi husika. Katika nchi nyingi majukumu ya makundi haya (pamoja na maelezo kuhusu mahusiano yake na makundi mengine, na sheria na taratibu jinsi litakavyoendeshwa) vinawekwa bayana kwenye wakala wa maelewano au hadidu za rejea kwa kundi viongozi kama itakavyokubalika. Kazi za kawaida za kundi kiongozi zilizo katika utendaji ni; · Mpango mzima wa maamuzi: Mkakati wa EITI una ugumu wake na unahitaji uratibu wa karibu wa wadau mbali mbali na madaraka ya kuweza kufanya maamuzi muhimu ya kiutekelezaji. · Kutengeneza Mipaka ya Programu ya EITI: Kazi muhimu ya kundi kiongozi ni kuamua na inapobidi kuelezea na kupitia na kuboresha mipaka ya ujumla ya programu ya EITI. Hii itajumuisha kuamua makampuni yapi na vyanzo vipi vya mapato vitahusishwa; ngazi za 14 maelewano na ukaguzi; kama serikali ndogo zitahusishwa kwenye programu; na jinsi ripoti ya mwisho itakavyo chapishwa. Mambo haya yameelezewa kwenye sura 3: Upatikanaji wa mipaka ya Programu ya EITI. · Kuendeleza au kukubaliana na mpango wa kazi na kudhibiti maendeleo: Kuandaa mpango wa kazi ni moja kati ya vigezo vya EITI, makundi viongozi kwa kawaida huwa yanahusika kwenye kupitia na kupitisha mpango wa kazi wa EITI. Baadhi ya makundi yanafanya kazi kwa karibu sana na sekretarieti na kutengeneza mpango wa kazi wao wenyewe. Baada ya mpango wa kazi kupitishwa baadhi ya makundi yamekutana na hali ya kupitiwa kwenye matumizi ya fedha au kupata taarifa za mara kwa mara kuhusu matumizi ya fedha. · Kuteua na kusimamia wasimamizi na mashirika ya usuluhishi: kwenye nchi zote, makundi viongozi yamekuwa yakihusishwa moja kwa moja kwenye kuteua mkaguzi au msimamizi kuhakiki malipo na mapato yaliyoletwa na serikali au makampuni. Kwenye nchi nyingi kundi kiongozi linatoa kazi hii kwa kikundi maalum kama ilivyo kwenye hadidu za rejea. · Ripoti za Kitaalamu: kundi kiongozi pia linajukumu la kufanya kazi na msimamizi ili (i) kutengeneza mfumo wa kuripoti kuhusu mchakato wa EITI kwa wakala wa serikali na makampuni; (ii) kutengeneza muongozo kwa ajili ya serikali na makampuni unaaonyesha jinsi ya kukamilisha na kukusanya ripoti hizo; (iii) kuamua ni mara ngapi ripoti za EITI ziwe zinaandikwa; na (iv) kusuluhisha mambo mengine yoyote ya kitaalamu kuhusu usimamizi wa mkataba wa ukaguzi na timu ya usimamizi. · Kuleta ufahamu kwa Uma kuhusu EITI: makundi viongozi mengi (au makundi madogo) yanakazi kubwa ya kutawanya ripoti za EITI na kukuza ufahamu wa uma ili EITI ifahamike na kueleweka, sio tu na wadau wanaohusika kwenye mchakato bali pia na uma mzima. ( Mpango wa kazi wa EITI mara nyingi unaonyesha jinsi ya kutekeleza hili; kwa mfano kupitia vyombo vya habari, maonyesho ya kitaifa , mitandao na kuendelea) · Kupitia na kuondoa vikwazo kwenye utekelezaji : makundi viongozi mara kwa mara yanagundua na kuelezea vikwazo vinavyojitokeza kwenye utekelezaji wa EITI, kwenye makakai wa kazi njia za kuondoa vikwazo hivyo zinatengenezwa. Kwa mfano; umuhimu wa kuunda masharti ya 15 kujitolea au yanayolindwa kisheria yanayoiwezesha serikali na makampuni mengine kuweka taarifa za malipo na mapato yao wazi. Mfano wa agizo la serikali toka Peru lililoanzisha kundi kiongozi na kuorodhesha wanachama na kazi zake linapatikana kwenye CD kama kiambatisho D. Mwisho, ni neno kuhusu kazi ya kundi kiongozi kwenye mchakato wa udhibiti. Pamoja na kuwa wakati wa kuandika ripoti hii hakuna nchi iliyokuwa imeanza mchakato wa uthibitishaji chini ya taratibu za Bodi ya EITI, kazi ya msingi ya baadae ya makundi viongozi itakuwa ni kupitia na kuthibitisha ripoti pale zitakapo kamilika. 16 SURA 3: UPAMBANUZI WA MIPAKA YA PROGRAMU YA EITI UTANGULIZI Ijapokuwa EITI ina vigezo vinavyojieleza, pamoja na mfumo wa uthibitishaji unaoeleweka, utekelezaji wake umechukua miundo ya aina mbali mbali kwa nchi tofauti kutegemea na hali ya nchi na sekta zake. Sura hii inawasilisha viini vya programu mbali mbali za EITI zilizo tengenezwa na nchi husika. Kumbuka: Jinsi mambo yaliyoandikwa katika taarifa hii yanavyokwenda kwenye kiini cha ripoti ya EITI ya nchi husika, ni muhimu kuisoma sura hii sambamba na sura ya 7: Uandaaji wa ripoti ya EITI, ambayo inazungumzia mchakato wa kitaalam wa kutengeneza ripoti za EITI. Maeneo muhimu ya maamuzi Uzoefu wa utekelezaji wa EITI mpaka hivi sasa unaonyesha kwamba jambo la kwanza ambalo nchi za EITI limehitaji kulifanya ni kufanya maamuzi muhimu juu ya mapana ya mchakato mzima wa EITI. Hii ni kutokana na kuwa maamuzi tofauti yanapelekea programu tofauti za EITI, maamuzi ya awali yaliyoorodheshwa hapa chini yanahitaji uangalizi wa ndani na ushauri wa wadau na unaonyesha kuwa ndilo jambo lililojadiliwa zaidi na makundi viongozi ya EITI. Mambo haya makuu matano ya kwenye nchi hizi ni kama yafuatayo (kila moja litajadiliwa kwa undani kwenye sura hii): · Mchakato wa usuluhishi au uchunguzi: Maamuzi muhimu kwa nchi za EITI kuhusu ripoti za EITI zitakuwa ni makubaliano ya malipo au mapato (yatakayoyofanywa na kampuni inayotumiwa kama msimamizi), au kama itakwenda zaidi ya hapo na kuruhusu taarifa za malipo na matumizi zikaguliwe kwa viwango vinavyokubalika kimataifa (kwa maana ya kufanywa na kampuni ya ukaguzi yenye sifa zinazostahili). 17 · Uwezo wa kutimiza malipo au ushiriki wa kampuni: Nchi binafsi zimeweka viwango vya kutimiza malipo (yaani viwango vya malipo ambavyo chini ya hapo kampuni haishirikishwi kwenye mchakato wa EITI kwa sababu za kiutendaji) au kwa ushiriki wa kampuni (yaani utendaji wa kampuni ambao ukiwa chini ya hapo kampuni haihusishwi na mchakato wa kuripoti EITI). · Uandaaji wa ripoti za mapato na matumizi ya fedha kwa uwazi kutoka katika makampuni na watu binafsi kwenye ripoti za EITI: Kwa kuongezea kwenye kutimiza malipo, kiini cha msingi kwenye wigo wa EITI ni kiwango cha mchanganuo wa data katika ripoti za EITI, kwa kutambua au kutokutambua jumla ya malipo yanayofanyika na makampuni. · Kujumuisha serikali ndogo au malipo ya huduma kwa jamii: Baadhi ya nchi za EITI zinamua kuripoti malipo yaliyotolewa kwa serikali kuu. Programu zingine huwa zinaamua kuripoti malipo yaliyotolewa kwa serikali ndogo (kwa mfano wilayani na kwa viongozi wa kimila) au kwa makundi ya huduma/jamii. · Kuhusisha sekta zingine au malipo yasiyohusisha uzalishaji: Namba ndogo sana ya nchi imeamua kuhusisha rasilimali zingine (kwa mfano misitu) kwenye programu zao za EITI. Baadhi wameamua kukuza wigi wa programu zao za EITI kuhusisha vyanzo vya mapato ambavyo havina uhusiano na shughuli za uziduaji na uzalishaji. Kwa ujumla tofauti na baadhi ya uchanganuzi, EITI inafaa na inaweza fanyika kwenye nchi zote zile za uchimbaji madini pamoja na zinazojishughulisha na uzalishaji wa gesi na mafuta. Maendeleo ya EITI kwenye nchi za uchimbaji madini haikubaliani na mtazamo kuwa EITI inafaa tu kwa nchi za mafuta na gesi. 18 MAMBO YANAYO ZINGATIWA WAKATI WA KUTENGENEZA WIGO WA PROGRAMU YA EITI Sifa ya pamoja ya mambo hayo matano hapo juu ni kuwa yote yanaangalia ni kiasi gani cha taarifa kitapatikana na kuwekwa bayana na mchakato wa EITI. Maamuzi kuhusu haya mambo yatakuja baada ya mijadala mirefu na wadau kuhusu kiwango cha uwiano kati ya upatikanaji wa data, gharama za upatikanaji, manufaa yake na jinsi programu ya EITI itakavyoiwianisha na sekta nzima ya usimamizi na utawala bora. Mfano wa taarifa iliyoorodhesha wigo wa programu ya EITI toka Ghana inapatikana kwenye CD kama kiambatisho E. Hakuna jibu sahihi linalotolewa kwa mambo haya kila nchi ya EITI itakuwa na jibu lake linaloendana na vigezo vya EITI. Hata hivyo baadhi ya sababu za msingi zinaweza kutambuliwa kwenye uzoefu wa nchi za EITI kuhusu wigo wa programu ya EITI: · Kiasi cha data zilizokuwa tayari kwa umma: katika baadhi ya nchi ni taarifa chache sana kuhusu malipo ya makampuni na mapato ya serikali ambazo zipo wazi kwa umma zimewekwa kwenye chanzo kimoja na rahisi kueleweka. Kwa baadhi ya nchi data hizo tayari zipo na zinapatikana kwenye vyanzo vichache ambavyo ni rahisi kufikiwa. SANDUKU 3.1 MITAZAMO TOFAUTI KWENYE NCHI ZINAZOZALISHA MAFUTA, GESI NA ZA UCHIMBAJI MADINI Toka kuanzishwa kwake, EITI imekuwa ikizihusisha nchi zinazo jishughulisha na uzalishaji wa mafuta na gesi, pamoja na zile za uchimbaji madini. Baadhi ya ripoti za mwanzoni za EITI zilitoka kwa nchi zinazozalishaji mafuta na gesi, hata hivyo hivi karibuni nchi zinazo jihusisha na uchimbaji zimeanza kutekeleza EITI na kutoa ripoti za EITI. Kutokana na utafauti wa sekta hizi za mafuta gesi na madini na mtiririko wake wa masuala ya kifedha, tofauti zipo kwenye wigo wa programu ya EITI zinazotumiwa na sekta hizi: - Kampuni zinazomilikiwa na serikali (mara nyingi zikihusishwa kwenye mchakato huu wa EITI toka kwenye hatua za awali 19 sana na kutakiwa kutoa taarifa zao zaidi ya makampuni mengine zinapatikana zaidi kwenye sekta za mafuta na gesi kuliko kwenye sekta ya madini) - Shughuli za uzalishaji gesi na mafuta kwa kawaida ni kubwa (kwa uwekezaji na mapato) kuliko uzalishaji wa madini, ambapo kampuni ndogo za mafuta au gesi ni muhimu katika mapato. Uzalishaji wa madini kwa upande mwingine unaweza kuwa mdogo sana kwa kulinganisha. Hii inatokana na viwango vya utimizaji malipo vilivyowekwa ili kushiriki kwenye EITI; nchi chache sana zimetoa makampuni ya gesi na mafuta kwenye programu ya EITI, lakini nyingine zimeamua kupunguza nchi chache za madini ili kuongeza ufanisi. - Kwenye nchi nyingi za uchimbaji kuna wachimbaji wadogo wadogo. Mpaka hivi sasa kuna uzoefu mdogo kwenye utekelezaji wa EITI juu ya jinsi ya kuwahusisha wachimbaji wadogo wadogo kwenye mchakato huu,pamoja na kuwa nchi chache zimeanza kulifikiria hili. Njia mojawapo japokuwa haijajaribishwa inaweza kuwa ni kuwafuatilia mawakala na wasafirishaji wa madini haya nchi za nje, hii ni kwa sababu bishara hiyo huwa inashikiliwa na watu wa chache tu katika nchi husika. - Uzalishaji wa madini una madhara ya haraka kwa jamii inayoizunguka, watumiaji wa barabara, bandari) ukifananisha na uchimbaji wa mafuta ambao mara nyingi unakuwa ndani ya bahari. Hivyo makampuni ya madini mara nyingi yanalipa pesa nyingi kwa serikali ndogo, au fungu la malipo kwa serikali kuu yanagawiwa na serikali kuu kwa majimbo yenye shughuli za uchimbaji pale ambapo kuna malipo yanapelekwa kwa serikali ndogo, ;wigo wa EITI inabidi uongezwa ili kujumuisha malipo kama hayo. Uzoefu pia umeonyesha kuwa kwa sababu uwepo wa makampuni ya uchimbaji uko wazi zaidi kuliko wa makampuni ya gesi na mafuta, makampuni haya ya uchimbaji yanahakikisha jamii inaelewa kuhusu uwepo wao pale mahali na umuhimu wa malipo wanayoilipa serikali. · Ubora wa wa data za mapato miliki ya jamii: kwa data ambazo tayari zimeisha tengenezwa na zinapatikana, kama zimekaguliwa kwa viwango vya kimataifa au bado zina tengeneza mwelekeo wa wigo wa maamuzi ya EITI. 20 · Mtazamo wa umma juu ya kiwango cha uwazi kwenye nchi: Bila kuhimili taarifa zinazotolewa na serikali na makampuni, mtazamo wa uma juu ya uhakika wake kwa ujumla umekuwa pia ni kitu muhimu. · Rasilimali zilizopo kukamilisha mchakato wa EITI: Jambo la msingi kwenye wigi wakati mwingine ni suala la kiasi cha rasilimali watu na fedha kilichopo kwa ajili ya shughuli husika, iwe toka serikalini au toka kwa wafadhili wanaounga mkono programu ya EITI. Kwa ujumla ukadiriaji wa sababu hizi umesaidia wadau kuweka mwelekeo wa programu ya EITI kwenye nchi zao. Kwenye nchi ambazo taarifa kidogo sana zilikuwa zimetolewa, au kwenye nchi ambazo ubora wa data hauridhishi umma, wadau wa EITI wanaweza kuamua kutumia mchakato mpana na unao angalia mambo kwa undani zaidi. Kwa nchi ambazo data za ubora wa juu zipo kwenye milki ya umma mchakato wa ngazi ya juu zaidi wa EITI utakuwa unafaa ili kutengeneza ushiriki mkubwa wa wadau mbali mbali na kuleta data za EITI zilizoripotiwa pamoja. Uzoefu unaonyesha kuwa wigo wa EITI unawekwa kwenye mapitio na unaboreshwa na kubadilishwa inapobidi, ndio maana baadhi ya nchi zilianza na programu finyu na baada ya kupata ushauri na kuzalisha ripoti ya kwanza ya EITI, zikaamua kuongeza wigo wa programu zao. Mtindo huu wa kufuata hatua unaruhusu kujifunza na uaminifu kujengeka baina ya wadau kabla ya maboresho ya wigo huo. Jambo la Msingi la Kujifunza Uzoefu wa nchi kadhaa kama unavyotazamwa na Benki ya Dunia ni kuwa nchi zenye programu ya EITI iliyopana zaidi zimetengeneza ripoti zenye ubora wa juu zaidi na zimenufaika zaidi na mchakato wa EITI. Taarifa zaidi kuhusu mradi zinawasilishwa katika mpango unaoeleweka na bora zaidi. Hata hivyo kuna suala la kungalia matumizi ya fedha na manufaa yanayotokana na matumizi hayo: Baadhi ya nchi zimekuwa kwenye wakati mgumu kupata uwiano kati ya wigo wanaotaka kuufikia na ule ambao 21 unaendana na rasilimali walizonazo. Nchi hizi zinaona kuwa jinsi wigo wa mchakato wa EITI unavyozidi kuwa mkubwa, fedha nyingi zaidi zitahitajika na rasilimali watu itatakiwa kuongezeka hii itahusisha pia kuongezeka kwa muda wa kutengeneza ripoti ya EITI. Kwa ukweli nchi zote zinazoongeza gharama zake za EITI huwa zinajilipa kwa namna moja au nyingine (kwa mfano kuongezeka kwa ukusanyaji wa mapato), lakini wadau wanahitaji kuwa bayana juu ya uwiano uliopo kwenye kupata wigo wa programu ya EITI. EITI vile vile ni mchakato ambao wadau wanajifunza mambo mengi wakati wa utekelezaji. Ndio maana baadhi ya nchi huwa zinaamua kuanza na mchakato ambao una wigo finyu na kuendelea na mkakati mpana zaidi baada ya kuandaa ripoti ya kwanza. URIPOTI, USULUHISHI NA UKAGUZI WA MCHAKATO WA EITI Vigezo vya EITI vinahitaji usuluhishi na uchapishaji wa data za malipo na mapato ambazo zilitakiwa zikaguliwe kwa viwango vya kimataifa. Hii inahakikisha kuwa data zinazotumika kwenye EITI zinafikia viwango vinavyokubalika. Kuna namna kadhaa za ukusanyaji, usawazishaji na mara nyingine ukaguzi wa data za mapato au matumizi kwa nchi mbali mbali zinazotekeleza EITI. (Hii inatokea zaidi kwa nchi zenye shughuli za uchimbaji mafuta, gesi na madini, kwa sababu mifumo tofauti inatumika kwa kuelezea na kuripoti katika ngazi ya taifa). Mfano wa ripoti za EITI umeambatanishwa kwenye CD. Kabla ya kupitia tena mafundisho toka kwenye njia hizi mbali mbali, ni muhimu kuwa bayana kwenye maneno yanayotumika kwenye mchakato wa EITI. Hivi sasa nchi zinazo tekeleza EITI zimekubaliana na mambo manne kwenye ukaguzi/ usawazishaji kwa kuzithibitisha ripoti za EITI. Mambo hayo ni haya yafuatayo:-; · Makubaliano: Katika nchi nyingi, makampuni na mashirika yanayomilikiwa na serikali pamoja na wakala wa serikali wanawajibu wa kutengeneza tamko la fedha la mwaka ambalo linakaguliwa katika viwango vya kimataifa. Katika hali kama hii mchakato wa wadau 22 mchanganyiko ambao una kubaliana na kuchapisha data hizi unaweza kuwa unatosha kufikia vigezo vya EITI. Kwenye utaratibu huu makampuni yana kusanya mfumo wa data wa EITI uliokamilika, wakaguzi wao wenyewe wanaweza kusema kuwa data hizo zimetoka kwenye tamko la fedha lililo kaguliwa katika viwango vya kimataifa. Msimamizi anapokea data hizo na kuziangalia kama data hizo zinaendana. Msimamizi atatafuta taarifa toka kwa kampuni au toka kwa serikali (kama kuna utofauti utakaoonekana kati ya viwango vilivyoripotiwa) na ataomba data zaidi kuelezea utofauti uliojitokeza. Data zilizokusanywa na tofauti zozote ambazo hazija elezewa pamoja na mapendekezo ya uboreshaji vitaripotiwa kwenye ripoti ya EITI na msimamizi. · Makubaliano kutokana na ukaguzi finyu: Mabadiliko katika makubaliano yaliyotumika hapo juu ambayo baadhi ya nchi zimetumia ni kwa msimamizi (au kampuni tofauti) kufanya ukaguzi mwingine wa tamko la fedha, pamoja na ule uliofanya awali kwa kampuni ambazo hazija kaguliwa katika viwango vya kimataifa. Mabadiliko haya yanaweza kutokea katika nchi ambazo ubora wa tamko la fedha la kampuni zinazo ripoti una mchanganyiko, kukiwa na baadhi zilizokaguli kwa viwango vya kimataifa na baadhi hazija kaguliwa katika viwango hivyo. · Makubaliano na majaribio ya uchunguzi kwa mapatano maalum: Kwa baadhi ya nchi kampuni ya ukaguzi ina teuliwa kuangalia data za malipo na mapato kama ilivyo elezwa hapo juu. Na kuliziba hili kwa majaribio finyu ya kipengele maalum cha kampuni au akiba ya serikali ambayo ndio msingi wa taarifa zitolewazo kwa ajili ya mchakato wa makubaliano. (Kwa mfano kampuni ya ukaguzi inaweza kuhoji uhalali wa gharama ambazo makampuni yameombwa kupunguziwa kama punguzo la kodi, hivyo kuhakikisha kuwa makampuni yanatumia thamani sahihi za masoko kupata thamani ya uzalishaji. · Ripoti za EITI zilizokaguliwa: Katika mfumo huu kampuni ya ukaguzi inateuliwa kufanya ukaguzi wa data zote zilizotolewa kwenye ripoti za EITI za makampuni yote na wakala wa serikali waliohusishwa katika mchakato huu, na kutoa mapendekezo ya kichunguzi kuhusu EITI ripoti yanayoendana na viwango vya kimataifa. Utaratibu huu kwa asili yake ni wa kiundani sana. Unahusisha kuangalia usahihi madhubuti wa mapato na matumizi na ukamilifu wake; pia 23 unahusisha uthibitishwaji wa mali na mtiririko wa pesa. Hivyo basi Kampuni ya ukaguzi ya EITI linahitaji fedha za kutosha kukamilisha zoezi hili; pia litahitaji hadidu za rejea zitakazo ipa uhalali na ruhusa yote kuona tamko la fedha la serikali na makampuni na rekodi kuhakiki data na ripoti zilizokaguliwa. Kutokana na gharama na mapana yake, njia hii ya kufanya ukaguzi kamilifu imetumika kwenye nchi chache tu. Hii ni kutokana na kukosa kiasi cha taarifa ambazo kampuni inabidi izitoe kama sehemu ya makubaliano, ambazo ni nyingi na zinahitaji jitihada ya juu kuzipata kuliko kiasi cha taarifa kitakachohitajika wakati wa ukaguzi wa ziada. Kaguzi hizo zimeongeza uwazi na uwajibikaji, na nchi zilizopitia ukaguzi huu mara nyingi zaidi ya kulipia ukaguzi huu wenye matokeo ya mapato na malipo yaliyoboreka. Mchakato wa EITI na uthibitishwaji wa ndani wa data zilizoripotiwa katika hali hii sio tu unajibu swali hili " ni nini mapato na matumizi yaliyoripotiwa" lakini pia unajibu swali hili "Makampuni yalilipa yalichotakiwa kulipa kwa serikali kama ilivyo kwenye mikataba yao na sheria ya kodi?" Mahali ambapo programu ya EITI inajumuisha aina hii ya uchunguzi, nchi zimeona ni muhimu kufikiria kwa undani kutoka mwanzo kuhusu mchakato ambao wakala wa makusanyo ya mapato wataweza (katika malengo ya kati na marefu) kuchukua jukumu la kufanya kaguzi za malipo ya makampuni. Aina hii ya utendaji inafanikiwa kama ikiwa inafanyika mara kwa mara na kama shughuli ya serikali inayoweza kukisiwa kuliko kutokea kama sehemu ya programu ya EITI. SANDUKU 3.2 AINA NYINGINE ZA UKAGUZI Ripoti ya kawaida ya EITI inagusia kwenye nini kimelipwa na nini kimepokelewa ­ yaani inahusika na kukusanya taarifa kwa kutegemea matamko ya fedha yaliyopo na mtiririko wa mapato. Baadhi ya nchi zimechagua kutekeleza ukaguzi wa undani. Kaguzi hizo zinajumuisha; 1. UKAGUZI WA MADHUBUTI: Hizi ni kaguzi zinazotumika kupima kiasi na ubora asili wa matokeo ya shughuli za uchimbaji mafuta, gesi na madini, kwa sehemu mbali mbali kwenye uzalishaji, utengenezaji na usafirishaji. Aina hii ya uchunguzi inafaa zaidi kwa nchi ambazo 24 mapato ya nchi yanategemea hisa za uzalishaji (yaani, kiwango cha uzalishaji kinachopitipitishwa kwa serikali) na pale ambapo inahisiwa kuwa kiwango cha uzalishaji ni zaidi ya kile kinacho ripotiwa na kulipiwa kodi. Ukaguzi madhubuti pia unatumika kutambua pale ambapo uzalishaji unapotea kati ya hatua mbili ­ kwa mfano kwa kupitia upotevu au wizi kiasi cha mafuta yanayofika kwenye sehemu ya usafishaji au usafirishaji ni pungufu ya kilichotakiwa kufika. Pia zinatumika kutambua pale ambapo ubora wa uzalishaji unabadilishwa au kuripotiwa tofauti ­ kwa mfano pale mafuta ya ubora wa juu yanapochanganywa na yale ya ubora wa chini, au usafi wa madini unapewa kiwango cha juu au cha chini. 2. UKAGUZI WA MCHAKATO: Aina hii ya ukaguzi inatumika kugundua jinsi fedha zinavyo lipwa, kukusanywa na kugawanywa tena. Kaguzi hizi ni muhimu kwa kuwa kuna namna nyingi ambazo mapato ya serikali yanaweza kupotea kama mifumo hii haifanya kazi kwa ufanisi. Kwa mfano kama mapato yanakusaywa na wakala wa serikali ambae sio benki kuu ya nchi hiyo, wakala anayekusanya malipo hayo anaweza kuchelewesha uhamishwaji wa pesa kwenye benki kuu ili kupata faida kutokana na pesa zilizokusanywa (wakati huo makubaliano ni kati ya kampuni na benki kuu). Tofauti hizi za muda zinaweza kutumika kupotosha mapato kwani bei za rasilimali hizi zinabadilika kila siku ­ mara nyingine kwa kiasi kikubwa katika muda mfupi sana. Vile vile kwa kuwa mauzo ya mafuta gesi na madini yanahusisha matumizi ya fedha za kigeni, tofauti ndogo katika kuripoti muda halisi wa mauzo inaweza pelekea faida ambayo haipitii kwa wakala wala benki kuu. 3. KAGUZI KINYUME NA MKATABA: Kwenye nchi nyingi, makubaliano tofauti tofauti yanafanyika kwa kila mgodi au kisima. Hii ni kwa sababu gharama, hatari na ugumu wa uziduaji unatofautiana kutoka mradi mmoja hadi mwingine. Kisima kilicho karibu na pwani , au kinachonufaika na miundo mbinu ya uma itakuwa na hatari na gharama za kiwango cha chini kwa kampuni kuendelea na uzalishaji, kwahiyo italipa kodi na hisa za uzalishaji za kiwango cha juu kuliko kisima ambacho kiko mbali na pwani kwenye kina kirefu. Huu mradi mwingine utakuwa na gharama zaidi na hatari nyingi katika uzalishaji, na kampuni itahitajika kutengeneza njia zake binafsi za usafirishaji, mradi wa aina hii unaweza kulipa kodi na hisa za uzalishaji za kiwango cha chini. Kwa sababu ya tofauti hizi za mikataba, baadhi ya nchi zimeamua kufanya "ukaguzi kinyume na mikataba" ili kuhakikisha kuwa makampuni yanalipa kodi na hisa sahihi za uzalishaji. 25 Mtazamo kuhusu aina nyingine za ukaguzi Katika utekelezaji wa EITI kwenye nchi nyingi, kumekuwa na mtazamo wa umma kuwa rushwa na ubadhilifu kwenye sekta hii inahusisha wizi wa moja kwa moja wa mafuta, gesi au madini ­ na wigo wa EITI unazungumzia hili. Kwenye baadhi ya nchi (Kwa mfano, kwenye nchi zenye mabomba yaliyo nje au ambapo vitu vinamilikiwa kinyume na sheria), hii inaweza kuwa ndivyo ilivyo na ukaguzi wa zaidi unaweza kusaidia. Hata hivyo uzoefu unaonyesha kuwa rushwa na ubadhilifu kwenye tasnia ya uziduaji ni kama wizi wa fedha, kama mifumoko ya bei isiyoelezeka, gharama za uhamishaji, mauzo ya chini ya bei ya soko na kuendelea. Hii inaonyesha kuwa ukaguzi mchakato au ukaguzi kinyume na mikataba ni muhimu kwa kugundua rushwa na ubadhilifu kama ulivyo ukaguzi madhubuti. Kwa malengo ya muda mrefu inaweza kushauriwa kuongeza uwezo wa usimamizi wa makusanyo ya mapato ya sekta ili kupima ulinganifu wa mikataba na malipo ya kodi kwa umakini. MAJADILIANO KUHUSU MALIGHAFI Makampuni yote yanayo fanya shughuli zake katika nchi husika yatakuwa ni sehemu ya mchakato wa kuripoti data za malipo kwa msimamizi. Lakini "kitabu cha asili cha EITI" kinaweka mipaka kwenye utaratibu huu ambapo utekelezaji unajali kupunguza matumizi ili kuweza kuweka kiwango cha malighafi kwenye kiasi cha malipo au ukubwa wa makampuni yaliyo katika nchi husika (ukiacha malipo au kampuni ndogo) kama ilivyo elezewa kwenye Picha 3.1. 26 PICHA 3.1 VIWANGO VYA MALIPO NA MAKAMPUNI Makampuni Kizingiti cha chini cha Malipo machache Malipo mengi au yote viwango vya kampuni makubwa yanawekwa yanawekwa wazi na wazi na makampuni makampuni mengi au mengi au yote yote Malipo machache Kizingiti cha chini cha makubwa yanawekwa Malipo mengi au yote viwango vya kampuni wazi na makampuni yanawekwa wazi na machache makampuni machache Kizingiti cha juu cha Kizingiti cha chini cha Malipo viwango vya malipo viwango vya malipo Viwango vya Malipo: Baadhi ya malipo yaliyoripotiwa na makampuni yanaweza kuwa si sahihi, na mchakato wa kukusanya data za nyongeza kwenye biashara ndogo kama hii unaweza kuzidi manufaa yake. Katika hali kama hiyo nchi inaweka viwango vya kutimizwa ambavyo vitaweka kando baadhi ya mambo madogo yasiyo fikia kiwango kilichowekwa. Viwango vya Makampuni: Kwa kuwa ukubwa na uzalishaji wa makampuni yaliyomo kwenye nchi yanatofautiana, serikali itaweka viwango vinavyotakiwa kufikiwa na makampuni na makampuni yatakayokuwa chini ya viwango hivyo yatatakiwa kuripoti EITI. Matumizi ya Maamuzi Kupata viwango vinavyotakiwa kutimizwa mara nyingi inaweza kupelekea mijadala migumu. Maelezo kuhusu nini ni kiwango cha kutimizwa na nini sio ni suala la maamuzi na linabadilika kwa nchi tofauti, na pia kwa makundi ya washikadau tofauti katika nchi. Hatimaye nchi zimeamua kuweka viwango vya kutimizwa kwa ufanisi kwa sababu inaruhusu mchakato kuendelea kwa haraka bila kuingia gharama na muda wa ziada ambao ungehitajika kushughulikia biashara na makampuni madogo. 27 Hakuna viwango vilivyowekwa tayari kwa nchi zinazo tekeleza EITI. Uzoefu unaonyesha kuwa makundi viongozi ya washikadau yanahitaji kuviweka viwango hivi vya kufikiwa kwenye mapitio ili kuhakikisha gharama na ufanisi wa mchakato na pia kulinda heshima ya mchakato mzima wa EITI ambao unaonekana kuwa si wa uwazi sana. Jaribio la mwisho kama viwango vya kutimizwa vilivyowekwa ni sawa au la ni kuwa hakutakuwa na madhara ya viwango hivyo au madhara yoyote makubwa kwenye uripoti wa data za EITI kama matokeo ya kuweka kando hizo ripoti za EITI. Aina ya Malipo Baadhi ya nchi zinaamua kulishughulikia hili suala la viwango vya kufikiwa kwa kuweka kando baadhi ya vyanzo vya mapato ambavyo vinachangia kwa kiasi kidogo sana kwenye pato la taifa. Kwa mfano aina moja ya kodi inaweza kuchukua asilimia 20 ya mapato yote ya tasnia ya uziduaji wakati aina nyingine ya kodi inachukua asilimia 0.1 tu. Katika hali kama hii inawezekana kuiweka kando hii yenye mchango mdogo bila kuwa na madhara yeyote katika mchakato mzima. Ni muhimu kwa wote walio teuliwa kupitia ripoti za EITI yaani makundi ya wadau na wasimamizi; kuhakikisha kuwa viwango vyote vya kufikiwa vya malipo vilivyowekwa kwenye mkataba vinawekwa pia kwenye ripoti ya EITI. Hii ni rahisi kuitimiza kwa kumtumia afisa wa ngazi ya juu katika kampuni husika kutoa ushahidi wa maandishi kuwa viwango vyote vya vyanzo vya mapato vimewekwa bayana; kwa kuchapisha mkataba mzima au sehemu ya mwaka wa fedha wa mkataba; au kwa kuutoa mkataba kwa msimamizi au mkaguzi kwa minajiri ya siri. Kuyagawa Makampuni Tendaji Njia nyingine ya kuweka viwango vya kufikiwa ni kwa kampuni kulipa mapato yote yanayohitajika ya tasnia ya uziduaji na kuziweka kando zile kampuni zote ambazo hazitafikia kwenye asilimia hiyo. Kwa mfano makampuni matano yanaweza kuwa na jukumu la kulipa asilimia 99 ya mapato yote ya tasnia ya uziduaji, wakati asilimia 1 iliyobakia inalipwa na makampuni madogo 10. Kiwango kilichowekwa kwenye asilimia 99 ya mapato kitajumuisha kiasi kikubwa mno cha mapato yanayolipwa na namba ndogo ya makampuni, na kuweka kando kiasi kidogo sana cha mapato kinacholipwa na namba kubwa ya makampuni. Nchi nyingi zinalielezea suala hili kwamba (haliko tu kwenye 28 tasnia ya uziduaji) kwa kuwa na kitengo cha walipa kodi wakubwa kinachoangalia wachangiaji wakubwa wa pato la taifa. MJADALA KUHUSU KIASI CHA WINGI NA UPUNGUFU Kwa kuongezea kwenye viwango vya kufikiwa, suala la msingi kwenye wigo wa EITI ni kiasi cha wingi wa taarifa ambacho ripoti ya EITI iliyochapishwa inajumuisha, ikifuatana na kutambua au kutokutambua malipo yaliyoripotiwa na kampuni na aina ya malipo. Itambulike kwamba suala la wingi/ upungufu ni kuhusu kiasi gani cha taarifa kimetolewa kwenye ripoti ya EITI iliyochapishwa. Kama sehemu ya makubaliano au ukaguzi wa makampuni yatahitaji kutoa kauli kamili ya upungufu kwa mkaguzi ili aweze kufananisha data za kampuni na zile za serikali. Kwa suala la viwango vya kufikiwa hakuna sera ya kimataifa ya EITI kuhusu hili; ni juu ya nchi yenyewe kuamua ni njia ipi itumike, kwa namna ambayo itafikia viwango vya kuidhinishwa. Mwishowe nchi zitafuata kiwango cha uwazi ambacho idadi kubwa ya wadau inakubaliana nacho. Kwa nchi nyingi suala hili limekuwa likileta mijadala yenye utata wa hali ja juu kwa wadau. Uzoefu unaonyesha kuwa nchi zinazoamua kutoa taarifa zake zaidi kuliko kutoa kidogo zinajijengea uaminifu kwa washikadau, lakini pia pamoja na kuwa mjadala ni muhimu isiwe sababu ya kuchelewesha utekelezwaji wa mkakati mzima. Njia tofautitofauti zilizochukuliwa na nchi malimbali zinaonyeshwa kwenye Picha 3.2 Picha inaonyesha kwamba kampuni au aina ya mapato yanaweza kuripotiwa katika viwango vinavyo badilika, kufuatana na wigo wa EITI maamuzi ya makundi viongozi: · Mkusanyo/ mgawanyo kwa aina ya mapato: Baadhi ya nchi za EITI zimeamua kuweka wazi taarifa za malipo na mapato kwa aina za mapato (kwa kampuni zote); kwa mfano kama serikali imepokea (jumla ya) $X kwenye mrahaba, $Y kwenye hisa za uzalishaji. Nchi nyingine za EITI zimeunganisha malipo kwa mapato yote ili kile kitakachowekwa bayana 29 ndio (jumla ya malipo yote yanayotolewa na mkampuni kwa serikali kwa mfano, Kampuni X ililipa $Y kwa serikali kwa kila aina ya mapato. · Mkusanyo/ mgawanyo wa Kampuni: Baadhi ya nchi zinaamua kuzitawanya taarifa za kampuni ili malipo yanayotolewa na kampuni kwa aina ya mapato yawe wazi. Hakuna nchi ya EITI iliyochagua kiwango cha juu cha ujumuishaji ­ jumla ya makampuni yote kwa mapato yote ambayo yataonyeshwa na serikali imepokea kiwango cha $X (toka kwa mapato ya aina zote) toka kwa kampuni zote. MALIPO NA MAPATO KWA SERIKALI NDOGO UGATUAJI MADARAKA Kwa baadhi ya nchi za EITI, malipo makubwa yana tolewa kwa serikali ndogo (ikijumuisha serikali ya mkoa, wilaya na mamlaka za manispaa, pamoja na viongozi wa jadi). Njia za aina hii ya malipo kwa serikali ndogo ni kama zifuatazo: · Malipo au miradi ya hiari toka kwa makampuni: Baadhi ya makampuni yanaamua kufanya malipo kwa serikali ndogo kwenye maeneo wanayofanyia kazi, (wakati mwingine za hali ya juu)mipango ya maendeleo ya jamii ambayo italeta bidhaa za umma ( kwa mfano shule, vituo vya mafunzo, vituo vya afya, barabara na n.k) kwa watu walio katika maeneo yanayoathiriwa na shughuli zao. 30 PICHA 3.2 MKUSANYO WA MAKAMPUNI NA MALIPO · Malipo au miradi ya hiari toka kwa serikali kuu: Baadhi ya serikali zinatumia kiasi cha mapato waliyokusanya kutoa malipo maalum (yaani hakuna utaratibu maalum wa kiasi gani au mara ngapi yatatolewa kwa serikali ndogo au huduma zaidi za uma kwa watu wanaoishi katika maeneo ambayo makampuni ya uziduaji yanashughulika. · Malipo ya lazima toka kwa makampuni: Katika baadhi ya nchi, kwa sheria au kwa makubaliano ya mkataba, makampuni yanatakiwa kutoa malipo fulani moja kwa moja kwa serikali ndogo, au kutoa hudumu fulani za kijamii kwa maeneo wanayofanyia kazi. Kwa nchi nyingi kuna vyanzo fulani vya mapato (kwa mfano, kodi za barabara au kodi za ardhi) ambazo zinakusanywa na serikali ndogo pekee. · Malipo ya lazima toka kwa serikali kuu: Baadhi ya nchi zina sheria ambazo zinaitaka serikali kuu kutoa asilimia fulani ya mapato ya kodi yaliyolipwa na makampuni kwa serikali ndogo ambapo makampuni ya uziduaji yanafanyia kazi zake. 31 EITI katika ngazi ya Serikali ndogo Suala la malipo kama ni ya hiari au ni lazima kwa serikali ndogo yanatakiwa yajumuishwe kwenye mchakato wa EITI, huwa inaamuliwa kwa kigezo cha viwango vya kufikiwa ­ yaani malipo yanayotolewa ni ya kiwango cha juu kiasi kwamba kutoyahusisha kwenye mchakato huu itamaanisha mkakati hauonyeshi hali halisi ya nini kampuni zinailipa nchi. Wakati ni nchi chache tu zilizojumuisha malipo ya serikali ndogo kwenye programu zao za EITI, nyingi zinalifikiria hilo. Mapato ya serikali kuu kwa ujumla hayatofautishiki mara yanapoingia kwenye bajeti ya jumla kwa hiyo ni vigumu kuioanisha mapato ya tasnia ya uziduaji na matumizi fulani ya serikali kuu. Kwa malipo au mgawanyo kwa serikali ndogo kuna uwezekano wa kutengeneza uwiano huo. Mambo yanayo husishwa na malipo kwa serikali ndogo kwenye programu za EITI yanajumuisha: · Pale ambapo malipo ni ya hiari (yaani hayana muongozo wowote wa kiwango cha kodi au kanuni), ni ngumu kwa mkaguzi kuchunguza kama data zilizo tolewa na kampuni au serikali ndogo ni sahihi na zimekamilika. · Pale ambapo malipo yanayotolewa kama matumizi ya kampuni kwa huduma kwa jamii iwe kwa hiari au kama amri, suala la uthibitishwaji wa bei huwa linajitokeza. · Uwezo wa serikali ndogo mara nyingine unakuwa finyu kushughulika na mahitaji ya kuripoti ya programu ya EITI katika hatua hiyo. SEKTA SAIDIZI NA BIASHARA ZINGINE ZIHUSUZO MAFUTA, GESI NA MADINI Kwenye nchi nyingi za EITI kumekuwa na mijadala kuhusu wapi pa kuikuza EITI kwenda kwenye sekta zingine zisizo husiana na mafuta, gesi na madini (kwa mfano misitu na uvuvi), au kwa mambo ya mafuta gesi na madini yasiyo 32 na uhusiano na utafiti au uzalishaji (kwa mfano usafishaji, uchenjuaji na usafirishaji) ­ au kwa yale makubaliano ya kibiashara ambayo kwa usanifu yameacha nje ya wigo wa vigezo vya EITI (kwa mfano utoaji wa leseni za uziduaji au matumizi kwa umma ya bajeti ya taifa) Kwa karibu programu zote za EITI, makubaliano haya ya kibiashara yako nje ya wigo wa mkakati wa EITI. Nchi zimeona kuwa kuna sababu za msingi kufanya EITI iangalie zaidi mafuta, gesi na madini: · EITI yenyewe kwa upande wa mapato na malipo ni changamoto: Kutengeneza mlingano wa data za mapato na malipo unaojitosheleza toka kwenye sekta moja inaweza kuwa shughuli ngumu, bila hata ya kuongeza sekta. · Kuongeza sekta ina maana kuongeza idadi ya wadau: kwa kubaki kwenye mafuta, gesi na madini, EITI itaweza kuendelea kwa kazi nzuri kwa kuwa namba ya watu na mchakato utakuwa unaweza kusimamiwa. Kupanua programu ya EITI italeta hatari ya kuongeza namba kuwa ya wadau wenye mitazamo tofauti tofauti. · Tasnia ya uziduaji haihuishwi: Kwa asili yake tasnia ya uziduaji inahusisha usimamizi wa rasilimali zinazokwisha. Mapato mengine ya mafuta, gesi na uchimbaji Katika sekta ya uziduaji , baadhi ya nchi zinazotekeleza EITI zimejadili kuhusu kujumuisha makubaliano mengi ya kibiashara zaidi ya yale ya utafiti na uzalishaji kama mapato na malipo yanayohusiana na usafirishaji (kwa mfano gharama za mabomba zinazoweza kuleta mapato makubwa kwa serikali) na uchenjuaji (kwa mfano gharama za usafishaji mafuta au ukolezaji madini ambazo shughuli za namna hii zinaweza kujumuisha kama sehemu ya uzalishaji na usafirishaji). Kuhusu makubaliano ya kibiashara nje ya utafutaji na uzalishaji, baadhi ya nchi (sio zote) zimejumuisha mapato hayo kwenye wigo zao za EITI (kwa mfano , malipo ya makampuni ya kusafisha mafuta). Pamoja na kuwa kujumuisha mapato haya ni kutengeneza mazingira magumu ya kazi na haipo kwenye 33 vigezo vya EITI, nchi inaweza kuona umuhimu "kufuata njia ya makubaliano ya kibiashara kwenye mafuta, gesi na uchimbaji madini ili kupata uelewa mzuri wa mtiririko wa fedha kwa sekta nzima, na ikiwezekana kupata uelewa mzuri kuhusu uhusiano kati ya thamani ya mkondo unakoelekea na kule ulikotokea, makubaliano ya kibiashara (yahusianayo na utafutaji na uzalishaji). Uzoefu unaonyesha kuwa wadau wanaofikiria kupanuka kwa EITI zaidi ya malengo yake ya msingi ya utafutaji na uzalishaji inaweza kuangalia (i)kama EITI yenyewe imewasilisha kwa kiasi cha kuridhisha, ikihusisha uthibitishaji wa nje unaoridhisha (ii) kama upanukaji huo wa wigo wa mkakati wa EITI una hatari ya kuunda mkakati ambao gharama zinazidi manufaa. Hata hivyo uzoefu unashauri kuwa, kuongeza uwazi kwenye sekta moja na aina ya makubaliano ya kibiashara inaongeza uhitaji wa uwazi kwenye sekta nyingine na makubaliano mengine ya kibiashara. Zaidi ya hapo kwenye baadhi ya nchi (kwenye nchi zinazozalisha mafuta zaidi) mifumo ya makubaliano ya kugawana uzalishaji ­ PSA inatumika ambapo mafuta au gesi iliyozalishwa inagawanywa kwenye hisa kati ya makampuni yaliyozalisha na serikali ("gharama ya mafuta" na "faida ya mafuta" kwa ajili ya gharama na faida na hisa za serikali za uzalishaji). Hisa za serikali huwa zinaachwa kwa kampuni iliyozalisha na kuziuza kwa niaba ya serikali, au kwa kampuni za serikali au wakala wa masoko, au kwa wakala mwingine. Katika hali hii umakini unahitajika kwenye mchakato wa EITI kuwa na uhakika kuwa hisa za uzalishaji za serikali zinatumika ipasavyo. Wakati baadhi ya nchi zinafikiria kujumuisha thamani ya fedha ya PSA kwenye wigo wa programu ya EITI, utendaji katika nchi nyingi za EITI umekuwa ni kwa kuripoti ujazo halisi tu. Makampuni zalishaji yasiyomilikiwa na serikali yanaamini kuwa fedha za PSA sio tatizo kwao ­ yaani kampuni inatakiwa izingatie jinsi inavyotoa taarifa za ujazo wa uzalishaji na jinsi ulivyo gawiwa. 34 Mwisho, kuna nchi ambazo zina vyote tasnia kubwa za mafuta, gesi na uchimbaji madini. Nchi hizi zimekuwa na mpango wa kuweka tasnia zote kwenye mpango wa kazi wa EITI, ila mara nyingi wanaanza kuangalia zaidi kwenye sekta iliyo tawala zaidi ya zingine. Hii imeruhusu nchi hizi kuendelea katika kiwango kinacho simamika na kutumia mafunzo yaliyopatikana toka kwenye utekelezaji wa EITI kwenye tasnia moja hadi nyingine, na tasnia ndogo hapo baadae. KUTOFAUTISHA KATI YA EITI HALISI NA "EITI YA ZIADA" Kutokana na mgawanyiko wa programu za EITI ambazo zimekuwa zikitekelezwa na nchi mbali mbali, wadau wapya kwa EITI mara nyingine wamepata shida kutofautisha kati ya EITI halisi na "EITI ya ziada". EITI halisi inajumuisha hatua zilizochukuliwa na nchi ili kujumuisha na kukubalika katika vigezo na uthibitishwaji wa EITI wa kimataifa. "EITI ya ziada" inajumuisha hatua ambazo nchi imezichukua zaidi ya vigezo vya kawaida vya EITI na alama za uthibitishaji. Sanduku 3.1 linaelezea uchaguzi ambao wafanya maamuzi wa nchi wanakutana nayo. Ni muhimu kufahamu kuwa kwenye mambo mengi yanayofanyika hakuna "sera" ya kimataifa ya EITI, na nchi tofauti zinatumia njia tofauti. Hivyo sanduku hili halionyeshi sera ya EITI katika mambo hayo. 35 JEDWALI 3.1 KUTOFAUTISHA KATI YA EITI HALISI NA "EITI YA ZIADA" MAHITAJI YA VIGEZO VYA VIASHIRIAEITI MFANO WA KWENDA ZAIDI YA EITI TUKIO HALISI HALISI YAANI "EITI YA ZIADA" Ukaguzi wa data Ambapo kampuni zimekwisha kukaguliwa Baadhi ya nchi zimeamua kukagua za makampuni na katika viwango vya kimataifa, hazihitaji tena sehemu au data zote za EITI zilizo serikali kwa kukaguliwa tena kwa mara ya pili wakati wa kusanywa na makampuni. viwango vya mchakato wa EITI. (Ukaguzi unaweza kuwa kimataifa muhimu kama makampuni hayana tamko la fedha lililo kaguliwa katika viwango vya kimataifa) Ukaguzi wa ziada Hauitajiki katika EITI Nchi moja imeamua kufanya ukaguzi wa mchakato au wa aina hii kama sehemu ya programu ukaguzi wa malipo ya EITI. kwa kuzingatia mkataba uliopo Idadi ya Makampuni yote yanayotoa malipo kwa Baadhi ya nchi zimeamua kuzitaka makampuni serikali yanatakiwa kuripoti kwa EITI nchi zote bila kujali ukubwa au yanayotakiwa kiwango cha malipo kuripoti kama kuripoti sehemu ya mchakato wa EITI. Vyanzo vya Vyanzo vyote "muhimu" vya mapato lazima Baadhi ya nchi zimeamua kujumuisha mapato yaripotiwe kama sehemu ya mchakato wa malipo yote bila kujali wingi wa vinavyotakiwa EITI. (Makundi viongozi yanahitaji kuamua mapato kama sehemu ya mchakato kuripotiwa chini vyanzo vipi vya mapato au ukubwa wa wa EITI ya EITI malipo) vinatambulika kama muhimu Bila kujali kama Hakuna hitaji la kuwasilisha ripoti ya EITI ripoti ya EITI katika muundo wowote. Hatahivyo, imewasilisha msimamizi au mkaguzi atahitaji kuonyeshwa katika mkusanyikotaarifa zote zilizotawanyika ili aweze au mgawanyiko kukamilisha kazi yake na kutengeneza ripoti sahihi ya EITI. (Kundi kiongozi litahitaji kuamua mipaka ya ripoti ya mwisho ya EITI na kiwango cha mtawanyiko wa taarifa. 36 MAHITAJI YA VIGEZO VYA VIASHIRIAEITI MFANO WA KWENDA ZAIDI YA EITI TUKIO HALISI HALISI YAANI "EITI YA ZIADA" Majumuisho ya Si vigezo vya EITI wala viashiria uthibitishaji (Swala la makundi viongozi katika malipo katika inashauri kama malipo kwa serikali ndogo nchi husika: kama malipo muhimu hatua ya serikali pia yajumuishwe. "serikali" haija elezewa yametolewa kwa serikali ndogo, ndogo kwahiyo inaweza kujumuisha au hivyo makundi viongozi yataangalia kutojumuisha serikali ndogo. jinsi ya kujumuisha malipo ya aina hiyo kama sehemu ya mchakato wa EITIkupata picha nzima ya malipo ya kampuni). Kujumuisha Kitabu cha marejeo cha EITI kinaangalia zaidi Namba ndogo ya nchi imepanua makubaliano ya malipo na mapato yanayo tokana na vyanzo programu zake za EITI kujumuisha malipo zaidi ya halisia au utafiti na uzalishaji tu. makampuni au malipo ambazo yale ya utafiti na hazihusiani moja kwa moja na na uzalishaji utafutaji na uzalishaji wa mafuta, gesi Kujumuisha sekta Haihitajiki na EITI Nchi moja imejumuisha misitu ndani zingine zaidi ya ya muundo wake mzima wa programu mafuta, gesi na ya EITI. uchimbaji madini 37 SURA 4: KUUANDAA MPANGO WA KAZI WA EITI UTANGULIZI Katika ngazi ya taifa nchi zinahitaji kuuandaa mpango makini wa kazi kwa ajili ya utekelezaji wa EITI (na mahitaji yake kwa masuala ya siasa na fedha). Mpango wa aina hiyo wa kazi unatakiwa kuwa na vigezo vya uthibitishaji vya EITI na unaruhusu nchi tekelezaji: · Kuandaa bayana kazi mbali mbali zinazotakiwa kufanyika ili kutekeleza programu ya EITI; · Kugundua utegemezi katika kazi tofauti tofauti na kuandaa mpangilio wa hatua mbali mbali; · Kufikia makubaliano bayana na wadau wote kuhusu jinsi programu ya EITI itakavyotekelezwa; na · Kutumia plani hiyo kama msingi wa kutafuta misaada ya kitaaluma na fedha (kama zitahitajika) toka nje kwa ajili ya program ya EITI ya taifa. UUNDAJI NA USHAURI JUU YA MPANGO WA KAZI WA EITI Usanifu wa Mpango wa Kazi Uzoefu wa chi tekelezi kwenye kuuandaa mpango wa kazi wa EITI unaonyesha kuwa ni mchakato unaojumuisha vyote kushauriana na kushirikiana; kwa maneno mengine inaundwa kwa kiasi kikubwa na aina ya programu ya EITI inayo tekelezwa. Majadiliano ya awali kati ya wadau wote wa mipaka ya programu ya EITI (angalia Sura 3: Upambanuzi wa Mipaka ya Programu ya EITI) ni kipengele muhimu cha maandalizi ya programu ya kazi, ikijumuisha masuala kama ya kujumuisha malipo yatolewayo kwa serikali ndogo; kufanya uthaminishaji au makubaliano au ukaguzi kamili; hatua muhimu; na mengineyo. Mwisho kiwango cha uharaka wa utekelezaji na rasilimali zilizopo zitaunda mpango wa kazi. Kwenye nchi nyingi, chombo ambacho kinajukumu la kuandaa mpango wa kazi wa EITI ni sekretarieti ya EITI au kitengo cha utekelezaji. Nakala ya mpango wa kazi inasambazwa katika mchakato wa kukusanya ushauri. 38 Nakala zinakuwa na ufanisi zaidi iwapo makundi viongozi ya wadau yamezipitia kwa undani, kuzielewa na kuzikubali kiofisi. Nchi ambazo zimetumia mipango ya kazi iliyotolewa na serikali zimekuwa zikipitiwa na kuwa haziendani na hali halisi kwa kuwa zinaelezea mambo yale tu ambayo serikali inayaona kuwa ni muhimu, na kuacha mambo ambayo yanaweza kuonekana ni muhimu na makampuni au wadau wa vyama vya kijamii. Uzoefu ni kuwa mipango ya kazi ya EITI sio nyaraka tu; zinapitia marekebisho yanayoendelea, na nchi nyingi zinazotekeleza EITI zinamaliza mzunguko wake wa kwanza na mipango ya kazi tofauti na ile waliyoanza nayo. Kwa kawaida baadhi ya matukio na mpangilio wa mambo unaonekana pale tu mchakato rasmi wa EITI unapoanza. Jaribio zuri la kuonyesha kama mpango wa kazi umekamilika, ni kwa kuusoma uhusiano kati ya madhumuni, na mpango wenyewe wa kazi dhidi ya vigezo na viashiria uhakiki vya EITI. Mpango mzuri wa kazi utakuwa na matukio ambayo yanawezesha nchi kutekeleza vigezo vyote vya EITI na kufikia viashiria uthibitishwaji vyote. Mpango wa kazi ni nyaraka ya umma na inapatikana kirahisi kwenye tovuti au sehemu zingine ambazo umma unaweza kuzifikia. Kama ilivyoelezwa, uzoefu wa nchi zinazo tekeleza EITI kwenye mipango ya kazi unabadilika kutegemeana na mipaka ya programu yao ya EITI na wadau. Hata hivyo uzoefu huo ukiunganishwa pamoja na muongozo wa kitabu cha marejeo cha EITI kwa pamoja vinaonyesha kuwa baadhi ya mambo yanahitaji kuwemo kwenye kila mpango wa kazi wa EITI. Jedwali 4.1 linaweka mambo hayo bayana. Mfano wa mpango wa kazi uliokamilika wa Timor Leste upo kwenye CD kama kiambatisho F. Muundo ambao nchi nyingi umezitumia pale unapoandaa mipango ya kazi unazingatia: · Madhumuni: Haya ni malengo ya juu ya programu ya EITI ­ kipengele cha msingi chenye mapana katika mkakati. 39 · Vitendo: Kweli kila madhumuni kuna mtiririko wa vitendo vya kutimizwa ili kuyafikia madhumuni hayo. · Mpangilio: Baadhi ya matukio hayataweza kufanyika mpaka matukio fulani sehemu nyingine kwenye mpango wa kazi yawe yamekamilika kwa mafanikio. · Ratiba: Inaonyesha tarehe ambayo tukio linategemewa kuwa limekamilika · Upande wenye jukumu: inaonyesha ni ushirika upo au mtu binafsi mwenye jukumu la kutimiza tukio. · Gharama na vyanzo vya ufadhili: inaonyesha gharama zinazotegemewa za kutimiza tukio pamoja na vyanzo vya ufadhili kwa mpango mzima wa kazi au matukio binafsi. SANDUKU 4.1 MAMBO YANAYOKUWEMO KWENYE MPANGO WA KAZI 1. KUWALETA PAMOJA WASHIKADAU: Mpango wa kazi utatakiwa uwe na mpango unaoelezea jinsi washikadau watakavyo tambuliwa na kuwa pamoja ­ na jinsi kundi kiongozi litakavyo teuliwa na shughuli zake zitakavyoungwa mkono. 2. KUONDOA VIKWAZO KWENYE UTEKELEZAJI: Mpango wa kazi utahitaji kuwa na mpango ambao unaelezea mambo ya: - Jinsi vikwazo katika utekelezaji vitakavyo tambuliwa - Jinsi ya kuhakikisha kuwa makampuni na wakala wote wa serikali yataweza kuweka wazi data zilizo kaguliwa kisheria. - Jinsi ya kuhakikisha kuwa makampuni yote yatashiriki katika mchakato. 3. KUJENGA UWEZO KWA SERIKALI: Mpango wa kazi utahitaji kuwa na vitendo vinavyo elezea mambo yafuatayo:-_ - Jinsi serikali itakavyo unga mkono kuendesha mchakato wa EITI - Jinsi sekretarieti au kitengo cha utekelezaji kitakavyo undwa na kuungwa mkono - Mahitaji ya serikali ili iweze kutengeneza ripoti yake ya mapato iliyopokea - Kuna nchi nyingine inayotekeleza EITI iliyo kwenye ukanda mmoja na nchi husika ambapo serikali inaweza kujifunza 4. KUJENGA UWEZO KWA MAKAMPUNI NA VYAMA VYA KIJAMII:Mpango wa kazi utahitaji kuwa na vitendo ambavyo vitaelezea mambo ya: - Jinsi makampuni yatakavyohusishwa kwenye mchakato - Mambo ambayo makampuni yatahitaji kufanya ili yaweze 40 kuandaa ripoti kwa kuzingatia tarakimu zilizokaguliwa ­ juu ya nini wameilipa serikali. - Jinsi vyama vya kijamii vitakavyohusishwa kwenye mchakato - Jinsi mambo yahusuyo kujenga uwezo wa vyama vya kijamii yatakavyo angaliwa ­ kwa mfano wana uelewa mzuri kuhusu tasnia ya uziduaji na ya malipo mbali mbali na mapato. - Kuna makampuni mengine au vyama vya kijamii kwenye nchi nyingine katika ukanda mmoja na nchi husika ambazo zina jihusisha na utekelezaji wa EITI ambako makundi ya nchi husika yanaweza kujifunza? 5. UTENGENEZAJI WA RIPOTI YA EITI: Mpango wa kazi utahitaji kuwa na mpango ambao unaonyesha mambo yafuatayo: - Mchakato gani wa ushauri utapitiwa ili kupata mipaka ya programu ya EITI? - Jinsi gani kampuni ya ukaguzi itateuliwa kuandaa ripoti ya EITI - Jinsi mfumo na muongozo wa uandishi wa ripoti kwa serikali na makampuni utakavyosanifiwa - Jinsi kampuni la ukaguzi litakavyo simamiwa na kulipwa - Jinsi ripoti ya EITI itakavyopitiwa na kusambazwa 6. USAMBAZWAJI WA PROGRAMU YA EITI: Mpango wa kazi utahitaji kuwa na mkakati unaaonyesha mambo ya: - Jinsi washikadau wote wanaoathiriwa au kupenda kujihusisha na mchakato wa EITI watakavyohusishwa. - Ni vyombo gani vya habari na mawasiliano vitatumika kuielezea EITI? - Ni jinsi gani taarifa juu ya mchakato na ripoti za EITI zitawasilishwa katika njia rahisi na ya kueleweka na kuweza kupatikana kirahisi na kila mahali kwa umma. - Jinsi gani ripoti za EITI zitasambazwa na kujadiliwa 7. USIMAMIZI NA UTATHMINI WA PROGRAMU ZA EITI: Mpango wa kazi utahitaji kuwa na mkakati ambao unaelezea mambo yafuatayo: - Jinsi programu nzima itakavyo simamiwa na ni nini kitakuwa kigezo cha mafanikio - Katika hatua gani programu itapitiwa ili kufahamu kama inafanya kazi vizuri, kama sivyo, ni jinsi gani mabadiliko yatafanyika. - Lini na vipi mabadiliko yatafanyika na ripoti ya uthamini kutolewa. 8. KUANDAA NA KUFADHILI MPANGO WA KAZI: Mapango wa kazi utahitaji kuwa na mkakati unaonyesha mambo yafuatayo:- - Jinsi mpango wa kazi wenyewe utakavyoandaliwa na kupitiwa - Nani atakuwa na jukumu la kufanya mabadiliko yeyote kwenye mpango wa kazi - Jinsi gani, ufadhili na rasilimali zitapatikana na kupangwa kusaidia mikakati yote ya mpango wa kazi. 41 MUDA WA UTEKELEZAJI Kwa kuangalia mipaka mbali mbali ya mipango ya kazi ya EITI, kuna utofauti kwenye muda uliotumika na nchi mbali mbali kuweka programu ya EITI. Baadhi wamekwenda kwa haraka na kufanikiwa kuandaa ripoti ya kwanza ya EITI ndani ya mwaka mmoja wa kujiunga na mkakati huu na kuunda makundi viongozi ya washikadau kusimamia kazi nzima ya EITI. Hata hivyo, Utekelezaji wa haraka haraka unakuwa na matatizo kwa sababu ya kukosa ushauri wa kutosha kutoka kwa washikadau ambao mara nyingi huwa unachelewesha uandaaji wa ripoti ya EITI. Kwa wastani imezichukua nchi kati ya miezi 18 ­ 24 kutoka kujiingiza kwao kwa mara ya kwanza kwenye mkakati huu mpaka kutoa ripoti ya kwanza ya EITI ­ na muda mrefu zaidi kwa baadhi ya sehemu kukiwa na sababu maalum. Baadhi ya nchi kwa mfano, programu ya EITI imecheleweshwa na uchaguzi, mabadiliko ya serikali au mabadiliko ya maafisa wa ngazi za juu na mawaziri. Hata hivyo, asili ya utekelezwaji wa EITI ni kuwa kuna nchi chache sana za EITI ambazo hazikuwa na haja ya kupitia maendeleo yake ya EITI na kuweka marekebisho kwenye mchakato. Hiki si kitu kibaya ­ EITI ni mchakato wa kitaalamu ambao unahusisha washikadau wengi, na nchi nyingi zinajifunza jinsi ya kutekeleza kwa kuanza na kuingia kwanza kwenye mchakato wenyewe. Sababu zinazoweza kuongeza au kupunguza kasi ya utekelezaji zinajumuisha: (i) upana wa programu ya EITI inayotakiwa kuwasilishwa (ikiwa na programu ngumu zaidi zinazohitaji muda mrefu kuzitekeleza) (ii) Msimamo wa kiongozi wa EITI (sababu moja kubwa ya kuendesha EITI kwa urahisi) (iii)ushirikishwaji wa makampuni na vyama vya ushirika, na (iv) ukosefu wa rasilimali watu na fedha. UFADHILI WA PROGRAMU YA EITI Kwenye nchi zinazo tekeleza EITI, sekta za mafuta, gesi na uchimbaji madini zinakuwa ni tasnia ya mabilioni ya dola. Kutokana na hili hata uwekezaji mdogo ukiongezwa uwazi unaweza kuleta manufaa makubwa kwenye mapato. 42 Gharama kubwa ya kutekeleza mkakati ni kwenye muda na kujitoa kwa wadau mbali mbali ambao watatakiwa waonyeshe msimamo kwenye kusimamia na kuongoza programu ya EITI. Kwa kuongezea kwenye fungu la uhakika na la kudumu toka kwenye bajeti ya serikali vyanzo vingine vya ufadhili na misaada ya kitaalamu ambavyo nchi tekelezi zimetumia inajumuisha: · Ufadhili wa EITI toka kwenye amana ya wahisani inayo simamiwa na Benki ya Dunia: Amana ya EITI toka kwa wahisani mbali mbali (MDTF) inayosimamiwa na benki ya dunia inatumiwa na wafadhili wengi kuweka ufadhili wao kwa nchi zinazotekeleza EITI. Amana hizi zinatoa ufadhili moja kwa moja kwa nchi zinazotekeleza EITI na pia inatumika kutoa misaada ya kitaalamu (kwa kupitia washauri wa EITI) kwa nchi hizo. Ili kuongeza mapato yake, amana hii ina kawaida ya kuangalia rasilimali zake kwa nchi ambazo: (i) zimeonyesha msimamo wake kwa mchakato wa EITI na zina uwezekano mkubwa wa kuwasilisha ripoti za EITI ndani ya muda muafaka; (ii)zimeandaa mpango makini wa kazi za EITI an (iii) zimefikia vigezo vya kuchaguliwa kwenye MDTF. · Ufadhili wa kitaaluma na fedha toka kwa wahisani na Benki ya Dunia: Wahisani wengi wametoa pia misaada ya kifedha na kitaaluma kwa nchi zinazotekeleza EITI. · Makundi ya vyama vya kijamii vya kimataifa: mashirika kama, Taasisi ya kuangalia mapato; Muungano wa chapisha unachokilipa na Uwazi wa Kimataifa yanaweza kutoa ushauri na misaada kwa makundi ya vyama vya kijamii yanayoshiriki kwenye utekelezaji EITI. · Makampuni ya tasnia ya Uziduaji: Katika baadhi ya nchi makampuni yameonyesha msimamo kusaidia kwenye gharama za ndani za utekelezaji wa EITI na zile za makundi viongozi ya wadau, hata hivyo aina hii ya misaada lazima iwekwe mbali na utekelezaji (kwa mfano kuchangia kwenye mfuko wa taifa wa kuunga mkono EITI unaojitegemea) ili kuhakikisha kuwa hakuna mashtaka ya ushawishi usio sahihi kwenye mchakato wa EITI. Nchi ambazo zimepokea ufadhili kutoka kwa wahisani wengi mara nyingi zimeona ni vema kuwakutanisha mara kwa mara wafadhili hao, kitengo cha utekelezaji na makundi viongozi ili kuhakikisha kuwa hakuna uwazi au mchangamano kwenye ufadhili. Wakati vyanzo vya nje vya ufadhili vinaweza 43 kuwa muhimu kwenye kuanzisha programu ya EITI, haziwezi kutegemewa kutoa ufadhili wa kudumu kwa miaka mingi. Kwa sababu hiyo nchi nyingi zinazotekeleza EITI zinatafuta namna ya kuwa na fungu la kudumu kuwezesha ufadhiliwa EITI toka kwenye bajeti zao wenyewe ili programu hizi ziwe ni sehemu ya utendaji wa serikali. Jedwali 4.1 linaonyesha mfano wa bajeti ya programu ya EITI. Kwa hali halisi gharama ya programu ya EITI ina badilika kwa kutegemeana na mipaka ya programu yenyewe. Namba zilizo tolewa hapo ni za makadirio tu . Vile vile bajeti kwa kawaida inawasilisha kama sehemu ya mpango wa kazi na hivyo itaweka aina za matumizi yatakayotumika kwa matukio maalum. 44 JEDWALI 4.1 MFANO WA BAJETI YA EITI ILIYORAHISISHWA (KWA MWAKA) KITU GHARAMA MLIPAJI Kuunga mkono kazi na utendaji wa makundi viongozi $5,000 Serikali ya wadau (kwa mfano, kutoa usafiri kwa wanachama ili wakutane kwenye miji mbali mbaliinapobidi; upatikananji wa viburudisho; vifaa vya kuandikia; na kadhalika) Kuanzisha na kuendeleza kitengo cha utekelezaji (kwa $60,000 75% Serikali; 25% amana mfano, kulipa mishahara ya wafanyakazi, mambo ya za EITI kompyuta na vifaa vya mawasiliano; vifaa vya kuandikia na kadhalika) Kukodi kampini la ukaguzikushauri kuhusu uzalishaji $200,000 60% serikali; 40% amana wa mfumo wa kuripoti, na kukagua data za malipo na za EITI mapato kwa miaka miwili Mawasiliano na programu za usambazaji (utengenezaji $50,000 Misaada toka kwa wa nyenzo za EITI; kutengeneza website ya EITI; wahisani A kufanya makongamano na maonyesho ya barabarani ya EITI Kujenga uwezo na programu za mafunzo kwa wakala $50,000 25% amana za EITI; 50% wa serikali, makampuni na vyama vya ushirika Serikali; 25% vyama vya vinavyohusika na utekelezaji wa EITI ushirika vya kimataifa Msaada wa kiushauri kusaiidi kutengeneza taratibu/ $20,000 Misaada toka kwa sheria kuwezesha uripoti wa EITI kuendelea wahisani B Kukodi mthaminishaji wa kujitegemea $30000 Serikali (kwa mwaka) Jumla ya Fedha toka kwa wahisani wa nje $190,000 Wahisani wa nje Jumla ya Fedha toka serikalini $225,000 Serikali JUMLA KUU US$ 415,000 JUMLA 45 SURA 5: KAZI YA SERIKALI KWENYE UTEKELEZAJI WA EITI UTANGULIZI Wakati EITI ni mchakato wa washikadau mbali mbali, iko wazi kuwa ni serikali ndio itakuwa na changamoto ya utekelezwaji katika nchi husika. Sura hii ina angalia mambo ambayo serikali zimeyaangalia na ambayo zinatakiwa ziyaangalie ili kuweza kutekeleza EITI kwa mafanikio. Kwa kuongezea kwenye kuweka tamko bayana kwenye uamuzi wa kutekeleza EITI, kuhakikisha kuna rasilimali watu na fedha za kutosha, na kuteua kiongozi wa ngazi ya juu wa kuongoza EITI (angalia Sura 1: kuanza Programu ya EITI), kuna ngazi kuu tatu za kazi ambazo serikali imekuwa ikizizingatia kwenye mchakato wa EITI: · Kuunga mkono na kutoa Uongozi wa Kisiasa: kwenye nchi zote, serikali inatoa muongozo na njia za kisiasa (Sekretarieti au kitengo cha utekelezaji ili kusaidia kundi kiongozi la washikadau na kuandaa mpango wa kazi) na rasilimali za kuipeleka mbele EITI. · Kuweka misingi ya kisheria ya utekelezaji: Katika baadhi ya nchi kumekuwa na vikwazo vya kisheria ambavyo vimeathiri utekelezwaji wa EITI, ambavyo vimehitaji taratibu mpya au zilizoboreshwa au sheria kuruhusu, kwa mfano wa kuachiwa kwa data za EITI. · Kuweka bayana mapato ya serikali: kama sehemu ya mlingano wa data au mchakato wa ukaguzi, serikali inahitaji kutoa data za mapato yaliyotokana na tasnia ya uziduaji na uhakika wa data zilizotolewa. KUTOA MUONGOZO WA KISIASA NA KUUNGA MKONO MCHAKATO WA EITI Kuendesha mchakato unaoshirikisha washikadau wa aina nyingi kama ilivyo EITI inahitaji rasilimali za serikali zilizotolewa maalum kwa shughuli hii kuunga mkono kazi ya washikadau. Inahitaji msimamo wa hali ya juu sana kutoka serikalini na kwa viongozi hai na wa ngazi za juu wa kisiasa. Katika nchi zote zinazotekeleza EITI, hii imeisababisha serikali ihitaji kuunda sekretarieti ya EITI au kitengo cha utekelezaji kuelekeza mkakati. Katika hatua za awali za mkakati (japo mwaka wa kwanza), hii imekuwa mara nyingi ikihitaji mtu wa kudumu anayewekwa kwa ajili ya utekelezaji wa EITI. Timu hizi zimekuwa kubwa kwenye nchi ambazo zimechukua mipaka mikubwa zaidi 46 au kwenye nchi ambazo zina rasilimali za kutosha. (angalia sura 3: Upambanuzi wa Mipaka ya Programu ya EITI). Kazi za kitengo cha utekelezaji cha EITI ni: · Kuunga mkono kikundi kiongozi cha washikadau na kiongozi wa EITI: Kitengo cha utekelezaji kinaratibu maendeleo yote ya EITI, ikijumuisha kuitisha mikutano ya makundi viongozi; kugawa ajenda; makaratasi ya mikutano na kumbukumbu za mkutano; na kutoa usaidizi kwa makundi viongozi na kiongozi wa EITI kwenye maamuzi na ufuatiliaji. · Kuratibu nafasi ya serikali: EITI mara nyingi inahitaji kuhusika kwa wizara mbali mbali au mawakala wa serikali, kitengo cha utekelezaji kina shauriana na serikali ili kuja na msimamo madhubuti juu ya maamuzi yake kwenye mambo mbalimbali ya EITI. · Kuandika na kushauriana kuhusu mpango wa kazi wa EITI: Kuandaa na kushauri juu ya mpango wa kazi wa EITI. · Kuandaa rasilimali: kitengo cha utekelezaji wa EITI kinaelezea kuhusu rasilimali zinazohitajika yaani watu na fedha kukamilisha mpango wa kazi wa EITI ­ gharama ya kitengo cha utekelezaji na mpango wake wa kazi; gharama ya msimamizi au mkaguzi kukagua au kurekebisha data za malipo na mapato; na kikundi cha mawasiliano kushauriana na washikadau na kusambaza matokeo. · Kusaidia kugundua na kuweka bayana vikwazo vya taratibu na sheria za utekelezaji: Katika baadhi ya matukio hii imehitaji kitengo cha utekelezaji kuandika na kushauriana juu ya taratibu na sheria mpya. · Kusimamia zabuni na mchakato wa utoaji mikataba ya wakaguzi na wasimamizi: wakati kazi ya kampuni simamizi/ ukaguzi zinasimamiwa na kundi kiongozi, kwa kawaida ni serikali ndiyo inayotoa zabuni, kusaini mkataba na malipo kwa huduma inayohitajika. · Kumtambulisha msimamizi na kuwezesha uhusiano wake na makampuni ya uziduaji pamoja na wakala wa serikali. 47 · Kuratibu mahesabu ya mapato ya serikali kwa usawazishaji: kitengo cha utekelezaji kina ratibu wizara na wakala wa serikali ambazo zinapokea mapato toka kwa makampuni ya uziduaji kwa kutoa tamko la mapato ya serikali kwa msimamizi au kuziweka data bayana ili kumuwezesha mkaguzi kutoa kauli hiyo. · Kuwasiliana na kushauri kuhusu EITI: Katika mchakato mzima wa EITI, vitengo vya utekelezaji vinashauriana kwa mapana na wadau waliopo, ikijumuisha wale walio nje ya makundi viongozi, na ndio kiini cha kutoa taarifa juu ya mkakati kwa washikadau; kuendesha warsha, makongamano, na maelezo kwa vyombo vya habari kuhusu EITI; pamoja na kuiendesha tovuti ya EITI (angalia Sura 8: Uwasilishwaji wa EITI). Nchi tofauti zimekuwa na namna tofauti ya kuangalia vitengo vya utekelezaji viwajibike kwa nani. Katika baadhi ya nchi vinawajibika kwa kiongozi wa EITI; kwa baadhi ya nchi kwa wakala maalum wa serikali. Kwenye nchi zingine vinawajibika kwa makundi viongozi ya wadau. Mfano wa hadidu za rejea za sekretarieti ya EITI, huko Mongolia, inapatikana kwenye CD kama kiambatisho G. KUJENGA UWEZO KWA KITENGO CHA UTEKELEZAJI NA WAKALA WA SERIKALI Katika nchi nyingi utekelezaji wa EITI umehitaji vitengo vya utekelezaji, pamoja na wakala wa serikali anayehusishwa kwenye mchakato wa kuripoti, kutekeleza mpango bayana wa kujenga uwezo ili kuwaruhusu wawekezaji kuendeleza mchakato wa EITI. Baadhi ya ujenzi huu wa uwezo haukwepeki kuwa ni suala la rasilimali fedha ­ kwa mfano kulipa mishahara ya wafanyakazi wa kudumu wa EITI. Baadhi ya ujenzi wa uwezo unaweza fanyika kwa kupitia mafunzo mafupi. Nchi nyingi zinazoanza programu ya EITI zimejifunza toka kwa nchi jirani ambazo zimeshajiunga na mchakato huu. Hii ni kuandaa safari za mafunzo kwenda kwa nchi tekelezi au kwa kuwaleta washikadau wanaohusika na utekelezaji toka nchi tekelezi kuja kutembelea nchi ambayo inaanza programu ya EITI. Uzoefu unaonyesha kuwa vitengo vya utekelezaji vinavyofanikiwa ni vile:- · Vyenye rasilimali watu na fedha toka serikalini zinazoongezeka katika hatua za awali; 48 · Vina mawasiliano ya karibu na wanachama wa kundi kiongozi la washikadau na wanawajibika kwa maamuzi ya kikundi. · Vinaongozwa na mtu ambae ana uwezo wa kufanya kazi kwa ushirikiano na makampuni pamoja na vyama vya ushirika. · Vinaweza kumpata kiongozi wa EITI na wizara za serikali zinazohusiana na EITI, kwa urahisi · Viko kwenye wakala ambazo zina rasilimali zake za kutekelezea mkakati au inafahamu vizuri mchakato mzima unaohusika na kusimamia ufadhili unaotoka nje; na · Ina wafanyakazi wenye mchanganyiko wa uzoefu na ujuzi unaohitajika kutekeleza mkakati kama wa EITI. Katika baadhi ya nchi hizi zimefanikiwa kwa kukusanya wafanyakazi toka wakala mbali mbali wa serikali, au toka kwa wadau wengine, kuwaingiza kwenye kitengo cha utekelezaji. KUHAKIKISHA USHIRIKI WA JUMLA WA KAMPUNI NA MAMBO YA USIRI Mambo ya msingi mawili ambayo nchi zote zinazotekeleza EITI zinakutana nayo ni (i) jinsi ya kuhakikisha kuwa makampuni yote yameshiriki kwenye mchakato na (ii) jinsi ya kuelezea mambo ya usiri ambayo wakala wa serikali au makampuni yanaweza kuwa nayo. Mambo haya ni muhimu kuangaliwa katika hatua za awali za EITI kwa sababu kuhakikisha kuwa kampuni zote zinazo fanya kazi zinaripoti malipo yote yanayotakiwa na vigezo vya EITI. Pia ni mambo muhimu kwa kuwa ushiriki usiokamilika wa makampuni au kuondolewa kwa taarifa kwenye mapato muhimu kunaweza kugandamiza uwezo wa EITI ya nchi husika. Zifuatazo ni hatua mbali mbali ambazo nchi imezichukua: · Kuweka wazi kwa hiari: Makampuni yote yakubali kwa hiari kushiriki mchakato wa EITI. · "Barua ya kuliwaza": Baadhi ya nchi zimetoa "barua ya kuliwaza" kwa makampuni ili kuyahakikishia kuwa utoaji wao wa data kwa mtu wa tatu, hakutachukuliwa na serikali kama uvunjaji wa sheria au mkataba. 49 · Uwekaji wazi wa lazima: Baadhi ya nchi zimetoa agizo, kutoa kanuni mpya au kupitisha sheria mpya ambazo zinalazimisha ushiriki wa makampuni yote kwenye mchakato wa EITI. Njia za kujitolea zimefanikiwa kwenye baadhi ya nchi, lakini kwa baadhi ya nchi imegundulika kuwa ushirikishwaji wa hiari umesababisha baadhi ya makampuni kutokamilisha mchakato mzima. Wakati makampuni kwenye baadhi ya nchi yamewasilisha maoni yao juu ya sheria au kanuni zinazo lazimisha uwazi, nchi ambazo zimefanya hivi zimeona zinatengeneza usawa na mazingira ya mlingano kwa makampuni. Kila kampuni inatoa taarifa sawa sawa na mpinzani wake. Mwisho nchi zimeona ni vizuri kuhusisha mamlaka za kodi wakati wa hatua za awali za mchakato kwa sababu kunaweza kukawa na kodi ambazo ni siri kisheria na mtu wa tatu hatakiwa kujua kiasi cha kodi kinachotolewa. KUWEKA MISINGI YA KISHERIA YA UTEKELEZAJI Katika baadhi ya nchi EITI imekuwa ikifanyika kama kitu cha kujitolea, kwa ushirikiano ambao washikadau wote wamekubaliana. Katika nchi zingine, uboreshwaji wa kanuni zilizopo au sheria au kanuni mpya au sheria vimehitajika ili kuanzisha utekelezaji wa mkakati. Katika hatua za baadae, kutoa msingi wa kanuni au sheria sahihi imekuwa ni tukio linalochukua muda mwingi, katika baadhi ya nchi, lakini pia imekuwa muhimu kuelezea mambo yahusuyo uimara wa mchakato (kutoa rasilimali ili kuhakikisha kuwa ripoti za EITI zinatolewa mara kwa mara) na usawa baina ya makampuni (haja ya kuhakikisha kuwa makampuni yote yako katika mlingano kuhusiana na suala la EITI). Nchi ambazo zimetumia muda mwingi kutengeneza kanuni na sheria zimeweza kutekeleza mchakato wake kwa haraka kwa kuwa kanuni na sheria zinaelezea kazi za kila mhusika katika mkakati. Hata hivyo, baadhi ya nchi ambazo hazina misingi hiyo ya kisheria zimeonekana kuchelewa katika utekelezaji (kwa mfano kutokuwa na uwezo wa kuhakikisha kuwa makampuni yote yana toa 50 data zake au kama mkaguzi/ msimamizi akienda kwa makampuni yatamruhusu apitie data zao za mapato na malipo). Mambo ambayo kwa kawaida yamekuwa yakielezewa na kanuni au sheria za EITI katika nchi tofauti yanajumuisha: · Kuanzisha taratibu za msingi ­ kuorodhesha umuhimu wa taratibu za uwazi katika kutoa taarifa za malipo ya kampuni na mapato ya serikali na umuhimu wa uangalizi wa washikadau (kupitia kundi kiongozi) kwa malipo na mapato ya tasnia ya uziduaji. · Kutenga majukumu kwa kuunga mkono na kusimamia mchakato wa EITI kwa wizara au wakala wa serikali (au kundi kiongozi) iliyopewa jukumu. · Kuweka malengo ya baadae katika bajeti ili kutenga fungu maalumu kwa ajili ya kusaidia gharama za uendeshaji wa shughuli EITI zinazo endesha na wizara au wakala husika. · Kulazimisha uwekwaji wazi wa malipo yote yatolewayo na makampuni na mapato yote yanayopokelewa na serikali ­ mara nyingi kwa kuondoa mazingira ya usiri (kwenye makubaliano) ambayo yatazuia kutokea kwa hili. · Kuanzisha kiwango cha kuripoti data zinazokusanywa chini ya EITI (hii inaweza kutegemea tamko la fedha baada ya ukaguzi kufanyika katika viwango vya kimataifa). · Kulazimisha ushiriki wa makampuni yote ya mafuta, gesi na uchimbaji madini kwenye mchakato wa EITI. · Kuhitaji uteuzi wa msimamizi au mkaguzi wa kujitegemea na makundi viongozi ya wadau ili kukagua data za malipo na mapato; kumhakikishia mkaguzi/ msimamizi kuzipitia kumbukumbu za fedha za makampuni. · Kutengeneza mipaka ya kazi ya msimamizi/ mkaguzi ­ hii ni , kuamua kama ama msimamizi au mkaguzi atalinganisha data na kuchunguza mapungufu au kuendesha kazi ya ukaguzi, au kuendesha ukaguzi wa jumla wa malipo na mapato na pia kuamua jinsi ripoti ya mwisho ya 51 msimamizi au mkaguzi itakavyo chapishwa na data zitawasilishwa kwa undani wa kiasi gani. Mfano wa sheria za EITI uko Nigeria inapatikana kwenye CD kama kiambatisho H. KUWEKA WAZI MAPATO YA SERIKALI Aina na kiasi cha data za fedha ambazo serikali inatoa kwa mchakato wa taifa wa EITI unabadilika kutegemeana na mipaka ya programu ya EITI (angalia Sura 3: Upambanuzi wa Mipaka ya Programu ya EITI). Ambapo nchi zinafuata makubaliano ya EITI , kitengo cha utekelezaji cha serikali au mamlaka ya kodi imetoa ripoti ya data za serikali kwa mkaguzi binafsi kuhusu malipo yote ambayo wakala mbali mbali za serikali na wizara zimepokea kutoka kwa makampuni ya uziduaji (ikijumuisha mgao wa serikali ndogo). Utofauti wowote utakaotambuliwa na msimamizi kati ya data zilizotolewa na serikali na zile zilizotolewa na makampuni yamejadiliwa na pande zote na mara nyingine yameelezewa na kuambatanishiwa ushahidi wa malipo binafsi (kwa mfano kumbukumbu za malipo). Katika hali ambayo serikali inafuata muundo wa ndani zaidi wa EITI (ambapo data za EITI zenyewe zina kaguliwa), serikali imetoa mkaguzi mwenye kuzifikia akiba za wizara na wakala wanaohusika na tasnia ya uziduaji. Mpaka leo, uhusishwaji mpana zaidi juu ya ukaguzi katika nchi zilizojiingiza kwenye mchakato wa EITI (zaidi ya uwezekano wa kuwa wamekagua data za mapato ya serikali) bado iko kwenye hatua za awali, pamoja na kuwa, kutokana na ukaribu wao na mapato ya serikali kwa nchi mbali mbali, nchi hizi zinaweza kutoa mchango mkubwa kwa mchakato wa EITI. 52 SURA 6: KAZI YA MAKAMPUNI NA VYAMA VYA KIJAMII UTANGULIZI Makampuni ya kimataifa ya mafuta, gesi na uchimbaji madini, pamoja na vyama vya kijamii vya kimataifa, wameshiriki kwenye utekelezaji wa EITI kwenye nchi nyingi; lakini makampuni mengi na vyama vingi vya kijamii ni wapya kwenye EITI. Kiwango cha ushiriki kwa hizi kampuni na makundi zinabadilika lakini kuna maeneo makubwa 4 ambayo wamechangia: · Kusaidia uanzishwaji wa haraka wa mchakato wa EITI na kuongoza mkakati: Nchi nyingi zimeanza mchakato wa EITI kiasi kwa utetezi hai wa makampuni au vyama vya kijamii ambavyo vinahimiza serikali kujiingiza kwenye EITI. · Kusaidia kuunda mipaka ya EITI: Kwa uanachama kwenye makundi viongozi ya EITI, makampuni, na makundi ya vyama vya kijamii yanasaidia upatikanaji wa mipaka ya programu ya EITI. · Utoaji wa data na ulinganishaji: makampuni na vyama vya kijamii vinahusika kwenye kuteua kampuni itakayo kagua data za malipo na mapato, na kampuni itakayoweka bayana malipo kwa serikali. · Kuwasilisha matokeo ya EITI: Mwisho, makampuni na vyama vya kijamii vina nafasi muhimu kwenye uwasilishaji wa matokeo ya EITI na kuzifikisha kwa makundi mengine ya vyama vya kijamii, makampuni na umma kwa ujumla. KUSAIDIA UANZISHWAJI WA HARAKA WA MCHAKATO WA EITI NA KUONGOZA MKAKATI Uzoefu kwenye matukio kadhaa ni kuwa serikali imefikiria na kuamua kutekeleza EITI kiasi kwa sababu makampuni na vikundi vya vyama vya kijamii vimekuwa na ushawishi wa pamoja kuhusu manufaa ya kujiunga na EITI. Pamoja na kuwa uhusiano kati ya makampuni na vyama vya kijamii wakati mwingine yanakuwa magumu, uzoefu umeonyesha kuwa makundi haya yameshirikiana kwa karibu kufikia lengo moja la kuiinua EITI, bila kujali mitazamo yao tofauti. 53 Zaidi ya hapo, makampuni na vyama vya kijamii wanashirikishwa kwenye mchakato wa taifa wa EITI kwa kupitia makundi viongozi ya washikadau (angalia Sura 2: washikadau na Muundo wa Utawala) KUSAIDIA KUPANGILIA MIPAKA YA EITI, URIPOTI NA UWEKAJI WAZI WA MAMBO YA EITI Sura iliyotangulia (angalia Sura 3: Upambanuzi wa Mipaka ya Programu ya EITI) inachanganua njia ambazo mipaka ya programu binafsi ya EITI inabadilika. Maamuzi haya ya msingi yanafanyika wakati wa awali kabisa wa mchakato wa EITI yakishirikishwa washikadau wote (walio katika makundi viongozi ya washikadau) kuamua programu ipi ya EITI itekelezwe. Makampuni na vyama vya kijamii ni sehemu ya asili ya mchakato huu. Hasa kwa kuwa maswali kuhusu mipaka ya EITI yameonyesha kuwa na mijadala mingi na mchangamano kwenye utekelezaji wa EITI. Vivyo hivyo kwenye nchi zote, makampuni na makundi ya vyama vya kijamii yamekuwa yakishirikishwa , kwa makundi viongozi wa washikadau, katika kuteua na kusimamia kampuni za usimamizi na ukaguzi wa data za malipo na mapato, kwa mfano kwa kuzipitia na kusaidia kwenye uchambuzi wa zabuni zilizopokelewa kutoka kwa makampuni ya umma kama hayo. Mwisho, kwa kutegemeana na mipaka ya EITI inayotumika, kila kampuni iliyo na shughuli zake ndani ya nchi husika na inashiriki mchakato huu inatakiwa kukusanya data za malipo; kama inahusu, uthibitisho kuwa data zilizokusanywa kwenye mfumo wa kuripoti zinatokana na tamko la fedha la kampuni iliyokaguliwa katika viwango vya kimataifa; maelezo kwa msimamizi kama kuna mapungufu ambayo hayajaelezewa; na kwa nchi ambazo zina EITI zake zina kwenda mbali zaidi, maelezo ya ziada au kumbukumbu kama zitakavyohitajika. UWASILISHWAJI WA MATOKEO YA EITI Makampuni na makundi viongozi yote yana nafasi muhimu kwenye kuwasilisha matokeo ya EITI kote kwa nchi na kwa dunia nzima (angalia sura 8: Uwasilishwaji wa EITI). Makampuni na makundi ya vyama vya kijamii 54 yameishafanya shughuli kadhaa za mawasiliano: yamefadhili makongamano kuhusu EITI kwa ajili ya makampuni mengine au makundi ya vyama vya kijamii; kutoa kauli za kuunga mkono EITI kwa vyombo vya habari na tovuti zao; na kutoa hotuba kuhusu EITI kwa wasikilizaji mbali mbali. KUJENGA UWEZO Katika nchi nyingi, programu ya EITI imejumuisha kutoa nafasi ya baadae kwa ujenzi wa uwezo na mafunzo maalum ya EITI kwa makampuni madogo na vyama vya kijamii, pamoja na serikali. Baadhi ya makampuni ya ndani ya nchi, kwa mfano, yanajua kidogo sana kuhusu EITI na yanaweza yasiweke taarifa za fedha katika mtindo ambao ni rahisi kufikika; pia yanaweza yasielewe nini kinahitajika toka kwao kama sehemu ya mchakato wa EITI. Ujenzi wa uwezo kwa vyama vya kijamii vinavyojua kuhusu EITI kwa vyama vingine ambavyo havina ufahamu wa kutosha ni kitu cha kawaida kwa programu ya EITI iliyoandaliwa na kutekelezwa na kundi kiongozi la taifa la EITI. Kwenye nchi nyingi, watu wachache wanaelewa mambo ya kitaaluma kuhusu mapato na malipo yanayoshughulikiwa na EITI, na miongozo10 kwa watumiaji na washikadau inahitajika mara zote. Programu za ujenzi wa uwezo kwa vyama vya kijamii kwa kawaida zinajumuisha: · Taarifa kuhusu jinsi makampuni ya uziduaji yanavyofanya kazi siku baada ya siku, mfumo wa hazina na mtiririko wa mapato, na jukumu la serikali kisheria kusimamia mambo mbali mbali ya utendaji wa makampuni. · Taarifa kuhusu aina mbalimbali za kodi ambazo makampuni yanalipa na jinsi kodi hizo zinavyo kaguliwa na kukusanywa. · Taarifa kuhusu mfumo wa ukaguzi wa makampuni, ikijumuisha gharama za uzalishaji, mapato, aina ya mapato, na kodi na malipo ya hisa za uzalishaji kwa serikali. 10Fahamu kuwa miongozo kwa vyama vya kijamii vinavyo fanyia kazi mambo ya EITI tayari ipo na inaandaliwa duniani na makundi ya vyama vya kijamii kama Taasisi ya kuangalia mapato na umoja wa "Chapisha unacholipa". Muongozo kwa makampuni unaandal;iwa na sekretarieti ya EITI. 55 · Njia za vyama tofauti vya kijamii kukubaliana juu ya mikakati ya kujiunga na utekelezaji wa EITI ­ kwa mfano, kwa kuunda muungano wa vyama vya kijamii vya ndani ya nchi vitakavyojishughulisha na uwazi katika mambo ya mapato. 56 SURA 7: UANDAAJI WA RIPOTI YA EITI UTANGULIZI Sura hii inaangalia uzoefu unaojitokeza kwenye kukamilisha ripoti za EITI. Kama ilivyoelezwa hapo awali mchakato huu unategemea na mipaka ya programu ya EITI (angalia sura 3: Upambanuzi wa Mipaka ya Programu ya EITI). Katika sura hii yote neno "msimamizi" limetumika kuonyesha kazi za kampuni inayotoa huduma katika kiini cha mchakato wa kulinganisha data za EITI (au wakati mwingine ukaguzi) na mchakato wa kuripoti EITI. Uzoefu unaonyesha kuwa moja kati ya mivutano ya kawaida kwenye mchakato wa EITI unatokea kwenye tofauti za matarajio au kiwango cha uelewa juu ya ni nini kitakuwemo au hakitakuwemo kwenye ripoti ya EITI. Kwa sababu hiyo nchi zile zilizoweza kuwa na programu ya EITI iliyofanikiwa zimetokea kuwa ni zile zilizo fanya kazi kubwa kuhakikisha kuwa kuna makubaliano baina ya washikadau juu ya mipaka ya mchakato, na katika hali ya kundi la washikadau kuelewa vizuri kazi ya msimamizi au mkaguzi na jinsi ripoti ya EITI itakavyoonekana. KUCHAGUA MSIMAMIZI (AU MKAGUZI, KAMA HALI IKO HIVYO) Kwenye nchi zote za EITI, jukumu la kuchagua msimamizi (au mkaguzi, kama hali iko hivyo) linabaki kwa kundi kiongozi la washikadau (au kundi dogo lililo pale), pamoja na kuwa shughuli halisi ya kukusanya zabuni na kuingia mkataba, na kampuni ya kutoa huduma iko chini ya serikali, ambayo ndiyo inayolipia gharama ya kazi. Ndani ya mipaka ya EITI iliyokubalika, nchi zimefanya uchaguzi wa makampuni haya ya kutoa huduma kwa kuelezea hadidu za rejea za utoaji huduma na kutoa nakala ya zabuni inayohitaji mapendekezo toka kwa makampuni ya kutoa huduma. Kwa kawaida makampuni ya mahesabu ya umma au makampuni ya ushauri. Makundi viongozi yamekuwa yakiangalia makampuni haya yanayoweza kuonyesha:- 57 · Uelewa mzuri juu ya jinsi tasnia ya uziduaji kwenye nchi husika inavyo undwa na mtiririko wa malipo ya makampuni na mapato ya serikali yalivyo; · Uzoefu kwenye sekta ya mafuta, gesi au uchimbaji madini na ufahamu wa ndani juu ya hazina na muundo wa kodi katika sekta hii; · Ujuzi mzuri na uwezo wa kufanya kazi inayotakiwa ndani ya bajeti iliyopo; · Kutokuwepo kwa migogoro yeyote ya kimaslai (na kampuni au serikali) au uwezo wa kujilinda dhidi ya migogoro ya aina hiyo; na · Uwezo wa kujitegemea, uaminifu na utendaji unaoheshimiwa na wanachama makundi viongozi ya washikadau. HADIDU ZA REJEA KWA MSIMAMIZO (MKAGUZI) NA MAMBO YANAYOTAKIWA KUWEMO KWENYE RIPOTI YA EITI Kama ilivyo elezewa ripoti za EITI za nchi, kwa ujumla zinakubaliana na vigezo vya EITI, zinatofautiana kwenye muundo na yaliyomo; zinategemeana na mipaka ya programu ya EITI, na kwenye uchaguzi wa kiasi cha kazi ambacho kitafanyika zaidi ya makubaliano (angalia sura 3: Upambanuzi wa Mipaka ya Programu ya EITI). Katika kupanga hadidu za rejea, kwa ajili ya ukaguzi wa data muhimu na suala la ripoti za EITI, mambo ambayo yamekuwa yakielezewa na nchi kwenye hadidu za rejea yamejumuisha: Vipengele vya mkataba na kazi ya maandalizi · Gharama ya kazi ya ukaguzi: Suala muhimu la kuangaliwa ni nani (kwa mfano serikali) atachukua jukumu la kulipa gharama ya mkataba na kupata historia ya maendeleo ya malipo juu ya mkataba huo. Wakati mkataba na ratiba ya malipo vinaweza kubadilika, kwa kuzingatia masaa ya kazi, mingi ni mikataba yenye gharama zisizo badilika; ambapo bidhaa iliyotajwa, katika ubora na muda unaokubalika zitafanyiwa malipo kila baada ya hatua fulani kufikiwa (kwa mfano, wakati wa 58 kuwasilisha mfumo wa ripoti, wakati wa kuwasilisha nakala ya awali ya ripoti, wakati wa kuwasilisha nakala ya mwisho ya ripoti na kuendelea). · Usimamizi wa kazi za mkaguzi: kwenye nchi nyingi, miongozo ya siku kwa siku imekuwa ikitolewa na makundi viongozi ya washikadau (au makundi madogo yaliyopo); miongozo inajumuisha kujibu maswali ya kitaaluma ambayo msimamizi (mkaguzi) atayauliza. · Jukumu la maandalizi ya kazi: Katika baadhi ya nchi nakala ya mfumo wa utekelezaji inaandaliwa na kitengo cha utekelezaji ili kupitishwa na kundi kiongozi (ambao msimamizi ataanza kuutumia), wakati kwenye nchi zingine msimamizi, kwa kupata ushauri toka kwa washikadau na kuandaa ­ mawasilisho ya awali ­ mfumo wa kuripoti ili kupitiwa na kupitishwa na kundi kiongozi. · Mafunzo kwa watumiaji kama sehemu ya mkataba: Baadhi ya makampuni ya wasimamizi yametakiwa, kufanya kazi na makundi viongozi kama sehemu ya mkataba katika kuandaa miongozo jinsi muundo EITI au mambo mengine ya mchakato wa EITI yatakavyofanya kazi, na kutoa mafunzo vitengo vitakavyohusika na utoaji wa data kama sehemu ya mchakato wa EITI. Katika hali kama hii nchi zimeweza kuendelea kwa haraka, na EITI kwa kufikia uelewa linganifu juu ya data zinazohitajika. · Usiri wa data na uzuizi wa kumbukumbu: Kipengele kitahitajika kuwekwa kwenye mkataba juu ya data zitakazotolewa kwa mkaguzi/msimamizi kuchukuliwa kama ni za siri na kipindi cha uzuizi wa data kujulikana. Yafuatayo yana jumuisha yaliyomo katika ripoti ya EITI pamoja na hadidu za rejea za msimamizi. Mambo muhimu ya mipaka · Idadi ya makampuni shiriki (na wakala wa serikali) watakao husishwa kwenye mchakato kama ilivyotambuliwa na kiwango cha umuhimu kilichowekwa na makundi viongozi ya washikadau; katika suala la vyombo vya serikali, hii inategemea na hali ya nchi na kama serikali ndogo zinahusishwa kwenye mchakato wa EITI. 59 · Kujumuishwa kwa aina ya malipo au kiwango: vyanzo gani vya malipo vinavyo jumuishwa kwenye mchakato? Hii inategemea kama makundi viongozi yameweka viwango vya umuhimu ambavyo chini ya hapo malipo hayahitaji kutolewa taarifa kwenye EITI, na au kama kundi kiongozi limeamua kuacha baadhi ya vyanzo vya mapato kwa kuwa ni vidogo sana. · Idadi ya marudio ya utengenezaji wa ripoti za EITI: Nchi nyingi zimeamua kuandaa ripoti za EITI kila mwaka, hata hivyo baadhi zimeamua kuandaa ripoti mara mbili kwa mwaka. Kwa kuongezea, mwanzoni kabisa mwa mchakato wa EITI baadhi ya nchi zimeamua kutumia EITI kwa miaka ya mwanzoni ili kupata uhakika wa malipo na mapato ya hiyo miaka ya awali. Idadi ya marudio ya uandishi wa ripoti na miaka inayo husishwa ni suala la mipaka ya programu ya EITI ya taifa na rasilimali fedha zilizopo kulipia gharama ya huduma ya ukaguzi. Picha 7.1 inaonyesha katika mchoro uliopangwa jinsi ripoti ya EITI inavyo andaliwa na kazi za washikadau mbali mbali katika mchakato mzima. Kazi za mlinganyo na uthibitishwaji wa ukaguzi wa ziada (Zaidi ua ulinganishaji) · Asili ya kazi za ulinganishaji (au ukaguzi): kama ilivyojadiliwa hapo awali (angalia sura 3: Upambanuzi wa Mipaka ya Programu ya EITI), mipaka ya kazi inaamua kama mchakato wa EITI wa nchi husika una mlinganyo na data zilizokusanywa au unahusisha ukaguzi wa ziada. Nchi zinazotumia mchakato wa mlinganyo zina chukulia kuwa data za fedha zinaaminika. 60 PICHA 7.1 MCHAKATO WA KURIPOTI EITI · Uhakika wa ziada kwenye makusanyo ya data: baadhi ya michakato ya ukaguzi wa data, hatua ya ziada imeongezwa kuhakikisha uaminifu wa data zilizotolewa na makampuni. Katika hatua hii, ofisa wa kampuni anahakikisha "ana zitoa" data zilizokusanywa, au data zinaambatana na tamko toka kwa mkaguzi wa kampuni kuhakikisha kuwa data za EITI zilizokusanywa zimetokana na tamko la fedha lililopo na lililokaguliwa katika viwango vya kimataifa. 61 · Uthibitishwaji wa ziada: wakati wa mchakato wa ulinganishwaji, swali hili limejitokeza mara kadhaa: kuna kitu katika data zilizo ripotiwa ambacho msimamizi anaweza kuhitaji kijaribiwe kwa uhakika zaidi? Haja ya uthibitishwaji wa ziada au majaribio inatakiwa pia itambuliwe kwenye mpango wa kazi, na fedha za ziada kutengwa kwa ajili hiyo. Ripoti za EITI zilizo kaguliwa katika Viwango vya Kimataifa · Undani na upana wa mipaka ya ukaguzi: Katika hali ambazo kazi na ripoti za EITI zinafanywa kama ukaguzi kamili, mipaka ya ukaguzi ndio msingi wa maamuzi: kwa mfano ukaguzi uende zaidi ya kukagua malipo na mapato kwa kuhusisha pia ukaguzi wa hazina halisi na mchakato wa sekta? · Ufikiwaji wa kumbukumbu za kampuni na serikali: kama kwenye kaguzi zingine, kampuni ya ukaguzi inahitaji kuwa na ruhusa ya kuzifikia kumbukumbu ili iweze kuthibitisha kuwa data zimekamilika na ni sahihi. Ushughulikiwaji wa mapungufu yaliyogunduliwa na msimamizi (mkaguzi) Kiwango cha ufuatiliaji: suala muhimu lililoonekana kwenye nchi kadhaa ni wigo wa ufuatiliaji unaotegemewa toka kwa msimamizi au mkaguzi pale mapungufu yanapo jitokeza. Kuna suala la gharama/manufaa, hivyo basi nchi nyingi zinataka msimamizi (mkaguzi) kufanya juhudi zaidi kupata taarifa kutoka kwa makampuni au wakala wa serikali kuhusu mapungufu ya data zilizo ripotiwa (ambayo yanaweza kutokea kutokana na sababu kadhaa za kiufundi ­ sio lazima yatokane na utendaji mbovu). Baada ya bidii ya ufuatiliaji msimamizi (mkaguzi) atawasilisha mapungufu ­ na ufuatiliaji utaendelea baada ya ripoti ya EITI kutolewa. Uwasilishaji na uchapishaji · Ripoti inaeleweka: Shughuli ya msingi ya mchakato wa EITI ni kupata data za mahesabu, ambazo mara nyingine zinakuwa ngumu kueleweka, na kuziwasilisha data hizi katika mtindo ambao ni rahisi kueleweka. Msimamizi/ mkaguzi atahitaji kuandaa ripoti ambayo itakuwa na 62 mambo mengi katika mtindo ambao unaeleweka kirahisi. Hadidu za rejea za kazi zinaonyesha wazi nani atakuwa na jukumu la kuchapa, kuchapisha na kusambaza ripoti (katika nchi nyingi, hii ni kazi ya kundi kiongozi sio msimamizi/ mkaguzi). Mfano wa hadidu za rejea za msimamizi wa EITI wa Cameroon, zipo kwenye kiambatisho I kwenye CD-ROM. UKUMBUSHO KWENYE MUUNDO WA KURIPOTI WA EITI Mijadala kwenye vipengele vilivyotangulia vya sura hii imefanya marejeo kwenye muundo wa kuripoti wa EITI. Miundo hii ama imesanifiwa kabla msimamizi hajachaguliwa au zinasanifiwa na kampuni ya ukaguzi iliyochaguliwa na inawasilisha kwenye hadidu za rejea. Uzoefu wa EITI unaonyesha kuwa usanifu wa miundo hii una maswali kuhusu jinsi itakavyofanya kazi, makampuni na serikali katika kukusanya data zao za fedha, imeanzisha mjadala baina ya washiriki kwenye makundi viongozi ya washikadau. Suala lingine la kawaida ambalo makundi viongozi yamezungumzia kwa kuzingatia muundo wa data wa EITI ni kuwa makampuni na wakala wa serikali wakati mwingine wametafsiri tofauti miundo inayotakiwa na hawajui data ipi haswa inatakiwa kuingizwa. Mambo mengine yanayohusiana na ufafanuzi wa kiutaalamu ambayo yameleta ugumu yanajumuisha:- · Kodi au masuala ya kitaaluma ­ mambo yanayohusiana na hayo kama mpangilio na uandishi maalum wa malipo mbali mbali ya kodi. · Kukokotoa na kuripoti data katika misingi ya kuendana ­ ama kwenye fedha taslim au inayotokana na mapato ya nyuma ya uwasilishaji wa mahesabu ya fedha. · Vipimo vya kuendana vya kuripoti uwingi na ubora wa ujazo halisi wa mafuta, gesi na madini · Uendano kwenye malipo ya kijamii (yakujitolea) toka kwa makampuni ya uziduaji ambayo wakati mwingine makampuni yanachukulia kama 63 malipo hayo si ya kujitolea na yamejumuishwa kwenye miundo ya malipo ya kodi ili yaripotiwe kwenye EITI na · Tafsiri ya fedha za nje, na mengineyo Kuyaelezea mambo haya, nchi nyingi pia zinaandaa miongozo mifupi kwa makampuni yanayojaza miundo hii ya kuripoti. Nchi tofauti zina mipango tofauti ya hazina ya kutambua aina gani ya kodi na malipo gani kampuni inatakiwa kuyafanya kwa serikali. Kwa sababu hii kila nchi itajitaji kuwa na muundo wa aina yake. Kiambatisho J kwenye CD kinaonyesha mfano wa muundo uliotumika Ghana kwa uchimbaji madini na Khazakstan kwa mafuta na gesi. Mafunzo maalum ya jinsi ya kukamilisha miundo Kama ilivyoonyeshwa hapo juu, katika baadhi ya matukio msimamizi (mkaguzi) amepewa kazi ya kutoa mafunzo na kuwaelekeza watumiaji jinsi ya kujaza miundo hii kwa kuendana na usahihi. Kwa ujumla, mawasiliano mazuri na nafasi ya kutoa muongozo wakati inaonyesha matatizo haya yanapotokea. MUHTASARI WA UHUSIANO KATI YA VIWANGO VYA KIMATAIFA VYA UKAGUZI NA VIGEZO VYA EITI Vigezo vya EITI vinajumuisha: "pale ambapo kaguzi za namna hiyo hazipo, malipo na mapato ni suala la mkaguzi wa kujitegemea anayetumia viwango vya kimataifa. "Kuna marejeo kwenye vigezo kuhusu: "malipo na mapato yana linganishwa na msimamizi mwenye uwezo anatumia viwango vya ukaguzi vya kimataifa". Viwango hivyo ni vile ambavyo vimekubalika kitaaluma na kimaadili kwa huduma za ukaguzi na uhakiki ambazo wahasibu wa umma na wakaguzi wanazitumia katika karibu kila nchi, ama kwa kukubaliana na sheria za ndani au kwa kukubaliana na uaminifu wao katika taaluma zao katika Mabaraza yao ya Taifa ya Uhasibu na Ukaguzi. Mabaraza haya ya taifa ni wanachama wa 64 Shirikisho la wahasibu la Kimataifa (IFAC, lenye makao yake New York, USA), ambayo inatoa viwango vya kimataifa vya ukaguzi (kwa kupitia viwango vya kimataifa vya ukaguzi na uhakikishaji, IAASB) kwa kuombwa na wanachama wote wa IFAC. Suala la viwango vya ukaguzi vya kimataifa limejadiliwa kwenye sura hii kwa uhusiano na vigezo viwili vya EITI: msimamizi au mkaguzi atahitaji kutumia viwango hivi vilivyokubalika wakati wa kuandaa ripoti za EITI, na kuwa malipo na mapato yaliyojumuishwa kwenye ripoti za EITI yenyewe yanahitaji kuwa sababu ya ukaguzi kukamilika kwa viwango vya kimataifa vya ukaguzi. Kama ilivyo bainishwa kwenye nchi nyingi za EITI, kigezo hiki kinafikiwa kwa ushirikiano na mazingira yaliyopo, pamoja na kuwa katika baadhi ya nchi uhamaji toka katika utaratibu wa taifa au viwango vya ukaguzi vya serikali au makampuni bado ni mchakato mrefu. 65 SURA 8: USAMBAZWAJI WA EITI UTANGULIZI Mbinu na vifaa vya kufikisha taarifa kuhusu EITI vimepata muitikio mzuri na makundi viongozi ya washikadau katika nchi nyingi. Hii ni kwa sababu mchakato wa EITI unaangalia zaidi sio tu kwenye uzalishaji wa data za malipo na mapato na kwenye mchakato wa washikadau, lakini pia kwenye kuhakikisha uwajibikaji kwa kuhakikishia wananchi wanajua, wanaelewa na wana nafasi kwenye programu nzima ya EITI na taarifa zinaandaliwa. Katika nchi zote zinazo tekeleza EITI, makablasha muhimu yanayohusiana na programu (kwa mfano, hadidu za rejea za kundi la washikadau, waraka wa maelewano , mpango wa kazi, na kuendelea) zinawekwa wazi kwa umma. Kanuni ya miongozo kwenye mawasilino ya programu ya EITI ni kuwa ripoti zinatakiwa kuwasilishwa katika mtindo ambao uko wazi na unaeleweka (na bila kuurahisisha kupita kiasi), na kwa msaada wa michoro na majedwali, ambayo yatapelekea urahisi wa kuelewa na ufupisho wa yaliyomo kwenye ripoti. MIKAKATI YA KAWAIDA YA MAWASILIANO NA VIFAA Nchi nyingi zinazo tekeleza EITI zimeandaa mikakati ya mawasiliano ambayo inagusia, njia za, (i) kugundua ni wadau gani wataathiriwa na, au wana shauku ya kujua kuhusu EITI; (ii)kuielezea EITI kwa wadau hao na kuamua kwa kutegemea na kila mdau ni jinsi gani watashirikishwa; (iii) kuwasilisha mjadala na maamuzi ambayo yanafanyika kuhusu mipaka ya programu ya EITI itakayo tekelezwa; (iv) kuwasilisha matokeo ya programu ya EITI; na (v) kupitia mchakato wa EITI mara kwa mara. 66 SANDUKU 8.1 ZANA MUHIMU ZA MAWASILINO KWA EITI 1. ZOEZI LA KUTAMBUA WASHIKADAU: Usahihi wa kutambua washikadau gani wanashauku ya kujua, au wataathiriwa na utekelezaji wa EITI; inatumika kuwataarifu washikadau kuhusu EITI na kutambua wanachama muhimu wa makundi viongozi ya EITI. 2. UCHUNGUZI NA UCHAGUZI: Inaweza tumika kugundua kiwango cha uelewa cha umma juu ya jinsi makampuni ya uziduaji yanavyoendesha shughuli zake na jinsi malipo yanavyotolewa na makampuni kwenda kwa serikali na jamii. Uchunguzi kama huu unaweza pia kugundua mambo mahimu ambayo washikadau watapenda kuona yakizungumziwa kwenye mchakato wa EITI, kusaidia kutengeneza mipaka ya programu ya EITI. Inaweza pia kutumika wakati wa programu ya EITI kama njia ya kuangalia madhara ya mkakati kwa umma ­ kwa mfano, kwa kuangalia idadi ya kura zilizopigwa wakati mchakato unaanza na baada ya kutolewa kwa ripoti ya kwanza kupima mabadiliko ya kiwango cha umakini juu ya tasnia ya uziduaji au mambo ya EITI na pia ya mitazamo ya uma. 3. MUITIKIO WA MAWASILIANO: unaweza tumika kuleta pamoja matokeo ya chunguzi na zoezi la kutambua washikadau ili kugundua mchanganyiko wa vyombo vya habari ambavyo vitarahisisha kufikiwa kwa washikadau tofauti. 4. WARSHA, MAKONGAMANO NA MAONESHO YA BARABARANI: Nchi nyingi za EITI zimefanya matukio mengi makubwa ya kijamii ambapo wadau wote na umma kwa ujumla wanaalikwa kupata maelezo kuhusu EITI, kujadili jinsi itakavyofanya kazi na kuamua jinsi mkakati utakavyo tekelezwa. Katika nchi nyingi matukio haya yamefanyika katika sehemu mbali mbali - kwa mfano, kwenye miji mikuu pamoja na kwenye miji muhimu ya kibiashara na kwenye maeneo yanayoathiriwa moja kwa moja na shughuli za uchimbaji mafuta, gesi au madini. 5. VITUO VYA TAARIFA KWA UMMA: Baadhi ya nchi zimeanzisha vituo vya taarifa kwa umma ambapo raia yeyote anaweza kwenda kupata taarifa kuhusu mkakati, nakala za ripoti, na taarifa kuhusu tasnia ya uziduaji. 6. HABARI NA MATANGAZO: Nchi zote za EITI zimefanya mikutano na waandishi wa habari, kufanya usahili na mashirika ya habari au kutangaza kwenye vyombo vya habari vya ndani, kwa kuzingatia ufikiwaji wa vyombo hivyo na idadi kubwa ya watu katika ngazi ya ndani ya nchi. 7. KUJENGA UWEZO KWA WAANDISHI WA HABARI: Baadhi ya nchi zimekuwa na vipindi vya mafunzo kwa waandishi wa habari kutoa taarifa zaidi jinsi mchakato wa EITI unavyofanya kazi, nani anahusika, na maelezo ya ripoti pale ambapo zimekwisha tolewa. 8. UANZISHWAJI WA TOVUTI YA EITI: Namba kubwa ya tovuti za taifa za EITI zimeanzishwa na serikali ili kutumika kama chanzo cha taarifa juu ya mkakati na kutoa taarifa za mambo yanayoendelea, kama kumbukumbu za vikao, taarifa na ripoti za EITI zilizokamilika. 9. MIJADALA YA UMMA: Baadhi ya nchi zimefanya mijadala ya umma na watu au makundi tofauti wakiwasilisha mawazo mbali mbali juu ya jinsi ya kuutekeleza mkakati. 67 Ukosefu wa mkakati wa mawasiliano ulioelezewa unapelekea hatari ya wadau muhimu kutokujua kuhusu au kuhusishwa kwenye mchakato wa EITI. Nchi zimegundua, hivyo basi ni muhimu kuhakikisha kuwa mkakati wa mawasiliano unawafikia watu wengi kadri inavyowezekana, kutambua kuwa kila mwanachama ni mpokeaji muhimu wa mapato kupitia matumizi ya serikali, na inasaidia kuleta uwajibikaji kwa serikali na makampuni kwa kuhakikisha kwamba umma unahusishwa na mchakato wa EITI. Nchi zinazo tekeleza EITI zimetumia ­ na zinaweza tumia ­ vifaa mbali mbali vya kuwasilisha EITI kwa taifa na zaidi, kama ilivyoonyeshwa kwenye sanduku 8.1. 68 SURA 9: MATOKEO: TATHMINI NA USIMAMIZI WA PROGRAMU ZA EITI UTANGULIZI Tathmini na usimamizi wa matokeo na madhara ya programu ya EITI ni njia muhimu ya kuhakikisha kuwa programu ya EITI inayotumika inaendelea kuwepo na inaanza kuleta mambo yanayotegemewa. Nchi ambazo hazijapitia programu zao za EITI zimapata wakati mgumu kugundua udhaifu kwenye programu hizo. Katika baadhi ya matukio hili limedhoofisha uungaji mkono wa mchakato wa EITI toka kwa washikadau. KUSIMAMIA NA KUTATHMINI UTENDAJI UNAOANZA Nchi nyingi zinazo tekeleza EITI zime fanya tathmini ya programu zao za EITI katika hatua mbali mbali, na zimekuwa zikiboresha mipaka na mpango wa kazi kutokana na tathmini hizo, hasa zile zilizofikia hatua ya kutoa ripoti za EITI. Sehemu ya kuanzia kwa tathmini hizo ni kwenye mchakato wa usimamizi na tathmini ­ mpango wa kazi unakubaliwa na washikadau, ambao unatoa msingi kwa kuzingatia nini kilitakiwa kukamilishwa. Mipango ya kazi inarekebishwa vile inavyotakikana na mchakato wa usimamizi na tathmini, na hatua za kazi kuboreshwa na kupangwa kama zinavyotakikana. Mapitio haya ya usimamizi na utathmini kwa kawaida imekuwa ikifanywa na ama sekretarieti ya taifa ya EITI au na mshauri wa kujitegemea aliyeajiriwa kwa ajili hiyo. Mapitio ya simamizi na tathmini yanaongozwa na kundi kiongozi la washikadau na inaweza kuchangiwa na kura na chaguzi za umma kama zinavyotakikana. Makundi ya washikadau na sekretarieti wanaweza wao wenyewe kujipa mamlaka ya kupitia shughuli zao wenyewe kama sehemu ya programu ya usimamizi na utathmini. Ikumbukwe kuwa kwa matokea bora zaidi, nchi zinaweza tumia vigezo vya EITI na viashiria uthibitishwaji wa EITI (kiambatisho B) katika mapitio haya. Mfumo wa kipimo cha matokeo Pamoja na kuwa uzoefu wa nchi kwa EITI bado ni mdogo, matokeo ya jumla ya EITI yalianza kujadiliwa katika nchi za EITI. MDTF inayo simamiwa na benki 69 ya dunia imeandaa mfumo wa matokeo ambao unaanza kutumika kwenye nchi fulani. Mfumo huu una dhumuni la kusaidia nchi za EITI kupima matokeo ya programu za EITI katika kipindi fulani, kwa kutumia viashiria ufanisi vilivyokubalika. Utaratibu kama huu ulitakiwa uiwezeshe picha ya matokeo ya EITI kuweza kuhifadhiwa. Kiambatisho C ni sampuli kielelezo ya kuwakilisha matokeo ya mfumo wa vipimo vya matokeo 70 SURA 10: MUUNDO WA KIMATAIFA WA EITI UTANGULIZI Wakati mjadala katika ripoti hii umekuwa kuhusu EITI katika ngazi ya taifa, vile vile kazi muhimu ya EITI inafanywa na waasisi wa EITI kimataifa kuisimamia EITI katika ngazi ya dunia; kuunga mkono nchi tekelezi; kuandaa sera na malengo ya EITI duniani; kutoa ushauri na vitendea kazi kwa mashirika na watu binafsi wanaojihusisha na utekelezaji wa EITI; na kuwaleta washikadau pamoja mara kwa mara kubadilishana mawazo juu ya uzoefu na kukubaliana juu ya sera. Muasisi wa EITI katika ngazi ya dunia pia ana jukumu la kuongoza mchakato wa uthibitishaji pamoja na vigezo vya EITI na miongozo ya utathmini, kama ilivyo jadiliwa hapa chini. Katika kuamua kutekeleza programu ya EITI, nchi hazitekelezi mchakato katika ngazi ya taifa tu, lakini pia kuwa sehemu ya utawala bora wa serikali chini ya mamlaka ya EITI. MUUNDO WA UTAWALA WA EITI KIMATAIFA Picha 10.1 inaonyesha muundo wa kimataifa wa utawala wa EITI. Hoja ya msingi ya mafundisho haya ni kuwa ni mchakato wa washikadau ndio unaojumuisha uhusishwaji wa serikali, makampuni ya uziduaji, vikundi vya vyama vya kijamii, serikali zinazounga mkono, wawekezaji na mashirika ya fedha ya kimataifa. Taasisi muhimu kwenye muundo huu wa utawala wa dunia ni kama ifuatavyo: · Bodi ya EITI: Bodi ya EITI ni chombo muhimu cha maamuzi kwa mkakati na kinasimamiwa na mwenyekiti aliyechaguliwa. Uanachama wa Bodi ya EITI unapatikana katika makongamano ya EITI. Bodi pia inafanya kazi na kamati ndogo ndogo nyingi ikigusia mambo kama ya uchimbaji madini. Kazi za msingi za bodi ni: (i) kuelezea mambo yote muhimu kwenye sera (ii) kufanya maamuzi juu ya sera inayoamua jinsi gani kazi za EITI zitafanyika kimataifa kwa kushauriana na washikadau; (iii) kuweka viwango vya chini kwa serikali na makampuni yanayo tekeleza mkakati (iv) kuongoza kazi ya sekretarieti ya EITI ya kimataifa 71 (v) kuhakikisha kuwa rasilimali za kutosha za kuunga mkono mkakati katika ngazi ya dunia; (vi) kuunga mkono kazi ya sekretarieti; na (vii)kuongoza mchakato wa utathmini, ambao umeelezewa kwenye kiambatisho B. PICHA 10.1 MUUNDO WA UTAWALA WAKIMATAIFA WA EITI · Sekretarieti ya EITI ya Kimataifa: Sekretarieti ina makazi yake, Oslo ndio sehemu ya kwanza ya mawasiliano kwa nchi zote zinazohusika na zinazotaka kujihusisha na EITI.Kazi kuu za sekretarieti ni kuunga mkono kazi za bodi kwa kuandaa sera na miongozo kwa mambo ambayo bodi inayafikiria na kuyafanyia utafiti; kusimamia mawasiliano yote ya kimataifa ya EITI, na kuwa sehemu ya kwanza ya mawasilino kwa washikadau wote wa EITI; kushughulikia suala la kuongeza namba ya nchi, makampuni na washikadau katika mchakato mzima wa EITI; kuandaa makongamano ya EITI; na kushirikiana na wahisani na mawakala, kama benki ya dunia, wanaotoa misaada ya kiufundi na kuunga mkono utekelezaji kwa nchi, na kushirikisha wahisani Benki ya 72 Dunia na kamati ya usimamizi ya wahisani wa EIT ili kuhakikisha misaada ya kutosha inapatikana kwa nchi zinazotekeleza mkakati. · Makongamano ya EITI: Kongamano ndio mkutano mkuu wa washikadau wote wanaojihusisha na mchakato huu duniani. Kazi kubwa za kongamano zimejumuisha mijadala na kupitisha sera muhimu zilizoandaliwa na bodi ya EITI; kuchagua wanachama na mwenyekiti wa bodi ya EITI; na kutumika kama sehemu ambapo washikadau kutoka nchi mbali mbali za EITI wanabadilishana mawazo na kuujenga mkakati. KAZI YA MASHIRIKA YA MAENDELEO YA KIMATAIFA KWENYE BODI YA EITI Mashirika ya maendeleo ya kimataifa, shirika la Fedha Duniani (IMF), Benki ya Maendeleo Afrika (AFDB), na Kundi la Benki ya Dunia (WBG) wanahudhuria vikao vya bodi ya EITI kama watazamaji na wanashiriki kwenye makongamano ya EITI. Kwa kuongezea pamoja na wakala wengine wahisani wanaotoa misaada ya kiufundi ndani ya nchi kwa nchi za EITI, Benki ya Dunia inaratibu kwa karibu sekretarieti ya EITI katika kutoa misaada ya kiufundi na fedha. Kama ilivyoelezwa, ufadhili wa kuendelea unatoka kwenye mfuko wa hisani unaosimamiwa na Benki ya Dunia na kuongozwa na Kamati ya usimamizi ya wahisani na Benki ya Dunia; Kamati inakutana mara mbili kwa mwaka kupitia maendeleo na mpango wa kazi wa mfuko huo wa hisani. Kama chombo kinachotofautisha wahisani na Benki ya Dunia, mfuko wa hisani sio sehemu ya bodi au sekretarieti ya EITI, lakini ina ratibu shughuli zake kuunga mkono malengo ya EITI na malengo ya ziada ya pamoja na waraka wa maelewano iko katika mchakato kati ya Benki ya Dunia na Sekretarieti ya EITI na Bodi ili kuweka muongozo wa uhusiano. Mfuko wa hisani ndio chanzo kikubwa lakini sio pekee kwa misaada ya ufundi na fedha kwa nchi zinazo tekeleza EITI. Wahisani wengine wengi (Kama DFID, GTZ na Serikali ya Norway) zinatoa ufadhili na kuunga mkono nchi zinazotekeleza EITI, na makundi ya vyama vya kijamii vya kimataifa kama taasisi ya kuangalia mapato inatoa misaada ya kiufundi na fedha kwa vyama vya kijamii vinavyojihusisha na mchakato huu. 73 SURA 11: USHAHIDI UNAOIBUKA JUU YA MADHARA YA PROGRAMU YA TAIFA YA EITI MATOKEO YANAYOIBUKA JUU YA PROGRAMU YA EITI Kwa kuwa programu za taifa za EITI zimeanza mnamo mwaka 2003, katika sehemu nyingi bado ni mapema kujua kiwango cha madhara yake. Nchi nyingi zimejiunga na mkakati mwaka, 2005, na nchi nyingi zilizoandaa ripoti za EITI zinafanya hivyo hivi karibuni. Jitihada za kutosha kupima matokeo na kusimamia na kutathmini mipangilio ya EITI 9 angalia sura 9: Matokeo: Usimamizi na utathmini wa Programu ya EITI) itapelekea kwenye uchunguzi wa hali ya juu kwenye madhara ya muda mrefu ya programu ya EITI, lakini kwa hivi sasa kuna habari juu ya ushahidi wa matokeo ya EITI kuanza kuonekana: · Msimamo wa serikali na makampuni unaoonekana: Kasi ya EITI inayoongezeka duniani na ndani ya nchi ni kielelezo cha msimamo katika uwazi kwenye malipo na mapato ya mafuta, gesi na madini,pia inajumuisha kutambuliwa kwa EITI kama kiwango cha kimataifa. · Ugunduzi muhimu wa mapungufu katika mfumo wa ukusanyaji mapato: Mchakato wa kuandaa ripoti za EITI kwa mtindo wa mzunguko , katika baadhi ya nchi umeonyesha mapungufu kwenye upitiaji na ukusanyaji wa mapato. Baadhi ya programu za EITI zimegundua utegemezi wa kupindukia wa kampuni kujitathmini yenyewe kwenye mambo ya kodi na au ukosefu wa uwezo kwenye wakala wa mapato kusimamia malipo ya kampuni. Katika hali hii baadhi ya programu za EITI, ama zimegundua moja kwa moja malipo ambayo yalitakiwa kulipwa lakini hayalipwi au imepelekea kuongeza mapato ya serikali. · Makusanyo na maelezo ya vyanzo tofauti vya taarifa za fedha: Katika nchi nyingi, matatizo katika utekelezaji wa EITI hayajasababishwa na uhaba wa taarifa za malipo na mapato; lakini, tatizo ni kuwa taarifa hizo zimetawanyika kwenye sehemu tofauti na hazijawekwa katika mtindo ambao unaeleweka na wananchi. Programu za EITI zimetoa mfumo kifanisi wa kukusanya taarifa katika sehemu moja, kuhakiki ukweli wake na kuelezea bayana zina maana gani. · Mchakato wa Ushirikiano: Mchakato wa washikadau umekuwa ukitumia muda mwingi lakini umepelekea kwenye sio tu kwenye kupunguza hofu 74 na hatari lakini pia katika nchi nyingi za EITI umetengeneza muundo ambao serikali, makampuni na vyama vya kijamii yameweza kufanya kazi pamoja kufikia malengo. Hii imetengeneza uaminifu baina ya pande hizi. Katika matukio mengi washikadau wameonyesha kukubaliana na jinsi wadau wengine wanavyoendesha shughuli zao. Hii imepelekea kwenye mawasiliano ya hali ya juu baina ya makampuni na makundi ya vyama vya kijamii, na kati ya vyama vya kijamii na serikali. Na pia imetengeneza kwa serikali na makampuni kuondokana na nafasi zao za "wasimamizi" na "wasimamiwa" wakati wanatimiza mchakato wa manufaa kwa wote. · Haja ya marekebisho mapana ya utawala: Kwa kuzingatia kwenye sekta moja na biashara moja muhimu, Programu ya EITI imeleta haja ya uwazi wa hali ya juu, na uwajibikaji kwa sekta zingine, makubaliano mengine ya kibiashara na sehemu zingine za utawala. Wakati EITI sio chombo pekee na kamilifu kufikia mahitaji mengine yote ya ziada inayo yatengeneza, mara zote ni hatua ya kwanza ya kusaidia kuweka utamaduni wa uwazi na uwajibikaji katika rasilimali za kuziduliwa kwenye nchi tajiri kwa rasilimali. 75 SURA 12: HITIMISHO: VIGEZO MUHIMU KWENYE PROGRAMU YA EITI ILIYOFANIKIWA MAMBO MUHIMU KATIKA RIPOTI HII Katika ripoti hii, tumeelezea uzoefu wa nchi zilizo tekeleza EITI. Kwa kuzingatia misingi ya upeo huu, inawezakana kutambua baadhi ya maudhui ambayo kundi la Benki ya Dunia linaamini nchi zitaona inawafaa, kama nchi inatekeleza EITI, inapitia uzoefu wake juu ya EITI au inafikiria kutekeleza EITI. Mafunzo haya na maudhui yanajumuisha: · Masuala ya Uongozi: Nchi ambazo zimeweza kutekeleza EITI kwa mafanikio makubwa zimefanikiwa kwa kuwa, pamoja na mambo mengine wamekuwa na muendelezo, kujitoa na kiwango cha juu cha uongozi. Hii imemaanisha kuwa mkakati umeongozwa katika hatua za juu za uongozi, huenda na waziri wa wizara mwenye nguvu ya kuhakikisha kuwa wakala wote wa serikali wanaoathiriwa na EITI wanatimiza majukumu yao. Kiongozi huyu anakuwa kwenye nafasi ambayo anaweza kusuluhisha migogoro na kutafuta rasilimali zinazohitajika kutekeleza mkakati. · Vyama vya kijamii vinaweza kushiriki na kushirikisha, sio tu kuangalia: wakati katika baadhi ya nchi zimehitaji kuingia kwenye mchakato wa EITI wa kushirikiana, ule ambao utahusisha vyama vya kijamii katika njia nyingi, makundi vyama vya kijamii yatachangia kwa kiasi kikubwa (pamoja na kuwa baadhi watahitaji muda kutoka kwenye nafasi ya kuchangia kuhamia kwenye kushiriki kikamilifu katika mkakati). Pale ambapo vyama vya kijamii vimeshirikishwa kikamilifu, nchi zimefanikiwa kuwasilisha programu makini za EITI zinazonufaisha washiriki wote. · Uwezo wa serikali inabidi utumike: Baadhi ya serikali zimezindua programu zao za EITI na kuanzisha makundi viongozi ya wadau kwa kuzingatia muda; mapema wakati wa mchakato walihitaji kutenga rasilimali watu na fedha za kutosha kwenye kazi ya kusimamia utekelezaji. · Ufanisi katika utoaji maamuzi wa washikadau ni muhimu mapema katika mchakato: Baadhi ya maamuzi muhimu yahusuyo mipaka ya programu ya EITI yanafanyika mapema katika mchakato. Watekelezaji wa EITI 76 waliofanikiwa ni zile nchi ambazo washika dau wameweza kujifunza kwa haraka, sio tu kuhusu EITI, lakini pia kuhusu mipaka ya programu ya EITI ambayo ni bora kwa nchi yao. · Kubadilishana maarifa ni muhimu, hasa katika kanda: Nchi nyingi zinazoanza mchakato wa EITI zimegundua ni vyema kujifunza kutoka kwa nchi zilizo tangulia kwenye mkakati huu, ambazo ziko kwenye ukanda wao; makundi ya serikali za kanda yasiyo rasmi na yale ya vyama vya kijamii yanaanza kutokea. · Kuanza ni muhimu ­ EITI ni mchakato wa kuingiliana: Uzoefu unaonyesha kuwa kuanza programu ya EITI ambayo ina mapungufu kwenye mipaka ni bora kuliko kutokuwa an EITI kabisa. Kufanya hata programu ya EITI ambayo ni finyu imepelekea uelewa wa pande zote na umesababisha kuanza kwa kazi na uhitaji wa kutekeleza programu ya EITI iliyo pana zaidi. · Nchi zinazo chapisha zaidi taarifa zilizo katika ubora wa juu zinanufaika zaidi na programu zao za EITI: Kiasi na ubora wa taarifa zinazo tolewa na nchi zinazo tekeleza EITI zinabadilika. Utofauti zaidi unaonekana kuhusu aina ya ukaguzi unao chukuliwa; kiwango cha mtawanyiko au mkusanyiko wa data; na kama serikali katika hatua za chini inashiriki katika mchakato. Uzoefu unaonyesha kuwa, programu zilizofanikiwa zaidi zinaruhusu kiasi kikubwa cha taarifa kuwa mikononi mwa umma. Hii inasaidia kutengeneza mazingira ya uaminifu baina ya makundi ya washikadau. Programu ya EITI iliyo pana zaidi inahitaji rasilimali nyingi zaidi, lakini gharama za ziada zitasaidia kutengeneza manufaa ya kueleweka. · Sheria inaweza kusaidia kuweka uhakika zaidi: Kumekuwa na mjadala kuhusu uhiari wa EITI. Mpaka hivi sasa ni juu ya nchi kuamua kama watekeleze EITI, EITI ni hiari. Lakini mara baada ya kuanza kutekeleza EITI, vigezo vya EITI vinataka ushirika wa makampuni na serikali kwa kuweka bayana mapato na malipo yao. Katika mtazamo huu EITI inaonekana kama "ina ulazima wa kitaifa" ambayo itaiwezesha nchi iweze kuthaminishwa kama , "Ina kibali cha EITI". Hivyo nchi zingine zimeona EITI inafanya kazi vizuri kama ikipewa nguvu ya kisheria, pamoja na mambo mengine, inatengeneza uhakika na wigo unaoelezeka vizuri kwa wote wanaohusika na mkakati wa utekelezaji. 77 · Programu pana ya mawasiliano ni muhimu: EITI ina mambo ya ufundi na inahusisha kwa mapana ya wadau mbali mbali. Kutokana na sababu hizi, nchi zile zilizoweza kuwa na programu za EITI zilizofanikiwa sana ni zile ambazo zimetengeneza programu za mawasiliano kuwataarifu, kushauriana, na kuhusisha washikadau ili EITI isiwe tu ni mchakato wa kuboresha mahesabu mbali na kuuongeza uwajibikaji kwa wananchi. · Mapitio ya mara kwa mara ya maendeleo yanasaidia: Jinsi mchakato wa utekelezaji unavyo endelea, nchi zimeona ni bora zikiwa zinafanya mara kwa mara mapitio ya ndani ya programu zao za EITI kwa mfano, kila baada ya uzalishaji wa ripoti ya EITI. Mapitio haya yanahimiza uboreshwaji na urekebishwaji wa programu · EITI kama hatua ya kwanza (au sehemu ya) programu ya marekebisho: EITI imefanikiwa kwenye nchi nyingi kutokana na kuzingatia uwazi. Kuzingatia uwazi ni kitu ambacho nchi zinaweza kujenga kwa kuhimiza marekebisho yenye mapana kwenye utawala wa sekta za mafuta, gesi na uchimbaji madini. EITI inaweza isiwe sahihi mara zote kwenye kuelezea mambo hayo, lakini, kanuni ya msingi ya uwazi na uwajibikaji inayozibeba programu zote za EITI itakuwa na matokeo bora kama zikifanywa kuwa sehemu ya shughuli za kila siku za serikali na usimamizi wa sekta. 78 KIAMBATISHO A: HAIDROKABONI ­ NA NCHI11 TAJIRI ZA MADINI 11Chanzo: Shirika la Fedha la Dunia (2007), Muongozo wa Uwazi wa Rasilimali na Mapato, http://www.imf.org/external/np/pp/2007/eng/051507g..pdf. 79 80 A OYilIIS WILUDN AY INAINUD 54 - 77 05 19 - 07 - - - - 55 94 77 68 88 IA 2. 0. 0. 0. 0. 1. 1. 1. 0. 5 14. GE GU 2004)( IMILSA OPO IYILI YOLI A YA TAUFA WILUDN AY IANNUD 99 76 59 - 09 - 12 15 42 15 18 36 12 5 IA 8. 5 OPO 0. 0. 0. 0. 0. 0. 0. 0. 0. 0. 1.1 63 32 9. 3. M GU 2004)( IMILSA IYIL OT A 4 W PA 2 6 7 8 1 5 9 8 U 45 - 2 19 - 4 36 - IF IBRAHU 2004ITAHSIN AY 35. 54. 35. 10. 7. 54. 25. 9. 39. 46. IA AFIAT IMLISA AL UUK YA AY 2 IA 8 1 1 7 6 3 4 7 8 3 9 3 2 4 1 1 1,50­ TOAPA A 36. 66. 36. 53. 58. 8. 4. 68. 11. 95. 46. 7. 24. 69. 24. 45. M 2000, WAIN 97 NIOBA TAS WKINOBAKORDI IML P 2005- ASI GD EJN 2000 AY AKA IA AY 6 2 3 4 1 7 7 3 9 1 7 8 2 6 2 W WA HA M IMLISA AL M RAAHSA 97. 90. 87. 74. 90. 44. 26. 88. 46. 92. 81. 22. 82. 52. 92. JU BI 0002 PDG ROKD A AY 3 8 3 2 5 8 2 6 7 1 5 7 5 3 1 AK IA 26. 32. 8. 23. 40. 4. 3 6. 5. 6. YA W 22. 26. 19. 14. 69. 46. HAI M TOAPA A WK IMLISA KWAIR M WAIN TAJI TAS CHIN WA NIOBAKORDIAH AY IA AY AY 5. 2. 7. 3. 7. 7. 6. 2. 5. 3. 5. 2. 1. 7. 10 26 2005- IMILSA AL M JU ANIZAH 70 77 32 71 87 27 69 88 60 30 65 79 25 74 1 A. JEDWALI *aireglA alognA *najiabrezA niarhaB malassuraDienurB *noore *aib maC moloC focilbupeR,ognoC **rodaucE *aeniuGlairotauqE *nobaG *aisenodnI *narI qarI *natshkazaK tia wuK 81 A OYilIIS WILUDN AY INAINUD 83 23 92 33 59 4 7 82 - 17 3 62 39 04 39 13 27 25 IA 0. 0. 2. 1. 0. 14. 26. 3. 0. 0. 1. 3. 1. 2. 0. 0. 3. 5 GE GU 2004)( IMILSA OPO IYILI YOLI A YA TAUFA WILUDN AY IANNUD 28 24 3 81 47 27 07 13 IA 5 OPO 3. 1. 0. 0. 1. 6. 2.2 54 26 07 05 19 05 68 26 24 93 0. 0. 0. 0. 8. 0. 6. 0. 0. 2. M GU 2004)( IMILSA IYIL OT A 4 W PA 7 U 4 1 9 8 7 1 1 6 2 2 3 7 - - 5 2 4 IF IBRAHU 2004ITAHSIN AY 60. 7. 49. 10. 58. 29. 50. 15. 38. 46. 29. 59. 34. 9. 44. 34. IA AFIAT IMLISA AL UUK YA AY IA 8 8 TOAPA A 3 IML 50. 45. 02 3 8 9 8 9 6 4 7 6 8 - 45. 46. 17. 39. 12. 24. 28. 28. 32. 25. 11 7 1 32. 35. M WAIN TAS WKINOBAKORDI P 2005- ASI GD 2000 AY EJN AKA IA AY 1 2 2 4 9 5 8 6 2 9 5 4 5 3 1 8 54 - W WA HA M IMLISA AL M RAAHSA 92. 17. 97. 60. 80. 78. 88. 80. 70. 59. 83. 42. 82. 21. 88. 70. JU BI 0002 PDG A AY 6 5 3 AK IA 44. 7. 32. 31 6 38. 62 8 3 3 8 3 7 7 8 4 9 7 7. 8. 9. 8. 7. YA W 31. 12. 19. 15. 24. 20. M TOAPA A WK IMLISA M WAIN TAS WA NIOBAKORDIAH AY IA AY AY 2. 3. 9. 4. 4. 1. 8. 3. 4. 2. 1. 8. 2. 5. 1. 80 33 78 24 83 68 21 -- 2005- IMILSA AL M JU ANIZAH 83 49 46 36 43 66 48 31 71 55 s ogaboT etair mE dna na aybiL *ocixe M airegiN ya stik wroN na mO rataQ *aissuR aibarAiduaS naduS airyS dadinirT natsine barA mkruT deitnU bezU aleuzeneV manteiV ne egar meY veA iili 05 ay 82 mb 20­ nje nishati A dh OYilIIS WILUDN AY 420. - - - - MI bi hal 5 IA ya GE GU 2004)( IMILSA INAINUDOPOIYILIN taoyN :o 00 za a 20 aa ch a F. isi Dunia. chid yai an vifuatavy o zo kipin gona nk Be hwas gevi mauz wa katika an iwk YOLI vya na A chapi ayo YA TAUFAM WILUDN AY IANUD - - - - ku ingis 25 wa 5 IA m GU 2004)( IMILSA OPOIYIL 080. oeledn m na a mae kw ilimiasa itokan azi u faida zilizo OT ndaliwaa madini ay angala imali A viashiria 4 ime za WUIFIBRAHU 2004ITAHSIN PAAY IA IMILSA AFIATAL F; ya 4 1 jumla rasil - - - MI C) a 15. 79. wa mluj au la (ROS IN rasilimali ya nchi zao UUK siri na ya na AY AY BOAK za e boni mapato nj OTAPAM IA 9. wafanyakazi ma ua sawa A 5 dini - - ni P 42 26 ya ala o nii ma WAINATS KWINOB 2005- IMLISA GD RODIAHEYNE an o makisi haidrokaeyne namad uzauk shati ni o na kw na wa WA KAORIDAH 2000AKAWM AY EJN IA IML AYALM ASI JU RAAHSABI WKAK 8 u 23 - - 1 viwang o asilia. 80. 72. WEO wa tajiri kanayo TO za ni yat anayk sieg UFEL lizia a ito Upunguf na 2000AKA PDGAY toa kuw ad M taarifa waang map fai ghafi, IA DAU 4 8 za nia.uD 65. 83. uliwa au au .6002 5002­ - bu ya ni 04 YA TOAPAM WAIN TAS WA WMAWKINOBAKORDIAH IMLISA MAYAN 73. 38. kwa na/ na/ mafuta, Ju 20 dhafe hwa.si ni ni zinazochuk boa nkieB wea aka m 5 kumbukum ya chap kaboor eza,re rokd vya mw ya Uing a 0502 AY zotei 200­ kw IA AY 9 - 7 8 nzi, hai ge ripoti haija haid kaa az a aka 20. 31 57. 63. [*] C nch za za 25. oeledn ma ta mw 4002 a a ilihda a kani a a ROS hisa hisa uf mae Mafu kw kw 2005- IMLISA AYALM JU NAIZAH TIAKAYAN UUJAYOTAPA wakuru a uish a uish pata a a * ya nyota wuk wa wa asilimi za e ajum u zin ny muishu ajumn kani kani bodi viashiria I ze s ha lin kij dhaef pata pata za nye A.1 Wastani au Wastani angala ya a.k MEYNEZ ak ya nchi o i. ozel wimukaT:o za zin zin aif aif aif Kwa [**]inao dwalieJ ii. pat Ma Mae iliyotumi anzhC Taar Taar Taar HICN aivloB 8d Cha ianaitruaM peicnirPdnaemoTo Sa etseL-romiT Nyara:o 1. 2. 3. 4. 5. 6. 7. 8. Chanz iili ­ ay 83 mb 0002 nje nishati taoyN za :o a chaid aa ch F. dh isi MI pin bi ki I an vifuatavy ya hal DINA UUK o zo gona MA W UIF OTAPAY katika 8 mauz 2 9 6 9 1 gevi iwk 0.1 0. 1. 1. 1.0 0.1 4.8 1 6 7 2. 5.2 6 hwas 0. 3. wa 25 an na IBRAHU IA 4 04 20 MIILSA AFIAT chapi ku ingis ayo wa LA m asilimia m na a IH kw uala itokan azi NCAYE PDG zilizo 3 7 9 2 9 1 2 7 ang faida NJA YAAI 32. 11. 11. 11 19 3.2 3.5 5.21 16. 3.62 20 1.8 47. 10. 4.6 6.8 18. 15. ndaliwaa madini ay ay imali a W UZOY MILISA ime za C) mluj jumla rasil ya au la NAAY 05 (ROS rasilimali zao NIIDA 20-0 AYAL nchi siri na pato ya na ma MA WINA 200AKA MUJAY 5. 1. 7. 4. 7. 3 e 79 39 52 33 87 7. .421 1.93 4. 53 2.15 9. 8. 6. 2. 8. 9. 3. 59 50 77 87 za 27 29 67 50 boni ua nj sawa W IA ma dini STA MA ni W WK MIILSA EJNARAH ala dini ASIB ma an - o 00 haidrokaeyne ma na yo uzauk shati ni 20AKA PDG kw na wa 6 4 viwang o u asilia. W MA YAAI 20. 6.1 4.2 .20 3.0 9.2 9.1 6.5 2.0 wa tajiri WKINIDA MILI ni yatokana anayk sieg AS lizia a ot ito Upunguf na paa ad MAY ANIZ kuw m waang ua fai au nia.uD ghafi, OTAPA HAAYAL uliwa kwa ya 5. 5 8. 9 9. 8 6. /an na/ mafuta, MADINI MA 62 6. 17 7.0 7.1 2.8 5. 17 0. 13 ni boni A KW WINATSA MUJAYAI dhafe hwa.si nkieB wea TOAPA ya zinazochuk kao boa m W 0052 IMILSA chap vya M YA zotei idrah rokd ya hai ripoti haija kaa [*] C nch za za 25. a sa a ilihda oeledn ma a TAJIRI ROS hi hisa uf mae e a uish a uish aw nyota wuk wa wa asilimi e ajum au u ajumn NCHI a ny ha lin muishu viashiria I A.2 dhef,ub mayaa ze s ak A.1 Wastani 2 005 Wastani angala kij ya a.k nye ya a hs ahdef m, nchi o ha in ALI taop, uba a, mun i. ii. pat ozel W INID u u abhs,u atlp,u Kwa [**]inao dwalieJ Ma Mae iliyotumi u isa isa ab ab isa ahhd a a, isa ab ab ab 1. 2. 3. 4. JED MA mlA abahS m Al ahhD mula/eitxuaB dha,abahs,niT teahpso Ph ahhD m um Al Ch abhS mlA ahhD ubahahD elitur,eitxuab,isa mlA ahhD ahhD aba Sh KIAMBATISHO B: MCHAKATO WA KUHALALISHA EITI 84 UFUPISHO WA MCHAKATO WA UHALALISHAJI WA EITI NA VIASHIRIA VYAKE (UFUPISHO HUU UNATOKANA NA "Muongozo wa uhalalishaji EITI" uliotolewa chini ya msaada wa Bodi ya EITI. TAHADHARI MUHIMU: Huu ni ufupisho wa muongozo wa uhalalishaji na viashiria vyake. Ni muhimu kusoma muongozo wa uhalalishaji na viashiria vyake na jedwali la ukaguzi kwa undani, kwa kuwa ufupisho huu umeandaliwa kumrahisishia msomaji sio maandiko ya topiki nzima. Mchakato wa kuhalalisha EITI Kongamano la EITI la Oktoba, 2006 lilipitisha utaratibu wa uthibitishaji, ambapo nchi zote za EITI zitahitajika kupitia (na kuingia gharama) ya uthibitishaji huo ­ kwa angalau kila baada ya miaka miwili. Wakati wa uandishi wa ripoti hii makundi machache ya kwanza yalikuwa kwenye mipango ya kuzindua uthibitishwaji wa kwanza wa EITI. Mchakato wa uthibitishaji uliokubalika unajumuisha mpangilio ulioelezea bayana na viashiria vilivyomo kwenye "Muongozo wa Uthibitishaji wa EITI" uliochapishwa chini ya msaada wa Bodi ya EITI. Muongozo wa uthibitishwaji uliokamilika umejumuishwa kwenye CD kama kiambatisho I. Hapa chini ni maelezo mafupi ya mchakato wa uthibitishwaji na ufupisho wa viashiria uthibitishwaji. Madhumuni ya mchakato wa uthibitishaji ni: 1. Kutoa kipimo cha maendeleo kwa nchi ambazo ziko kwenye mchakato wa kutekeleza EITI lakini bado hazija kamilisha utekelezaji. 2. Kutoa ukaguzi wa kujitegemea kwa nchi ambazo zimekamilisha utekelezaji wa EITI, kama mchakato wa EITI wa nchi hiyo unatimiza taratibu kufuatana na kanuni na vigezo vya EITI. 85 Mchakato huu unategemewa kutoa watekelezaji wazuri wa EITI kwa ukaguzi wa kujitegemea au kama au nchi hizo zimetimiza kiwango cha kimataifa cha uwazi na uwajibikaji ­ yaani kigezo cha EITI. Kwa kutegemea utaratibu wa uthibitishwaji, inategemewa kuwa na makundi mawili ya nchi za EITI: 1. Nchi tahiniwa ni zile ambazo zimejiunga kutekeleza EITI lakini bado hazija maliza mzunguko mzima wa kuripoti EITI. Ili kuweza kukubalika kama nchi tahiniwa ya EITI, serikali inahitaji kukamilisha walau viashiria uthibitishwaji vifuatavyo: a. Itoe tamko rasmi la dhumuni lake kujiunga na EITI b. Kujitoa kufanya kazi na vyama vya kijamii na makampuni kwenye utekelezaji wa EITI c. Kuteua kiongozi wa ngazi ya juu kuongoza utekelezaji wa EITI (kiongozi wa EITI) d. Kuwa na mpango wa kazi ambao umechapishwa na unapatikana. Mpango wa kazi utatakiwa ujumuishe malengo yanayopimika, ratiba ya utekelezaji na ukaguzi wa vikwazo vya kiuwezo. 2. Nchi zinazotimiza EITI ni zile ambazo zimetekeleza EITI. Zimetimiza viashiria vyote vilivyo kwenye muongozo wa uthibitishaji, ikijumuisha ushapishaji na usambazaji wa ripoti za EITI. Jukumu la mchakato wa uthibitishwaji ni kuruhusu usambazwaji wa wazi baina ya nchi zilizopitisha EITI na ziko kwenye mchakato wa utekelezaji (walau viashiria vya uthibitishaji 4 vya kwanza vilivyoonyeshwa hapo juu) na nchi zile zilizo tekeleza EITI pamoja na vigezo vya EITI na vimethibitishwa. Mbinu za Uthibitishaji za EITI Wakati wa kuandika, inategemewa kwanza uthibitishaji ufanywe na nchi husika na kundi kiongozi la washikadau kwa kuchagua kutoka katika makampuni ya kitaalamu yaliyopitishwa ambayo yamechunguzwa na sekretarieti ya EITI. Dhumuni ni kwa nchi kuwasiliana na moja kati ya makampuni haya na kulipia gharama moja kwa moja kuendesha mchakato wa 86 uthibitishaji kwa kutumia viwango vilivyomo kwenye muongozo wa uthibitishwaji. Kampuni la kuthibitisha litapitia taratibu na nyaraka zote za mchakato wa EITI wa nchi husika (kwa mfano, mpango wa kazi, ripoti za EITI na litakutana na washikadau muhimu wote wanaojihusisha na utekelezaji wa EITI katika nchi husika. Kampuni la uthibitishaji pia litapitia kiwango cha uhusishwaji cha makampuni na vyama vya kijamii kwenye mchakato wa EITI. Muongozo wa uthibitishaji unaonyesha kuwa kampuni la uthibitishaji litaandaa nakala za ripoti ya uthibitishaji inayo jumuisha ripoti juu ya maendeleo na ukaguzi wa jumla wa utimizaji au na viashiria muongozo wa uthibitishwaji. Nakala hizi zitatakiwa zitolewe kwa serikali na makundi viongozi ya washikadau, na kwa Bodi ya EITI. Mara baada ya kupitiwa na kuondoa mapungufu yote ya tafsiri, ripoti ya uthibitishwaji ichapishwe kwa nchi husika, na iwekwe kwenye tovuti ya kimataifa ya EITI. Muongozo wa uthibitishaji pia unatamka kuwa kama mthibitishaji akipendekeza kuondolewa kwa nchi kwenye EITI, Bodi ya EITI itabidi ifanye maamuzi. Mwisho muongozo wa uthibitishaji unahimiza nchi kupitia mchakato wa uthibitishwaji mara kwa mara, walau kila baada ya miaka miwili. Pia inahimiza nchi kufikiria kuhusu viashiria uthibitishwaji mapema wakati wa kuanza programu ya EITI kwa sababu zinatoa viwango bayana vya utekelezaji wa EITI na njia fanisi ya kuusimamia mpango wa kazi wa EITI katika viashiria uthibitishwaji tofauti wa muongozo wa uthibitishwaji kuhakikisha utimizaji wa muongozo wa uthibitishwaji. Viashiria Uthibitishwaji vya EITI Muongozo wa uthibitishwaji EITI unatengeneza viashiria maendeleo ambavyo vitakaguliwa na uthibitishwaji. Viashiria hivi vinafupishwa hapo chini (hivyo vilivyowekewa nyota vina jedwali la ukaguzi la viashiria vya undani lililotolewa kwenye "Viashiria uthibitishwaji vya EITI": Kujiandikisha 1. Serikali imetoa tamko lake rasmi na la uhakika kuhusu dhumuni lake la kutaka kujiunga na EITI? 87 2. Je Serikali imeahidi kufanya kazi na vyama vya kijamii na makampuni wakati wa utekelezaji wa EITI? 3. Je serikali imeteua kiongozi wa ngazi ya juu wa kuongoza utekelezaji? 4. Je mpango wa kazi wenye gharama zote umechapishwa na kupatikana sehemu zote, ukijumuisha malengo yanayopimika, ratiba ya utekelezaji na ukaguzi wa vikwazo vya uwezo wa (serikali, sekta binafsi na vyama vya ushirika)*? Maandalizi 5. Je serikali imeanzisha kundi linalo jumuisha washikadau mbali mbali la kusimamia utekelezaji wa EITI? 6. Je vyama vya kijamii vinahusishwa kwenye mchakato? 7. Je makampuni yanahusishwa kwenye mchakato? 8. Je serikali imeondoa vikwazo vyote vya utekelezaji wa EITI? 9. Je mfumo wa kuripoti umekubalika? 10.Je kamati ya washikadau imekubaliana na uteuzi wa kampuni ya ukaguzi/ usimamizi wa data? 11.Serikali imehakikisha kuwa makampuni yote yatatoa ripoti? 12.Je serikali imehakikisha kuwa ripoti za makampuni zinategemea kwenye mahesabu yaliyo kaguliwa katika viwango vya kimataifa? 13.Je serikali imehakikisha kuwa ripoti za serikali zinategemea kwenye mahesabu yaliyokaguliwa katika kiwango cha kimataifa? Ufichuaji 14.Je malipo yote muhimu ya mafuta, gesi na uchimbaji madini yaliyolipwa kwa serikali toka kwa makampuni yaliwekwa bayana kwa kampuni liliyopewa mkataba wa ukaguzi na kutengeneza ripoti ya EITI? 15.Je mapato yote muhimu ya mafuta, gesi na uchimbaji madini ya serikali toka kwa makampuni yalifichuliwa kwa kampuni ilyopewa mkataba wa kukagua mahesabu na kutengeneza ripoti ya EITI? 16.Je kundi la washikadau liliridhika kuwa kampuni iliyopewa mkataba wa kukagua mahesabu ya serikali na makampuni ulifanya hivyo kwa utimilifu? 88 17.Je ripoti ya EITI iligundua mapungufu na kuweka mapendekezo ya nini kinatakiwa kufanyika? Mtawanyiko 18.Je ripoti ya EITI iliwekwa wazi kwa umma katika namna yeyote ile · Kufikika na umma · Yenye mambo mengi na · Inayoeleweka Uthibitishwaji wa Kampuni. Ni jinsi gani makampuni ya mafuta, gesi na uchimbaji madini yaliunga mkono utekelezaji wa EITI?* Mapitio. Ni hatua zipi zimechukuliwa kutendea kazi mafundo yaliyopatikana, kuwasilisha mapungufu, na kuhakikisha kuwa utekelezaji wa EITI ni endelevu?*n 89 KIAMBATISHO C: SAMPULI YA MATOKEO YA MFUMO WA UPIMAJI WA EITI (NA VIASHIRIA) 90 NA na ya nia ka wa tasnia tas SHOI Uwazi zaidi ya MW AY ITIE kta ulioongeze usimamizi kwa se katikaika 91 YA mazuri a na ma. kaez kw jumla um OKEO utawala uziduaji zajiek wa za uziduaji dha MAT MALENGO Kuonge uwajibikaji ya Mazingira uwe ya Ubora kwa fe YA ivyo cha (na vil waze kae OKEO IT sh MAT ulioongI kiwango vya FD kwa kukope viwango) AIRI wa kaez wa cha SHOI shwa bora ASHIV AI MW Viwango bore CP Mtirirko Kuonge nchi wakala na ya e e OKEO oele na kwa ny ny ya inayo ITIE ndani nd eynewk ITIE F ye yapo za MAT haraka kazi na kupunguza MDT (ukaguzi) ITIE nchi kwe ,utaw( kwenye na kodi ­ misingi kama ITIE usishwah mae ya ti ...... TA za ya ya uvle F ya na kukamilika i wa ya I juu za o ti. ez dene na ripo YA MDT hasa e mipango em NCH chapishwa baje ny egt IT ria) BUI HARAKA ZAI Zinawe matoke nchi Ni fadhiliwa mafanikio ya Nchi u ufadhili misaada ZAI Ripoti zinaridhisha Makubaliano mapana Ubora makusanyo Uthibitishwaji uliofanikiwa EI ufadhili she Mitazamo mapungufu yaliyoripotiwa, kwe zilizo MJ YA KAZ · · · KAZ · · · · · · A RI NA wa HISA zilizo ITIE ya kazi VI iriki KAI mambo yaliyounda kaez ughuli wa kwa bitishwa ge MAENDELEO F sh ripoti wash KATI maagizo on kuteuliwa thi NI ya mkono wa ime ume NI MAJE MDT ya NCH ZAI dadiI Mrishonyuma watumiaji dadiI ungwa Ubora ZAI Kutoa kukamilika MSWG kukamilika Mpango kukubalika Kiongozi Ripoti Ubora NI MAENDELEO T UNAPI KAZ · · · · KAZ · · · · · · LII la na KWA kwa wa kwa wa AY TFD mkono ZIAK OKEO umma ngazi ITI M wa E AZ WAIKI dha ITIE kufikia taarifa maofisa MAT kife AY A ITIE kwa na dhumuni ndaliwa kazi ZIAK KUFAID AY oze za kwa ya na mteule ni Kiutaalamu ija uchapishwaji OG IKIF ya iliyoa wa uw wa ezel ANP kuongoza ya MI NI I rikali NI rikali juu NI OKEO nga ekt Kampe umma Mafunzo se Kuunga u Misaada ajili ripoti KUILII NI ITIE Matangazo juu se MSG washiriki Mpango Kiongozi ya NI KUSA MAT Kuje - - Msaada - - NI NCH YA Kujiandikisha - - - - Ripoti (3 ogne an ya wa laa wa ya vya IDF COI ihcn wa wa oej M aw lia vya o : aw laaw PF a) Mal za a mare og 92 ­ azi ktaes mijad RANGI uw na waeleu tasnia ogna o taik ch jan oze rasilim ya uw an ho ay ajiz viw wa eke ujaz dini uziduaji ogna ishwp (wakala Uwa (CAS; na shwa) viw cha bari ma lia a mtawanyik NA wa toa azi Uw kai ya kiw ak pko )o ­ TI Mwis tikaak yene bore kw futaa kai kwa ha miziuta a rikes EI AN map m kw uw ya kat ya o o minifuau za she mi m zilizos kw a TI utawala ya iliyo ka kat oekot aji aw vya wa na wa za kope vy EI ya ze mia ini. o ITIE wah ob aroB dilik u ku eshar kati ge 9data duaji dilik atik ITIE uma hwajisero ma uaji ba ra ba tasniaeyn nyumba a ya mad dilik A m pangoi Ma ya res uwajibik Uzi Upana vyom ya Ub u uzid Ma mka ngi Ma kwe uvgN za kw kaerobuK cha viwango kubo M zaidi mika onuK kusima za Ma CPI zia KUFUATA 3. Kubo - - - M - - - Zaidi - - - TIIE a a i wa ch na a az panga ku CHINI, zi Ka na ITIEeyne vy uish um toaka GAA ikij ogna kaitak mising si madini ota ge na si/ ayv vyama mch kiw ta, ge / wa ay kw ka HAPO aka ya mamiais zi)u mp uadaki map ITIE miniah mafu tau katiis kai an ngoawiv ud kat di aw maf ahdeifk Har ku MDTF nchi ashw ITIEeyn ko atiinI­ ya kwe ufani jamii ni umiato wa ya oe aw (ukagITIE ya watu,­ wa zina i an a a.ni uvele saidia a kw mpuni azh ikiwanafe ayv ha a kikanu ok awzenegn VIASHIRIA PULI Mt FT oz ku chN wana dha.fe te aw wa kodi. S ndeu A ­ weu aw ufadhili a pan o vueledne mayv wa a ya zime NOC o na MD O na waIT ma maka fikiwa ad makusanyo umITIE ya KW SAM na A TIIE mfumo na EI wai a oze zoe kwa akath an anzuk ini ya mc na ha aw dann wa niITIE uw d aw uw wa TIIE RI ya uz azi ya mii. IT vimeIT o kusimami wa borek awb MIFUM a fu kaz vy vya za iar ish zo a maija wa TOKA ASHI arhd ilihdafo akez kija EI kue yai EI an a aji a aw ota ku kat kuondoka ku aw wa bali oz o ku zo i do matamkoeyn A W ZAI geno VI uwe Ma zilil Ku mika Nchi hicN dhi hwajiser zili go kat Ma vyama Uhusishw Vige nchi potiR in kishe si mbihc kur ubo mt Uthibitishwaji Mchak ya Kuimarish u Uimarishwaji + idadI kwe Uimarishwaji kijamii pan 2. - - - M Mcha - - - - - - - Taasi - - - - ULIG MPUL o )o TA ni TF an SA ziliz CHA wai MD ywa"n zi fik mpang kwa ay ofa DOANO Ka waleo ku ­ na mmau na a FT TIIE QAQ ufanisi chukuliwa mua "uli e awzeleke kut i ot VILIVYO KU MD ezowu vya o nz nisha ya a iliyo ogr guzi nyle unp jirani. vy pr ay ajili ya (uka NA)AJO ya wa taarifa mafu uad in utawala ma nchi kuling o ya ziak matumizi kazi mak / nzieju a vya a wa kwa ar )u ubora sampuli keo TIIE ya na aw M ya ubora o/warsh mafunzoeyn (kwa ziada sab a u mat wa ikahsaw og iar ubo zi ju wa ka la mara. she o VIASHIRIA: ya le jamii,ik vituoeyn TF vy kama kuhusish ya vya kwe mahe­ aw aw nki, ya ik j )e ya kwa mipan ziog an kiiri YA KILA den wa u liu 4 imiozaa vya amang kwe lipoa be aki wan go a" dajin raa kion nie TI agizo m ufadhili wangoiv mae wenzo an uh jia yw ute m EI za shu ma NO aw aalam m ika maazimio adhili a ua a pan a a ika shugh ar makon washiriki wag matukio uf vy wa ya vy m al kazi sh ria ini kit ya vyama ya ofan yai ar ya ya ya ya ya at m wa bu ya u wa id wa shaez ak MIFA MPAKA ashiiV pitio "usi dhak dha daa adidI dhak o Maji Na nz adidI adidI adidI adidI jiba zi M Viwango Rasilimali (Uwiano aro Ma zilizofanywa (QAG) Vipin (uthaminish au Kundi linalokutan Mik Kuwe kaewuK kikiahuK Na fua 1. 1. Msa - - - M - - - - - Mtiririko - - - Ub - - Ukagu - - - - - - KIAMBATISHO D: NYENZO MUHIMU 93 Tovuti ya Taifa na Kimataifa ya EITI Tovuti ya kimataifa ya EITI: http://www.eitransparency.org Serikali ya Azerbaijan (kwa Kingereza na Kiazerbaijani): http://www.oilfund.az/ Serikali ya Gabon (kwa kifaransa): http://www.eitigabon.org/FRAN/index.htm Serikali ya Ghana (in Kingereza): http://www.geiti.gov.gh Serikali ya Kazakhstan (Kwa Kirusi, na baadhi ya Kikazakh and Kingereza): http://www.eiti.kz Serikali ya Liberia: http://eitiliberia.org/ Serikali ya Mauritania: http://www.mauritania.mr/itie/ Serikali ya Mongolia (kwa Kimongolia na Kingereza): http://eitimongolia.mn/ Serikali ya Nigeria: http://www.neiti.org/ Serikali ya: (Kwa Kihispania): http://www.minem.gob.pe/eiti/default.asp Nyenzo kwa ajili ya Makundi ya vyama vya kijamii Muungano wa Chapisha unacholipa : http://www.publishwhatyoupay.org Uangalizi wa mapato: http://www.revenuewatch.org Uwazi Kimataifa: http://transparency.org/ (tovuti ya dunia -- tovuti ya nchi pia ipo) Mashahidi Kidunia : http://www.globalwitness.org/ Tovuti za Benki ya Dunia Tovuti ya Benki ya Dunia ya Idara ya mafuta, gesi, uchimbaji madini na madawa: http://www.worldbank.org/ogmc Tovuti ya Benki ya Dunia ya EITI: http://www.worldbank.org/eititf Machapisho Yaliyochaguliwa Sekretarieti ya EITI 2006. "Muongozo wa Uthibitishwaji wa EITI" unaelezea mchakato wa uthibitishwaji. Unaainisha na kuelezea vigezo vya uthibitishwaji vitakavyotumika kila baada ya miaka miwili kutoa kipimo cha maendeleo cha kujitegemea kwenye nchi zinazotekeleza EITI. Inaweza kupatikana kwenye: http://www.eitransparency.org/document/validationguide. EITI Secretariat. 2005. The "EITI Source Book" outlines the EITI Principles and Criteria and provides guidance on implementation of the Initiative and some examples of how EITI has been implemented in various countries. It can be found at http://www.eitransparency.org/document/sourcebook. Global Witness. 2007. Oil Revenue Transparency: A Strategic Component of U.S. Energy Security and Anti-Corruption Policy. London: Global Witness. Global Witness. 2005. Making It Add Up: A Constructive Critique of the EITI Reporting Guidelines and Source Book. London: Save the Children/Global Witness. 94 Global Witness. 2004. Time for Transparency: Coming Clean on Oil, Mining and Gas Revenues. London: Global Witness. Goldwyn, D. L., and J. S. Morrison, ed. 2004. Promoting Transparency in the African Oil Sector: A Report of the CSIS Task Force on Rising U.S. Energy Stakes in Africa. Washington, DC: Center for Strategic and International Studies. Insight Investment. 2005. A Discussion Paper on Revenue Transparency. London: Insight Investment. International Monetary Fund. 2007. Resource Revenue Transparency Guide (available in Arabic, Chinese, Spanish, French, Portuguese, and Russian). Washington, DC: International Monetary Fund. Open Society Institute. 2005. Follow the Money. A Guide to Monitoring Budget and Oil and Gas Revenues. New York: Open Society Institute. Publish What You Pay. 2005. Extracting Transparency: The Need for an International Financial Reporting Standard for the Extractive Industries. London: Global Witness. Rosser, Michael. 2006. The Political Economy of the Resource Curse: A Literature Survey. IDS Working Paper 268, Centre for the Future State, Institute of Development Studies, Brighton, United Kingdom. Save the Children. 2005. Beyond the Rhetoric: Measuring Revenue Transparency in the Oil and Gas Industries. London: Save the Children. Save the Children. 2003. Lifting the Resource Curse. London: Save the Children. Soros, George, Macartan Humphreys, Jeffrey D. Sachs, and Joseph E. Stiglitz. 2007. Escaping the Resource Curse. New York: Columbia University Press. Transparency International. 2007. 2007 Corruption Perceptions Index. London: Transparency International. World Bank. 2004. Striking a Better Balance--The World Bank Group and Extractive Industries: The Final Report of the Extractive Industries Review, WorldBank Group Management Response. Washington, DC: World Bank. World Bank. 2003. The World Bank Group and Extractive Industries: The Final Report of the Extractive Industries Review. Washington, DC: World Bank. 95 Kundi la Benki ya Dunia Mkakati wa kuongeza Uwazi katika Tasnia ya Uziduaji (EITI) "Utekelezaji wa EITI ­ Matumizi ya Mafunzo ya Awali kutoka kwenye maeneo ya kiutendaji" Orodha ya Viambatisho (Nyaraka zilizo katika mfumo wa elektroniki ­ CD iliyoambatanishwa) Kiambatisho A: Dondoo toka kwenye Hadidu za Rejea za utafiti wa awali wa EITI ­ Zambia Kiambatisho B: Waraka wa maelewano juu ya utekelezaji wa EITI ­ Azerbaijan Kiambatisho C: Mpangilio wa EITI ­ Guinea Kiambatisho D: Agizo kwa kundi tekelezi la washikadau ­ Peru Kiambatisho E: Dondoo toka kwenye Ripoti ya awali ­ Ghana Kiambatisho F: Mpango wa kazi wa EITI ­ Timor Leste Kiambatisho G: Hadidu za Rejea za halmashauri ya EITI ­ Mongolia Kiambatisho H: Sheria ya EITI (Uzalishwaji wa marudio ­ Nigeria Kiambatisho I: Sapuli ya Hadidu za Rejea kwa ajili ya msimamizi wa EITI ­ Cameruni Kiambatisho J: Sampuli ya kiolezo cha ripoti za EITI ­ Ghana (Uchimbaji madini) na Kazakhstan (mafuta) Kiambatisho K: Kitabu cha marejeo cha EITI Kiambatisho L: Muongozo wa Uthibitishwaji wa EITI Kiambatisho M: Sampuli ya Ripoti za EITI zilizochapishwa hivi karibuni kutoka Novemba 1, 2007 a. Azerbaijan b. Cameruni c. Gaboni d. Ghana e. Guinea f. Jamuhuri ya Kyrgyz g. Mauritania h. Nigeria 96 VIELEZO A H Australia, I Azerbaijan, X, 13, 78, 80 hadidu za rejea, 4, 12, 13, 14, 15, 8, 32, 41, 42, 43, 47, 50 B hasara, 2, 13 hatari, 2, 8, 17, 18, 52, 59 Benki ya Dunia, I, V, XI, XII, xv, xix, xx, 4, 5, 9, 5, 27, hatua za kujiunga, 5 57, 60, 66, 67, 78, 80 Hispania, I Benki ya Dunia Cammeroon Faustin - Ange Koyasse, XI J Bodi, I, II, XII, XIII, xix, 5, 9, 16, 55, 57, 69, 71 Bodi ya EITI, xix, 55, 71 Jamuhuri ya Kyrgyz, X, 80 C K Cameruni, 80 Kiongozi wa timu Canada, I Anwar Ravat, XI changamoto, 13, 17, 30 Kongamano, xvii, 14, 57, 69 Charles McPherson kufikia malengo, 59 Shirika la Fedha Duniani, XI kujenga mazingira, 2 Clive Armstrong kukubaliana, 6, 13, 15, 40, 48, 55, 59 Umoja wa Fedha Duniani, XI kundi kiongozi, 11, 12, 13, 14, 15, 16, 24, 30, 31, 33, 35, 39, 41, 43, 44, 47, 53, 70 D kupambana na rushwa, xx, 3 kuratibu, I, 6, 14 DFID ­ Siera Leon kurekebisha, xx, 6, 10, 31 Allison George, XI Dunia, I, V, XI, xix, 4, 57, 63 M E mabenki ya maendeleo ya kanda, 5 madini, I, II, IX, X, XI, xv, xvi, xviii, 1, 3, 6, 8, 9, 10, 11, EITI, I, II, IX, X, XI, XII, XIII, XIV, xv, xvi, xvii, xviii, 2, 3, 6, 8, 10, 16, 17, 18, 19, 26, 35, 37, 42, 47, 48, 51, xix, xx, 1, 2, 3, 4, 5, 6, 7, 8, 9, 10, 11, 12, 13, 14, 15, 16, 55, 58, 62, 66, 67, 72, 73, 76, 78, 80, 85 1, 2, 3, 4, 5, 6, 7, 8, 10, 11, 12, 13, 14, 16, 17, 18, 19, 22, maendeleo, I, XI, XIII, xvii, 2, 5, 7, 8, 9, 14, 15, 14, 26, 23, 24, 26, 27, 28, 29, 30, 31, 32, 33, 34, 35, 36, 37, 38, 31, 42, 57, 62, 66, 67, 69, 71, 75, 76, 78 39, 40, 41, 42, 43, 44, 45, 46, 47, 48, 49, 50, 51, 52, 53, maendeleo endelevu, XI, xvii, 2 55, 56, 57, 58, 59, 60, 61, 62, 68, 69, 70, 71, 72, 73, 74, mafuta, I, II, IX, X, XI, xv, xvi, xviii, 1, 3, 6, 8, 9, 10, 11, 75, 76, 78, 80, 85 12, 2, 3, 6, 8, 10, 16, 17, 18, 19, 26, 35, 37, 42, 47, 48, 51, 58, 62, 66, 67, 72, 73, 76, 78, 80, 85 G majedwali, 50 Majimbo, 13 Gaboni, X, 80 makamapuni, XIV gesi, I, II, IX, XI, xv, xvi, xviii, 1, 3, 9, 10, 11, 2, 3, 6, 8, makusanyo ya mapato, xv, 8, 10 10, 16, 17, 18, 19, 26, 35, 37, 42, 47, 48, 51, 58, 62, 66, malengo ya EITI, 55, 57 67, 72, 73, 76, 78, 85 malengo ya ziada, 57 Ghana, X, 3, 48, 78, 80 maliasili, xvii, 2, 8 gharama, 2, 5, 7, 3, 6, 7, 8, 10, 11, 12, 17, 18, 24, 27, 28, malipo na mapato ya nchi, 1 31, 35, 40, 41, 42, 44, 46, 61, 69, 70, 72 mapato na matumizi ya taifa, xviii, 2 GTZ ­ Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo Mauritania, X, 78, 80 Kristian Lempa, XI mawakala wa serikali, 1, 31 Guinea, X, 80 mawasilino, 50, 56 97 mchakato, IX, XIII, XIV, xv, xvi, xvii, xviii, 6, 8, 9, 10, sekta, 1, 2, 3, 6, 8, 10, 11, 1, 2, 3, 10, 16, 17, 18, 19, 26, 11, 14, 15, 16, 1, 2, 3, 5, 6, 7, 8, 10, 11, 12, 16, 17, 18, 42, 46, 59, 62, 72, 75, 76 22, 23, 24, 26, 27, 30, 31, 32, 33, 34, 35, 36, 37, 38, 39, sekta zingine, 59 41, 43, 44, 46, 49, 50, 51, 52, 53, 55, 56, 57, 59, 60, 61, sera, II, xv, 13, 19, 55, 56, 57 62, 69, 70, 71, 72, 76, 78 serikali, I, II, V, IX, XII, XIV, xv, xvii, xviii, xix, xx, 1, 2, Meneja wa Programu 3, 4, 5, 6, 7, 8, 9, 10, 11, 12, 14, 15, 16, 2, 3, 5, 6, 7, 8, Anwar Ravat, XI 11, 13, 14, 15, 16, 17, 18, 22, 23, 24, 26, 27, 28, 30, 31, migogoro, 2, 42, 60 32, 33, 34, 35, 36, 37, 39, 40, 41, 42, 43, 46, 47, 48, 49, mjadala, xviii, 13, 47, 50, 55, 61 51, 52, 55, 58, 59, 60, 61, 62, 70, 71, 72, 75, 76, 85 mkakati, I, II, XII, xvii, xix, xx, 2, 4, 5, 6, 7, 8, 10, 12, 14, Shirika la fedha Duniani, 5 6, 13, 16, 17, 18, 23, 24, 26, 27, 30, 32, 33, 34, 37, 51, Shirika la Fedha Duniani 52, 55, 57, 58, 60, 61, 76, 85 Anton Op De Beke, XI Mpangilio wa utendaji, 6 mpango, IX, xviii, 7, 15, 5, 19, 22, 23, 24, 27, 28, 30, 31, T 32, 46, 50, 53, 57, 70, 71, 72, 76 mpango wa kazi, IX, 15, 19, 22, 23, 24, 28, 30, 31, 46, tasnia, xv, xvii, xx, 1, 3, 10, 12, 16, 17, 19, 24, 26, 27, 30, 50, 53, 57, 70, 71, 72, 76 35, 36, 42, 51, 75, 76, 85 muongozo, II, XI, xix, 5, 15, 16, 23, 24, 30, 48, 57, 69, tasnia ya uziduaji, xv, xvii, xx, 1, 3, 10, 12, 16, 17, 24, 70, 71 30, 35, 36, 42, 51, 75, 76 Muongozo wa uthibitishwaji, II, 69, 71 Mwandishi kiongozi wa ripoti U Sefton Darby, XI mwenyekiti wa bodi ya EITI, 57 uaminifu, 1, 5, 13, 42, 45, 49, 59, 61, 76 Ubeligiji, I N uchumi, xvii, xviii, 2, 3, 5 udhaifu, 53 nchi zenye utajiri wa malighafi, xv Ufaransa, I Nchi zenye utajiri wa rasilimali, xv Uholanzi, I Nigeria, X, XI, 36, 78, 80 uhusishwaji, 10, 36, 55, 71 Norway, I, XIII, 4, 57 Uingereza, I, XI, 66 Ujerumani, I O ukosefu wa uwezo, 58 Umoja wa Ulaya, I Oslo, I, XIII, 56 usimamizi, xvii, xviii, xx, 1, 2, 8, 11, 15, 3, 10, 17, 38, 53, 57, 62, 72, 75 P usimamizi wa maliasili, xvii, xx utafiti, X, 4, 9, 16, 17, 56, 80 Paulo De Sa utajiri, I, xv, xvii, 3 Meneja, Kitengo cha utendaji na Sera, XI utaratibu, xix, 1, 7, 10, 15, 49, 69, 70 progamu, 1 Utaratibu, 1, 11, 7, 54 Programu ya EITI, 1, 14, 22, 30, 31, 36, 41, 42, 58, 61 utawala, I, IX, xv, xx, 1, 2, 3, 4, 5, 8, 3, 55, 59, 62, 75, 76, 85 R utawala bora, xv, xx, 1, 2, 3, 55, 85 utegemezi, 22, 58, 75 rasilimali, I, xv, xvii, 1, 3, 4, 2, 5, 6, 8, 17, 22, 24, 26, 27, utekelezaji, II, X, XIV, xv, xviii, xix, xx, 4, 5, 7, 8, 12, 30, 31, 32, 33, 34, 44, 56, 59, 60, 61, 66, 67, 76, 85 14, 15, 1, 3, 6, 10, 19, 22, 24, 26, 27, 30, 31, 32, 33, 34, ripoti za EITI, xv, 15, 1, 2, 3, 6, 7, 12, 27, 44, 49, 51, 53, 35, 36, 37, 38, 40, 43, 51, 55, 56, 58, 60, 61, 62, 69, 70, 58, 70, 71 71, 72, 73, 75, 80, 85 Ripoti za Kitaalamu, 15 uthaminishaji, xix, 22, 76 uthibitishaji, xix, 5, 16, 1, 18, 19, 22, 55, 69, 70, 71 S uwajibikaji, xv, xvii, xviii, 1, 2, 8, 50, 52, 59, 62, 70, 75, 76, 85 sekretarieti, I, xix, 12, 14, 15, 22, 24, 30, 32, 39, 53, 55, Uwajibikaji, 1 56, 57, 70 98 uwazi, xv, xvi, xvii, xviii, 1, 3, 10, 2, 5, 8, 12, 13, 18, 26, wadau muhimu, 4 27, 34, 35, 40, 58, 59, 62, 70, 76, 85 wahisani, I, II, XII, 27, 56, 57 uwekezaji, xv, xvii, 2, 10, 3, 26, 75 wakati mgumu, 5, 53 uziduaji, XII, XIV, xvii, xviii, xx, 2, 3, 4, 5, 8, 10, 2, 8, waraka wa maelewano, 50, 57 12, 15, 17, 31, 32, 36, 39, 48, 51, 55 warsha, 4, 32, 76 uzoefu wa kiutendaji wa kimataifa, xx washauri, xix, 27 washikadau, I, X, XIII, XIV, 1, 4, 10, 11, 12, 13, 24, 26, V 30, 31, 32, 33, 34, 35, 38, 39, 41, 42, 43, 44, 47, 50, 51, 53, 55, 56, 57, 58, 60, 61, 62, 70, 71, 72, 76, 80 viashilia, xix wasimamiwa, 59 vigezo vilivyokubalika kimataifa, 1 wasimamizi, 13, 15, 12, 31, 43, 59 Viwango, IX, XIII, 11, 46, 48, 75, 76 wataalam, xix viwango ashiria, xix Wataalam, 14 vyama vya kijamii, I, II, XII, XIV, xx, 1, 4, 5, 8, 9, 11, watahiniwa wa EITI, xix 14, 23, 24, 27, 37, 38, 39, 40, 55, 57, 59, 60, 61, 70, 71, watendaji, 3 72, 76, 78, 85 vyanzo vya fedha, 7 Z vyanzo vya mapato, 1, 2, 12, 44 vyombo vya habari, XIII, 1, 15, 32, 39, 51, 76 Zambia, X, 4, 80 W wadau, II, XIV, xvii, xviii, 1, 2, 4, 5, 6, 7, 8, 9, 10, 11, 12, 14, 15, 1, 3, 5, 6, 12, 13, 17, 18, 19, 22, 23, 27, 32, 33, 35, 50, 51, 52, 59, 60, 62 99 ECO - AUDIT Tamko la Manufaa ya Kimazingira Benki ya Dunia imeahidi kulinda misitu na maliasili Vimeokolewa: zilizokatika hatari. Ofisi ya mchapishaji imechagua Miti 5 kudurusu EITI katika karatasi zilizo tengenezwa BTU milioni 4 za nishati ya kutokana na karatasi zilizo tumika zenye asilimia 30 ya jumla ufumwele, kama ilivyopendekezwa katika viwango vya 589 lbs za kaboni dai mkakati wa Green Press, mkakati usio wa faida wa oksaidi sawa na gesi za kuhimiza uchapishaji kwa kutumia ufumwele utokanao green house na misitu isiyo hatarini. Kwa taarifa zaidi pitia Galoni 1932 za maji taka www.greenpressinitiative.org. Pauni 320 za taka ngumu 100 Mkakati wa kuongeza uwazi katika tasnia ya Uziduaji ulianzishwa kama mkakati wa kidunia mnamo mwaka 2002. Tangu hapo EITI imekuwa ndio kiwango cha juu cha kimataifa katika kutangaza uwazi na uwajibikaji kwa nchi zinazotegemea mafuta, gesi na madini. Kama jinsi inavyoundwa katika mazingira ya umoja baina ya serikali, makampuni na vyama vya kijamii; EITI imekuwa ikiitwa "Muungano wenye maswali" na baadhi. Hata hivyo, muungano huu hivi sasa unasaidia kuongeza uwazi katika malipo na mapato kwenye nchi tajiri za rasilimali duniani kote kama sehemu ya programu zao za utawala bora. Utekelezwaji wa Mkakati wa kuongeza uwazi katika tasnia ya Uziduaji unajengwa katika misingi ya mafunzo yaliyopatikana toka kwa nchi zilizoanza utekelezaji huu wa EITI mapema. CD inayojumuisha sampuli za nakala zilizotolewa katika michakato ya EITI, inawakilisha uwasilishaji. Kitabu hiki kitasaidia wale walio wapya kwenye EITI kupata miongozo juu ya hatua mbali mbali za utekelezaji wa programu ya EITI na itawafaa wasomaji wanaofanya kazi kwenye maeneo yanayohitaji uwazi; utawala na kupinga rushwa; madini, mafuta, gesi na madawa na utawala mzima kwa ujumla. 101